< Zjevení Janovo 15 >

1 Potom viděl jsem jiný zázrak na nebi veliký a předivný: Sedm andělů majících sedm ran posledních, v nichž má dokonán býti hněv Boží.
Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
2 A viděl jsem jako moře sklené, smíšené s ohněm, a ty, kteříž zvítězili nad šelmou a obrazem jejím a nad charakterem jejím i nad počtem jména jejího, ani stojí nad tím mořem skleným, majíce harfy Boží,
Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
3 A zpívají píseň Mojžíše, služebníka Božího, a píseň Beránkovu, řkouce: Velicí a předivní jsou skutkové tvoji, Pane Bože všemohoucí, spravedlivé a pravé jsou cesty tvé, ó Králi všech svatých.
Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
4 Kdož by se nebál tebe, Pane, a nezveleboval jména tvého? Nebo ty sám svatý jsi. Všickni zajisté národové přijdou a klaněti se budou před obličejem tvým; nebo soudové tvoji zjeveni jsou.
Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
5 Potom pak viděl jsem, a aj, otevřín jest chrám stánku svědectví na nebi.
Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
6 I vyšlo sedm těch andělů z chrámu, majících sedm ran, oblečeni jsouce rouchem lněným, čistým a bělostkvoucím, a přepásáni na prsech pasy zlatými.
Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
7 A jedno ze čtyř zvířat dalo sedmi andělům sedm koflíků zlatých, plných hněvu Boha živého na věky věků. (aiōn g165)
Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn g165)
8 I naplněn jest chrám dýmem, pocházejícím od slávy Boží a od moci jeho, a žádný nemohl vjíti do chrámu, dokudž se nevykonalo sedm ran těch sedmi andělů.
Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.

< Zjevení Janovo 15 >