< Žalmy 113 >
1 Halelujah. Chvalte služebníci Hospodinovi, chvalte jméno Hospodinovo.
Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
2 Budiž jméno Hospodinovo požehnáno od tohoto času až na věky.
Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
3 Od východu slunce až do západu jeho chváleno buď jméno Hospodinovo.
Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
4 Vyvýšenť jest nade všecky národy Hospodin, a nad nebesa sláva jeho.
Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
5 Kdo jest rovný Hospodinu Bohu našemu, kterýž vysoko bydlí?
Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
6 Kterýž snižuje se, aby všecko spatřoval, což jest na nebi i na zemi.
atazamaye chini angani na duniani?
7 Vyzdvihuje z prachu nuzného, a z hnoje vyvyšuje chudého,
Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
8 Aby jej posadil s knížaty, s knížaty lidu svého.
ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Kterýž vzdělává neplodnou v čeled, a matku veselící se z dítek. Halelujah.
Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!