< Józua 21 >

1 Přistoupili pak přední z otců Levítského pokolení k Eleazarovi knězi, a k Jozue, synu Nun, a k předním z otců pokolení synů Izraelských,
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2 A mluvili k nim v Sílo, v zemi Kananejské, řkouce: Hospodin přikázal skrze Mojžíše, abyste nám dali města k přebývání, i podměstí jejich pro dobytky naše.
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 Dali tedy synové Izraelští Levítům z dědictví svého, vedlé rozkázaní Hospodinova, města tato i podměstí jejich.
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 Padl pak los čeledem Kahat, i dáno losem synům Arona kněze, Levítům, z pokolení Juda, a z pokolení Simeon, i z pokolení Beniaminova měst třinácte.
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 A jiným synům Kahat, z čeledí pokolení Efraimova, a z pokolení Danova, a z polovice pokolení Manassesova losem dáno měst deset.
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 Synům pak Gerson, z čeledí pokolení Izacharova, a z pokolení Asserova, též z pokolení Neftalímova, a z polovice pokolení Manassesova v Bázan losem dáno měst třinácte.
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 Synům Merari po čeledech jejich, z pokolení Rubenova a z pokolení Gádova, též z pokolení Zabulonova měst dvanácte.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 Dali tedy synové Izraelští Levítům ta města i předměstí jejich, (jakož přikázal Hospodin skrze Mojžíše, ) losem.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 A tak z pokolení synů Judových, a z pokolení synů Simeonových dána jsou města, kterýchž tuto jména jsou položena.
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 A dostal se první díl synům Aronovým, z čeledí Kahat, z synů Léví; nebo jim padl los první.
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 Dáno jest tedy jim město Arbe, otce Enakova, (jenž jest Hebron, ) na hoře Juda, a předměstí jeho vůkol něho.
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 Ale pole města toho i vsi jeho dali Kálefovi synu Jefone k vládařství jeho.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 Synům tedy Arona kněze dali město útočišťné vražedlníku, Hebron i předměstí jeho, a Lebno i předměstí jeho;
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 A Jeter s předměstím jeho, též Estemo a předměstí jeho;
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 Holon i předměstí jeho, a Dabir s podměstím jeho;
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 Také Ain s předměstím jeho, a Juta s podměstím jeho, i Betsemes a předměstí jeho, měst devět z toho dvojího pokolení.
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 Z pokolení pak Beniaminova dali Gabaon a předměstí jeho, a Gaba s předměstím jeho;
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
18 Též Anatot a podměstí jeho, i Almon s předměstím jeho, města čtyři.
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 Všech měst synů Aronových kněží třinácte měst s předměstími jejich.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 Èeledem pak synů Kahat, Levítům, kteříž pozůstali z synů Kahat, (byla pak města losu jejich z pokolení Efraim, )
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 Dali jim město útočišťné vražedlníku, Sichem i předměstí jeho, na hoře Efraim, a Gázer s předměstím jeho.
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 Též Kibsaim a předměstí jeho, a Betoron s předměstím jeho, města čtyři.
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 Z pokolení pak Dan: Elteke a předměstí jeho, a Gebbeton s předměstím jeho;
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 Též Aialon a předměstí jeho, a Getremmon s podměstím jeho, města čtyři.
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 Z polovice pak pokolení Manassesova: Tanach a podměstí jeho, a Getremmon s předměstím jeho, města dvě.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 Všech měst deset s předměstími jejich čeledem synům Kahat ostatním.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 Synům také Gersonovým, z čeledí Levítských, z polovice pokolení Manassesova dali město útočišťné vražedlníku, Golan v Bázan a předměstí jeho, a Bozran s předměstím jeho, města dvě.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 Z pokolení Izacharova: Kesion a podměstí jeho, a Daberet s předměstím jeho;
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 Jarmut a předměstí jeho, a Engannim s předměstím jeho, města čtyři.
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 Z pokolení pak Asserova: Mesal a předměstí jeho, též Abdon a podměstí jeho;
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 Helkat s předměstím jeho, a Rohob s podměstím jeho, města čtyři.
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 Z pokolení také Neftalímova: Město útočišťné vražedlníku, Kedes v Galilei a předměstí jeho, a Hamotdor s předměstím jeho, a Kartam s předměstím jeho, města tři.
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 Všech měst Gersonitských po čeledech jejich, třinácte měst s předměstími jejich.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 Èeledem pak synů Merari, Levítům ostatním, dali z pokolení Zabulonova Jekonam a předměstí jeho, Karta a předměstí jeho;
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 Damna a předměstí jeho, Naalol a předměstí jeho, města čtyři.
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
36 Z pokolení pak Rubenova: Bozor a předměstí jeho, a Jasa a předměstí jeho;
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
37 Kedemot a předměstí jeho, a Mefat s podměstím jeho, města čtyři.
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
38 A z pokolení Gádova: Město útočišťné vražedlníku, Rámot v Galád a předměstí jeho, a Mahanaim s předměstím jeho;
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
39 Ezebon a podměstí jeho, Jazer s podměstím jeho, města čtyři.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 Všech měst synů Merari po čeledech jejich, kteříž ostatní byli z čeledí Levítských, bylo podlé losu jejich měst dvanácte.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 A tak všech měst Levítských u prostřed vládařství synů Izraelských měst čtyřidceti osm s předměstími svými.
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 Mělo pak to město jedno každé obzvláštně svá předměstí vůkol sebe, a taková byla všecka ta města.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 Dal tedy Hospodin Izraelovi všecku tu zemi, kterouž s přísahou zaslíbil dáti otcům jejich; i opanovali ji dědičně, a bydlili v ní.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 Dal také Hospodin jim odpočinutí se všech stran podlé všeho, jakž byl s přísahou zaslíbil otcům jejich, aniž kdo byl, ješto by ostál proti nim ze všech nepřátel jejich; všecky nepřátely jejich dal Hospodin v ruku jejich.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 Nepominulo ani jedno slovo ze všelikého slova dobrého, kteréž mluvil Hospodin k domu Izraelskému, ale všecko se tak stalo.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.

< Józua 21 >