< Žalmy 106 >

1 Halelujah. Oslavujte Hospodina, nebo dobrý jest, nebo na věky milosrdenství jeho.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Kdo může vymluviti nesmírnou moc Hospodinovu, a vypraviti všecku chválu jeho?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Blahoslavení, kteříž ostříhají soudu, a činí spravedlnost každého času.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Pamatuj na mne, Hospodine, pro milost k lidu svému, navštěv mne spasením svým,
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 Abych užíval dobrých věcí s vyvolenými tvými, a veselil se veselím národu tvého, a chlubil se spolu s dědictvím tvým.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Zhřešili jsme i s otci svými, neprávě jsme činili, a bezbožnost páchali.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Otcové naši v Egyptě nerozuměli předivným skutkům tvým, aniž pamatovali na množství milosrdenství tvých, ale odporni byli při moři, při moři Rudém.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 A však vysvobodil je pro jméno své, aby v známost uvedl moc svou.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Nebo přimluvil moři Rudému, a vyschlo; i provedl je skrze hlubiny, jako po poušti.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 A tak zachoval je od ruky toho, jenž jich nenáviděl, a vyprostil je z ruky nepřítele.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 V tom přikryly vody ty, kteříž je ssužovali, nezůstalo ani jednoho z nich.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 A ačkoli věřili slovům jeho, a zpívali chválu jeho,
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Však rychle zapomenuli na skutky jeho, a nečekali na radu jeho;
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Ale jati jsouce žádostí na poušti, pokoušeli Boha silného na pustinách.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 I dal jim, čehož se jim chtělo, a však dopustil hubenost na život jejich.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Potom, když horlili proti Mojžíšovi v vojště, a Aronovi, svatému Hospodinovu,
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 Otevřevši se země, požřela Dátana, a přikryla zběř Abironovu.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 A roznícen byl oheň na rotu jejich, plamen spálil bezbožníky.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Udělali i tele na Orébě, a skláněli se slitině.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 A změnivše slávu svou v podobiznu vola, jenž jí trávu,
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Zapomněli na Boha silného, spasitele svého, kterýž činil veliké věci v Egyptě.
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 A předivné v zemi Chamově, přehrozné při moři Rudém.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Pročež řekl, že je vypléní, kdyby se byl Mojžíš, vyvolený jeho, nepostavil v té mezeře před ním, a neodvrátil prchlivosti jeho, aby nehubil.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Za tím zošklivili sobě zemi žádanou, nevěříce slovu jeho.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 A repcíce v staních svých, neposlouchali hlasu Hospodinova.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 A protož pozdvihl ruky své proti nim, aby je rozmetal po poušti,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 A aby rozptýlil símě jejich mezi pohany, a rozehnal je do zemí.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Spřáhli se také byli s modlou Belfegor, a jedli oběti mrch.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 A tak dráždili Boha skutky svými, až se na ně obořila rána,
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Až se postavil Fínes, a pomstu vykonal, i přetržena jest rána ta.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Což jest mu počteno za spravedlnost od národu do pronárodu, a až na věky.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Opět ho byli popudili při vodách sváru, až se i Mojžíšovi zle stalo pro ně.
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 Nebo k hořkosti přivedli ducha jeho, a pronesl ji rty svými.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 K tomu nevyplénili ani národů těch, o kterýchž jim byl Hospodin poručil,
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 Ale směšujíce se s těmi národy, naučili se skutkům jejich,
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 A sloužili modlám jejich, kteréž jim byly osídlem.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Obětovali zajisté syny své a dcery své ďáblům.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 A vylili krev nevinnou, krev synů svých a dcer svých, kteréž obětovali trapidlům Kananejským, tak že poškvrněna jest země těmi vraždami.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 I zmazali se skutky svými, a smilnili činy svými.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Protož rozpáliv se v prchlivosti Hospodin na lid svůj, v ošklivost vzal dědictví své.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 A vydal je v ruce pohanů. I panovali nad nimi ti, jenž je v nenávisti měli,
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 A utiskali je nepřátelé jejich, tak že sníženi jsou pod ruku jejich.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Mnohokrát je vysvobozoval, oni však popouzeli ho radou svou, pročež potlačeni jsou pro nepravost svou.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 A však patřil na úzkost jejich, a slyšel křik jejich.
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 Nebo se rozpomenul na smlouvu svou s nimi, a želel toho podlé množství milosrdenství svých,
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Tak že naklonil k nim lítostí všecky, kteříž je u vězení drželi.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Zachovej nás, Hospodine Bože náš, a shromažď nás z těch pohanů, abychom slavili jméno tvé svaté, a chlubili se v chvále tvé.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Požehnaný Hospodin Bůh Izraelský od věků až na věky. Na to rciž všecken lid: Amen, Halelujah.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Žalmy 106 >