< 3 Mojžišova 12 >

1 I mluvil Hospodin k Mojžíšovi, řka:
Bwana akamwambia Mose,
2 Mluv synům Izraelským a rci: Žena počnuc, porodí-li pacholíka, nečistá bude za sedm dní; podlé počtu dnů, v nichž odděluje se pro nemoc svou, nečistá bude.
“Waambie Waisraeli: ‘Mwanamke ambaye atapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada kwa siku saba, kama anavyokuwa najisi wakati wa siku zake za hedhi.
3 Potom dne osmého obřezáno bude tělo neobřízky jeho.
Mvulana atatahiriwa siku ya nane.
4 Ona pak ještě za třidceti a tři dni zůstávati bude v očišťování se od krve. Nižádné věci svaté se nedotkne a k svatyni nepůjde, dokudž se nevyplní dnové očištění jejího.
Kisha ni lazima huyo mwanamke asubiri kwa siku thelathini na tatu, ndipo atakaswe kutoka damu kwake. Hataruhusiwa kugusa kitu chochote kilicho kitakatifu au kuingia mahali patakatifu, mpaka siku za kutakaswa kwake zimetimia.
5 Pakli děvečku porodí, nečistá bude za dvě neděle vedlé nečistoty oddělení svého, a šedesáte šest dní zůstávati bude v očištění od krve.
Kama akimzaa mtoto wa kike, mwanamke huyo atakuwa najisi kwa majuma mawili, kama wakati wake wa hedhi. Kisha atasubiri kwa siku sitini na sita, ndipo atatakaswa kutoka damu kwake.
6 Když pak vyplní se dnové očištění jejího po synu aneb po dceři, přinese beránka ročního na obět zápalnou, a holoubátko aneb hrdličku na obět za hřích, ke dveřím stánku úmluvy, knězi.
“‘Siku zake za utakaso kwa ajili ya mwana au binti zitakapotimia, mwanamke huyo atamletea kuhani kwenye ingilio la Hema la Kukutania mwana-kondoo mwenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, na kinda la njiwa au hua kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
7 Kterýž obětovati ji bude před Hospodinem, a očistí ji, a tak očištěna bude od toku krve své. Ten jest zákon té, kteráž porodila pacholíka aneb děvečku.
Atavitoa mbele za Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yake, na kisha atakuwa safi kwa desturi ya ibada kutokana na kutokwa damu kwake. “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya mwanamke atakayezaa mtoto wa kiume au wa kike.
8 Pakli nebude moci býti s beránka, tedy vezme dvé hrdličátek, aneb dvé holoubátek, jedno v obět zápalnou a druhé v obět za hřích. I očistí ji kněz, a tak čistá bude.
Kama huyo mwanamke hana uwezo wa kumpata mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa, moja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kwa njia hii, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”

< 3 Mojžišova 12 >