< Sudcov 19 >
1 Stalo se také toho času, když krále nebylo v Izraeli, že muž nějaký Levíta, jsa pohostinu při straně hory Efraimské, pojal sobě ženu ženinu z Betléma Judova.
Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme. Basi Mlawi mmoja aliyeishi sehemu za mbali katika nchi ya vilima ya Efraimu, akamchukua suria mmoja kutoka Bethlehemu ya Yuda.
2 Kterážto ženina smilnila u něho. I odešla od něho do domu otce svého do Betléma Judova, a byla tam plné čtyři měsíce.
Lakini suria wake akafanya ukahaba dhidi yake, naye akamwacha akarudi nyumbani kwa baba yake huko Bethlehemu ya Yuda. Baada ya kukaa huko kwa muda wa miezi minne,
3 Vstav pak muž její, šel za ní, aby namluvě ji, zase ji přivedl, maje s sebou mládence svého a dva osly. Tedy ona uvedla jej do domu otce svého. Kteréhož když uzřel otec té děvky, zradoval se z příchodu jeho.
mume wake akaenda kumsihi ili arudi. Alikwenda na mtumishi wake na punda wawili. Yule mwanamke akamkaribisha nyumbani mwa baba yake, baba yake alipomwona akamkaribisha kwa furaha.
4 I zdržel jej tchán jeho, otec té děvky, tak že pozůstal u něho za tři dni. Tu také jídali i píjeli i nocovali.
Baba mkwe wake, yaani, baba yake yule msichana, akamzuia ili akae, hivyo akakaa na huyo baba mkwe wake kwa siku tatu, wakila, wakinywa na kulala huko.
5 Dne pak čtvrtého, když tím raněji vstali, vstal i on, aby odšel. Tedy řekl otec té děvky k zeti svému: Posilni se kouskem chleba, a potom půjdete.
Siku ya nne wakaamka mapema naye akajiandaa kuondoka, lakini baba wa yule msichana akamwambia mkwewe, “Ujiburudishe kwa kula kitu chochote, ndipo uweze kwenda.”
6 Sedli tedy a pojedli oba spolu, a napili se. Potom řekl otec děvky k muži: Posediž medle, nýbrž pobuď přes noc, a buď mysli veselé.
Basi wakaketi wote wawili ili kula na kunywa pamoja. Baadaye baba wa msichana akamwambia, “Tafadhali ubakie usiku huu upate kujifurahisha nafsi yako.”
7 Když pak vstal ten muž, chtěje předce jíti, mocí jej zdržel test jeho. A tak se vrátil a zůstal tu přes noc.
Basi yule mtu alipotaka kuondoka baba wa yule msichana akamsihi, basi akabaki usiku ule.
8 Potom dne pátého vstal tím raněji, aby se bral. I řekl otec té děvky: Posilň se, prosím. I prodlili, až se den nachýlil, nebo jedli oba.
Asubuhi ya siku ya tano, alipoamka ili aondoke, baba wa yule msichana akamwambia, “Jiburudishe nafsi yako. Ngoja mpaka mchana!” Kwa hiyo wote wawili wakala chakula pamoja.
9 Tedy vstal muž ten, aby šel, on i ženina jeho i mládenec jeho. I řekl mu tchán jeho, otec děvky: Aj, již se den nachýlil k večerou, medle zůstaňte přes noc; aj, dokonává se den, pobuď přes noc zde, a buď mysli veselé, a zítra tím raněji vypravíte se na cestu svou, a půjdeš k příbytku svému.
Basi wakati yule mtu alipoinuka aende zake, pamoja na suria wake na mtumishi wake, baba mkwe wake, yaani, baba wa yule msichana akamwambia, “Tazama sasa jioni inakaribia. Ulale hapa usiku unakaribia. Ukae, ukajifurahishe nafsi yako. Kesho unaweza kuamka mapema asubuhi na uende nyumbani kwako.”
10 On pak nechtěl zůstati přes noc, ale vstav, odšel, a přišel proti Jebus, jenž jest Jeruzalém, a s ním dva oslové s břemeny i ženina jeho.
Lakini akakataa kulala tena, akaondoka na kwenda mpaka Yebusi (ndio Yerusalemu), akiwa na punda wake wawili waliotandikiwa, pamoja na suria wake.
11 Když pak byli blízko Jebus, a den se velmi nachýlil, řekl mládenec pánu svému: Poď, prosím, obraťme se do města toho Jebuzejského, abychom v něm přenocovali.
Alipokaribia Yebusi na usiku ukiwa umekaribia, mtumishi akamwambia bwana wake, “Haya sasa natuingie katika mji huu wa Wayebusi tulale humo.”
12 Jemuž odpověděl pán jeho: Neobrátíme se do města cizozemců, kteréž není synů Izraelských, ale půjdeme až do Gabaa.
Lakini bwana wake akamjibu, “Hapana. Hatutaingia kwenye mji wa kigeni, ambao watu wake si Waisraeli. Tutaendelea mpaka tufike Gibea.”
13 Řekl ještě mládenci svému: Poď, abychom přišli k některému z těch míst, a zůstali přes noc v Gabaa aneb v Ráma.
Akasema, “Haya, tujitahidi tufike Gibea au Rama, nasi tutalala katika mji mmojawapo.”
14 Pomíjejíce tedy, odešli, a zapadlo jim slunce blízko Gabaa, kteréž jest Beniaminských.
Hivyo wakaendelea na safari, jua likachwea walipokaribia Gibea ambao ni mji wa Benyamini.
15 I obrátili se tam, aby vejdouce, zůstali přes noc v Gabaa. A když tam všel, posadil se na ulici města, proto že nebyl, kdo by je přijal do domu a dal jim nocleh.
Wakageuka ili kuingia na kulala Gibea. Wakaingia humo, wakaketi kwenye uwanja wa mji, wala hakuna mtu yeyote aliyewakaribisha kwake ili wapate kulala.
16 A aj, muž starý vracoval se od práce své s pole u večer, kterýž také byl s hory Efraimovy, a bydlil pohostinu v Gabaa; ale lidé místa toho byli synové Jemini.
Jioni ile mtu mmoja mzee toka nchi ya vilima ya Efraimu, aliyekuwa anaishi huko Gibea (watu wa sehemu ile walikuwa Wabenyamini), akarudi kutoka kwenye kazi za shamba.
17 A když pozdvihl očí svých, uzřel muže toho pocestného na ulici města. I řekl jemu ten stařec: Kam se béřeš, a odkud jdeš?
Alipotazama na kuwaona hao wasafiri katika uwanja wa mji, yule mzee akawauliza, “Ninyi mnakwenda wapi? Nanyi mmetoka wapi?”
18 Jemuž odpověděl: Jdeme z Betléma Judova až k stranám hory Efraimovy, odkudž jsem; nebo jsem byl odšel do Betléma Judova. Jduť pak do domu Hospodinova, a není žádného, kdo by mne přijal do domu;
Akamwambia, “Tumepita kutoka Bethlehemu ya Yuda, tunaelekea katika nchi ya vilima ya Efraimu, ambako ndiko ninakoishi. Nilikwenda Bethlehemu ya Yuda na sasa ninakwenda katika nyumba ya Bwana. Hakuna mtu yeyote aliyenikaribisha katika nyumba yake.
19 Ješto mám i slámu a obrok pro osly své, tolikéž i chléb, ano i víno pro sebe a děvku tvou, a mládence, kterýž jest s služebníkem tvým, tak že v ničemž nemáme nedostatku.
Tunazo nyasi na chakula cha punda wetu na mkate na divai kwa ajili yetu sisi watumishi wako, yaani mimi, mtumishi wako mwanamke, pamoja na huyu kijana tuliyefuatana naye. Hatuhitaji kitu chochote.”
20 I řekl muž ten starý: Měj ty pokoj. Èehoť se koli nedostává, nechť já to opatřím, ty toliko na ulici nezůstávej přes noc.
Yule mzee akawaambia, “Amani iwe kwenu! Karibuni nyumbani mwangu. Nitawapa mahitaji yenu yote, msilale katika uwanja huu wa mji.”
21 Tedy uvedl jej do domu svého, a obrok dal oslům; potom umyvše nohy své, jedli a pili.
Hivyo akamwingiza nyumbani mwake na kuwalisha punda wake. Baada ya kunawa miguu yao, wakala na kunywa.
22 A když očerstvili srdce své, aj, muži města toho, muži nešlechetní, obklíčivše dům, tloukli na dvéře a mluvili tomu muži starci, hospodáři domu, řkouce: Vyveď muže toho, kterýž všel do domu tvého, abychom ho poznali.
Walipokuwa wakijiburudisha, watu waovu wa mji huo, wakaizingira ile nyumba. Wakagonga mlango na kusema na yule mzee mwenye nyumba, “Mtoe nje yule mtu aliyeingia kwako, tupate kumlawiti.”
23 K nimžto vyšed muž ten, hospodář domu, řekl jim: Nikoli, bratří moji, nečiňte, prosím, zlého, poněvadž všel ten muž do domu mého, neprovoďte nešlechetnosti té.
Yule mwenye nyumba akatoka nje na kuwaambia, “Hapana, ndugu zangu msiwe waovu namna hii, ninawasihi. Kwa kuwa huyu mtu ni mgeni wangu msifanye jambo hili la aibu.
24 Aj, dceru svou, kteráž pannou jest, a ženinu jeho, ty hned vyvedu, i ponížíte jich, aneb učiníte jim, což se vám za dobré vidí; jen muži tomu nečiňte věci té hanebné.
Tazameni, hapa yupo binti yangu ambaye ni bikira na suria wa huyu mtu. Nitawatoleeni hawa sasa, mkawatwae kwa nguvu na kuwafanyia lolote mtakalo. Lakini kwa mtu huyu msimfanyie jambo ovu hivyo.”
25 Ale nechtěli ho uposlechnouti muži ti. Pojav tedy muž ten ženinu svou, vyvedl ji k nim ven, i poznali ji, a zle jí požívali přes celou noc až do jitra; potom pustili ji, když počínalo zasvitávati.
Lakini wale watu hawakumsikia. Hivyo yule mtu akamtoa yule suria wake nje kwa wale watu, nao wakambaka na kumnajisi usiku ule kucha mpaka asubuhi. Kulipoanza kupambazuka wakamwachia aende.
26 V svitání pak přišla žena ta, a padši, ležela u dveří domu toho muže, kdež byl pán její, až se rozednilo.
Alfajiri yule mwanamke akarudi kwenye ile nyumba bwana wake alikokuwa, akaanguka chini mlangoni, akalala pale hata kulipopambazuka.
27 Když pak vstal pán její ráno, otevřev dvéře domu, vycházel, aby se bral dále cestou svou. A aj, žena ta, ženina jeho, ležela u dveří domu, a ruce její byly na prahu.
Bwana wake alipoamka asubuhi na kufungua mlango wa nyumba na kutoka nje ili kuendelea na safari yake, tazama, yule suria wake alikuwa ameanguka pale penye ingilio la nyumba na mikono yake ikiwa penye kizingiti cha chini.
28 Jížto řekl: Vstaň, a poďme. A nic neodpověděla. Vzav tedy ji na osla, a vstav muž ten, odšel k místu svému.
Akamwambia yule suria, “Inuka, twende.” Lakini hakujibu. Yule bwana akamwinua akampandisha juu ya punda wake, wakaondoka kwenda nyumbani.
29 Když pak přišel do domu svého, vzal meč, a pochytiv ženinu svou, rozsekal ji s kostmi jejími na dvanácte kusů, a rozeslal ji po všech končinách Izraelských.
Alipofika nyumbani, akachukua kisu na kumkatakata yule suria kiungo kwa kiungo, sehemu kumi na mbili, na kuvipeleka hivyo vipande katika sehemu zote za Israeli.
30 A bylo, že kdožkoli uzřel, pravil: Nikdy se nestalo ani vidíno bylo co podobného od toho času, jakž vyšli synové Izraelští z země Egyptské, až do tohoto dne. Posuďte toho pilně, poraďte se a promluvte o to.
Kila mtu aliyeona akasema, “Jambo la namna hii halijaonekana wala kutendeka, tangu Israeli walipopanda kutoka Misri. Fikirini juu ya jambo hili! Tafakarini juu ya jambo hili! Tuambieni tufanye nini!”