< Žalmy 107 >
1 Oslavujte Hospodina, nebo jest dobrý, nebo na věky milosrdenství jeho.
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Nechť o tom vypravují ti, kteříž jsou vykoupeni skrze Hospodina, jak je on vykoupil z ruky těch, kteříž je ssužovali,
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 A shromáždil je z zemí, od východu a od západu, od půlnoci i od moře.
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Bloudili po poušti, po cestách pustých, města k přebývání nenacházejíce.
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 Hladovití a žízniví byli, až v nich svadla duše jejich.
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 Když volali k Hospodinu v ssoužení svém, z úzkostí jejich vytrhl je,
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 A vedl je po cestě přímé, aby přišli do města k bydlení.
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 Nechať oslavují před Hospodinem milosrdenství jeho, a divné skutky jeho před syny lidskými,
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 Poněvadž napájí duši žíznivou, a duši hladovitou naplňuje dobrými věcmi.
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 Kteříž sedí ve tmě a v stínu smrti, sevříni jsouce bídou i železy,
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 Protože odporni byli řečem Boha silného, a radou Nejvyššího pohrdli.
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 Pročež ponížil bídou srdce jejich, padli, a nebylo pomocníka.
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 Když volají k Hospodinu v ssoužení svém, z úzkostí je vysvobozuje.
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 Vyvodí je z temností a stínu smrti, a svazky jejich trhá.
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 Nechať oslavují před Hospodinem milosrdenství jeho, a divné skutky jeho před syny lidskými,
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 Poněvadž láme brány měděné, a závory železné posekává.
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Blázni pro cestu převrácenosti své, a pro nepravosti své v trápení bývají.
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 Oškliví se jim všeliký pokrm, až se i k branám smrti přibližují.
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 Když volají k Hospodinu v ssoužení svém, z úzkostí jejich je vysvobozuje.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 Posílá slovo své, a uzdravuje je, a vysvobozuje je z hrobu.
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 Nechať oslavují před Hospodinem milosrdenství jeho, a divné skutky jeho před syny lidskými,
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 A obětujíce oběti chvály, ať vypravují skutky jeho s prozpěvováním.
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 Kteří se plaví po moři na lodech, pracujíce na velikých vodách,
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 Tiť vídají skutky Hospodinovy, a divy jeho v hlubokosti.
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 Jakž jen dí, hned se strhne vítr bouřlivý, a dme vlny mořské.
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 Vznášejí se k nebi, sstupují do propasti, duše jejich v nebezpečenství rozplývá se.
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 Motají se a nakloňují jako opilý, a všecko umění jejich mizí.
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 Když volají k Hospodinu v ssoužení svém, z úzkostí jejich je vysvobozuje.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 Proměňuje bouři v utišení, tak že umlkne vlnobití jejich.
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 I veselí se, že utichlo; a tak přivodí je k břehu žádostivému.
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 Nechať oslavují před Hospodinem milosrdenství jeho, a divné skutky jeho před syny lidskými.
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 Nechť ho vyvyšují v shromáždění lidu, a v radě starců chválí jej.
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 Obrací řeky v poušť, a prameny vod v suchost,
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 Zemi úrodnou v slatinnou, pro zlost obyvatelů jejích.
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 Pustiny obrací v jezera, a zemi vyprahlou v prameny vod.
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 I osazuje na ní hladovité, aby stavěli města k bydlení.
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 Kteříž osívají pole, a dělají vinice, a shromažďují sobě užitek úrody.
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 Takť on jim žehná, že se rozmnožují velmi, a dobytka jejich neumenšuje.
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 A někdy pak umenšeni a sníženi bývají ukrutenstvím, bídou a truchlostí,
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 Když vylévá pohrdání na knížata, dopouštěje, aby bloudili po poušti bezcestné.
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 Onť vyzdvihuje nuzného z trápení, a rozmnožuje rodinu jako stádo.
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 Nechť to spatřují upřímí, a rozveselí se, ale všeliká nepravost ať zacpá ústa svá.
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 Ale kdo jest tak moudrý, aby toho šetřil, a vyrozumíval mnohému milosrdenství Hospodinovu?
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.