< Žalmy 135 >

1 Halelujah. Chvalte jméno Hospodinovo, chvalte služebníci Hospodinovi,
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Kteříž stáváte v domě Hospodinově, v síňcích domu Boha našeho.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Chvalte Hospodina, nebo jest dobrý Hospodin; žalmy zpívejte jménu jeho, nebo rozkošné jest.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Jákoba zajisté sobě vyvolil Hospodin, a Izraele za svůj lid zvláštní.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Jáť jsem jistě seznal, že veliký jest Hospodin, a Pán náš nade všecky bohy.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Cožkoli chce Hospodin, to činí na nebi i na zemi, v moři i ve všech propastech.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Kterýž způsobuje to, že páry vystupují od krajů země; blýskání s deštěm přivodí, a vyvodí vítr z pokladů svých.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 Kterýž zbil prvorozené v Egyptě, od člověka až do hovada.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Poslal znamení a zázraky u prostřed tebe, Egypte, na Faraona i na všecky služebníky jeho.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Kterýž pobil národy mnohé, a zbil krále mocné,
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Seona krále Amorejského, a Oga krále Bázan, i všecka království Kananejská.
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 A dal zemi jejich v dědictví, v dědictví Izraelovi lidu svému.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Hospodine, jméno tvé na věky, Hospodine, památka tvá od národu až do pronárodu.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Souditi zajisté bude Hospodin lid svůj, a služebníkům svým bude milostiv.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Ale modly pohanské stříbro a zlato, dílo rukou lidských,
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Ústa mají a nemluví, oči mají a nevidí.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Uši mají a neslyší, nýbrž ani ducha není v ústech jejich.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Buďtež jim podobní, kteříž je dělají, a kdožkoli naději svou v nich skládají.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Dome Izraelský, dobrořečte Hospodinu; dome Aronův, dobrořečte Hospodinu.
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Dome Léví, dobrořečte Hospodinu; kteříž se bojíte Hospodina, dobrořečte Hospodinu.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Požehnaný Hospodin z Siona, kterýž přebývá v Jeruzalémě. Halelujah.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Žalmy 135 >