< Žalmy 78 >
1 Vyučující, Azafovi. Pozoruj, lide můj, zákona mého, nakloňte uší svých k slovům úst mých.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Otevru v podobenství ústa svá, vypravovati budu přípovídky starobylé.
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Co jsme slýchali i poznali, a co nám otcové naši vypravovali,
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 Nezatajíme toho před syny jejich, kteříž budoucím potomkům svým vypravovati budou chvály Hospodinovy, ano i moc jeho a divné skutky jeho, kteréž činil.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Neboť jest vyzdvihl svědectví v Jákobovi, a zákon vydal v Izraeli, což přikázal otcům našim, aby v známost uvodili synům svým,
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 Aby to poznal věk potomní, synové, kteříž se zroditi měli, a ti povstanouce, aby vypravovali dítkám svým,
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 Aby pokládali v Bohu naději svou, a nezapomínali se na skutky Boha silného, ale ostříhali přikázaní jeho,
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 Aby nebývali jako otcové jejich, pokolení zpurné a protivné, národ, kterýž nenapravil srdce svého, a nebyl věrný Bohu silnému duch jeho.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 Jako synové Efraim zbrojní, ač uměle z lučiště stříleli, však v čas boje zpět se obrátili,
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 Nebo neostříhali smlouvy Boží, a v zákoně jeho zpěčovali se choditi.
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 Zapomenuli se na činy jeho, a na divné skutky jeho, kteréž jim ukázal.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Před otci jejich činil divy v zemi Egyptské, na poli Soan.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 Rozdělil moře, a převedl je; učinil, aby stály vody jako hromada.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Vedl je ve dne v oblace, a každé noci v jasném ohni.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Protrhl skály na poušti, a napájel je jako z propastí velikých.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Vyvedl potoky z skály, a učinil, aby vody tekly jako řeky.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 A však vždy přičíněli hříchů proti němu, a popouzeli Nejvyššího na poušti.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 A pokoušeli Boha silného v srdci svém, žádajíce pokrmu podlé líbosti své.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 A mluvili proti Bohu, řkouce: Zdaliž bude moci Bůh silný připraviti stůl na této poušti?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Aj, udeřilť jest v skálu, a tekly vody, a řeky se rozvodnily. Zdali také bude moci dáti chleba? Zdali nastrojí masa lidu svému?
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 A protož uslyšav Hospodin, rozhněval se, a oheň zažžen jest proti Jákobovi, a prchlivost vstoupila na Izraele,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 Proto že se nedověřili Bohu, a neměli naděje v spasení jeho,
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Ačkoli rozkázal oblakům shůry, a průduchy nebeské otevřel,
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 A dštil na ně mannou ku pokrmu, a obilé nebeské dával jim.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Chléb mocných jedl člověk, seslal jim pokrmů do sytosti.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 Obrátil vítr východní u povětří, a přivedl mocí svou vítr polední.
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 I dštil na ně masem jako prachem, a ptactvem pernatým jako pískem mořským.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Spustil je do prostřed vojska jejich, a všudy vůkol stanů jejich.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 I jedli, a nasyceni jsou hojně, a dal jim to, čehož žádali.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Ještě nevyplnili žádosti své, ještě pokrm byl v ústech jejich,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 A v tom prchlivost Boží připadla na ně, a zbil tučné jejich, a přední Izraelské porazil.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 S tím se vším vždy ještě hřešili, a nevěřili předivným skutkům jeho.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 A protož dopustil na ně, že marně skonali dny své, a léta svá s chvátáním.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Když je hubil, jestliže ho hledali, a zase k Bohu silnému hned na úsvitě se navraceli,
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 Rozpomínajíce se na to, že Bůh byl skála jejich, a Bůh silný nejvyšší vykupitel jejich:
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 (Ačkoli mu s pochlebenstvím mluvili ústy svými, a jazykem svým lhali jemu.
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 A srdce jejich nebylo upřímé před ním, aniž se věrně měli v smlouvě jeho),
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 On jsa milosrdný, odpouštěl nepravosti jejich, a nezahladil jich; častokrát odvracel hněv svůj, a nevzbuzoval vší zůřivosti své.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Nebo pamatoval, že jsou tělo, vítr, kterýž odchází, a nenavracuje se zase.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Kolikrát jsou ho dráždili na poušti, a k bolesti přivodili na pustinách.
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Týž i týž navracujíce se, pokoušeli Boha silného, a svatému Izraelskému cíle vyměřovali.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 Nepamatovali na moc jeho, a na ten den, v kterémž je vysvobodil z ssoužení,
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 Když činil v Egyptě znamení svá, a zázraky své na poli Soan,
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 Když obrátil v krev řeky a potoky jejich, tak že jich píti nemohli.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Dopustil na ně směsici žížal, aby je žraly, a žáby, aby je hubily.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 A dal chroustům úrody jejich, a úsilí jejich kobylkám.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 Stloukl krupami réví jejich, a stromy fíkové jejich ledem.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 Vydal krupobití na hovada jejich, a na dobytek jejich uhlí řeřavé.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Poslal na ně prchlivost hněvu svého, rozpálení, zůřivost i ssoužení, dopustiv na ně anděly zlé.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 Uprostrannil stezku prchlivosti své, neuchoval od smrti duše jejich, ano i na hovada jejich mor dopustil.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 A pobil všecko prvorozené v Egyptě, prvotiny síly v staních Chamových.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 Ale lid svůj vyvedl jako ovce, a vodil se s nimi jako s stádem po poušti.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Vodil je v bezpečnosti, tak že nestrašili, nepřátely pak jejich přikrylo moře,
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 Až je přivedl ku pomezí svatosti své, na horu tu, kteréž dobyla pravice jeho.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Vyhnav před tváří jejich národy, způsobil to, aby jim na provazec dědictví jejich přišli, a aby přebývala v staních jejich pokolení Izraelská.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Však vždy předce pokoušeli a dráždili Boha nejvyššího, a svědectví jeho neostříhali.
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Ale zpět odšedše, převráceně činili, jako i předkové jejich; uchýlili se jako mylné lučiště.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Nebo popouzeli ho výsostmi svými, a rytinami svými k horlení přivedli jej.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Slyšel Bůh, a rozhněval se, a u velikou ošklivost vzal Izraele,
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Tak že opustiv příbytek v Sílo, stánek, kterýž postavil mezi lidmi,
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Vydal v zajetí sílu svou, a slávu svou v ruce nepřítele.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Dal pod meč lid svůj, a na dědictví své se rozhněval.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Mládence jeho sežral oheň, a panny jeho nebyly chváleny.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Kněží jejich od meče padli, a vdovy jejich neplakaly.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Potom pak procítil Pán jako ze sna, jako silný rek, kterýž po víně sobě vykřikuje.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 A ranil nepřátely své po zadu, a u věčné pohanění je vydal.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Ačkoli pak pohrdl stánkem Jozefovým, a pokolení Efraimova nevyvolil,
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Však vyvolil pokolení Judovo, horu Sion, kterouž zamiloval.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 A vystavěl sobě, jako hrad vysoký, svatyni svou, jako zemi, kterouž utvrdil na věky.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 A vyvolil Davida služebníka svého, vzav jej od chlévů stáda.
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 Když chodil za ovcemi březími, zavedl jej, aby pásl Jákoba, lid jeho, a Izraele, dědictví jeho.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 Kterýž pásl je v upřímnosti srdce svého, a zvláštní opatrností rukou svých vodil je.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.