< Príslovia 10 >

1 Syn moudrý obveseluje otce, ale syn bláznivý zámutkem jest matce své.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Neprospívají pokladové bezbožně nabytí, ale spravedlnost vytrhuje od smrti.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 Nedopustí lačněti Hospodin duši spravedlivého, statek pak bezbožných rozptýlí.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 K nouzi přivodí ruka lstivá, ruka pak pracovitých zbohacuje.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 Kdo shromažďuje v létě, jest syn rozumný; kdož vyspává ve žni, jest syn, kterýž hanbu činí.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 Požehnání jest nad hlavou spravedlivého, ale ústa bezbožných přikrývají ukrutnost.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 Památka spravedlivého požehnaná, ale jméno bezbožných smrdí.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 Moudré srdce přijímá přikázaní, ale blázen od rtů svých padne.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 Kdo chodí upřímě, chodí doufanlivě; kdož pak převrací cesty své, vyjeven bude.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 Kdo mhourá okem, uvodí nesnáz; a kdož jest bláznivých rtů, padne.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 Pramen života jsou ústa spravedlivého, ale ústa bezbožných přikrývají ukrutnost.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 Nenávist vzbuzuje sváry, ale láska přikrývá všecka přestoupení.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 Ve rtech rozumného nalézá se moudrost, ale kyj na hřbetě blázna.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Moudří skrývají umění, úst pak blázna blízké jest setření.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 Zboží bohatého jest město pevné jeho, ale nouze jest chudých setření.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 Práce spravedlivého jest k životu, nábytek pak bezbožných jest k hříchu.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 Stezkou života jde, kdož přijímá trestání; ale kdož pohrdá domlouváním, bloudí.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 Kdož přikrývá nenávist rty lživými, i kdož uvodí v lehkost, ten blázen jest.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 Mnohé mluvení nebývá bez hříchu, kdož pak zdržuje rty své, opatrný jest.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 Stříbro výborné jest jazyk spravedlivého, ale srdce bezbožných za nic nestojí.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 Rtové spravedlivého pasou mnohé, blázni pak pro bláznovství umírají.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 Požehnání Hospodinovo zbohacuje, a to beze všeho trápení.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 Za žert jest bláznu činiti nešlechetnost, ale muž rozumný moudrosti se drží.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 Èeho se bojí bezbožný, to přichází na něj; ale čehož žádají spravedliví, dává Bůh.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Jakož pomíjí vichřice, tak nestane bezbožníka, spravedlivý pak jest základ stálý.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Jako ocet zubům, a jako dým očima, tak jest lenivý těm, kteříž jej posílají.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 Bázeň Hospodinova přidává dnů, léta pak bezbožných ukrácena bývají.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 Očekávání spravedlivých jest potěšení, naděje pak bezbožných zahyne.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 Silou jest upřímému cesta Hospodinova, a strachem těm, kteříž činí nepravost.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 Spravedlivý na věky se nepohne, bezbožní pak nebudou bydliti v zemi.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 Ústa spravedlivého vynášejí moudrost, ale jazyk převrácený vyťat bude.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 Rtové spravedlivého znají, což jest Bohu libého, ústa pak bezbožných převrácené věci.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

< Príslovia 10 >