< Józua 14 >

1 Toto pak jest, což dědičně obdrželi synové Izraelští v zemi Kanán, což uvedli jim právem dědičným k vládařství Eleazar kněz, a Jozue, syn Nun, a přední z otců, v pokolení synů Izraelských,
Maeneo haya ya nchi ambayo watu wa Israeli waliyapokea kama urithi wao katika nchi ya Kanaani. Urith huu uligawanywa kwao na Eliazeri kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya mababu wa familia zao kati ya watu wa Israeli.
2 Losem dělíce dědictví jejich, jakož přikázal Hospodin skrze Mojžíše, aby dal devateru pokolení a polovici pokolení.
Urithi wao ulichaguliwa kwa kupiga kura kwa makabila tisa na nusu, kama vile Yahweh alivyoagiza kwa mkono wa Musa.
3 Nebo byl dal Mojžíš dědictví půltřetímu pokolení před Jordánem, Levítům pak nedal dědictví u prostřed nich.
Kwa kuwa Musa alikuwa amewapa urithi makabila mawili na nusu ng'ambo ya Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi wowote.
4 Nebo synů Jozefových bylo dvoje pokolení, Manassesovo a Efraimovo; a nedali dílu Levítům v zemi, kromě měst k bydlení, a podměstí jejich pro dobytek a stáda jejich.
Kabila la Yusufu kwa uhalisia yalikuwa makabila mawili, Manase na Efraimu. Na hakuna sehemu yoyote ya urithi waliyopewa Walawi katika nchi, lakini walipewa miji ya kuishi ndani yake pamoja na sehemu ya malisho ya mifugo yao na kwa ajili ya riziki zao.
5 Jakož přikázal Hospodin Mojžíšovi, tak učinili synové Izraelští, a rozdělili zemi.
Watu wa Israeli walifanya hivyo kama vile Yahweh alivyomwagiza Musa, basi waliiganywa nchi.
6 Přistoupili pak synové Juda k Jozue v Galgala, i promluvil k němu Kálef, syn Jefonův, Cenezejský: Ty víš, co jest mluvil Hospodin k Mojžíšovi, muži Božímu, z příčiny mé a tvé v Kádesbarne.
Kisha kabila la Yuda lilikuja kwa Yoshua huko Giligali. Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi, akamwambia,”Unajua kile Yahweh alichomwambia Musa mtu wa Mungu juu yako na mimi huko Barnea.
7 Ve čtyřidceti letech byl jsem, když mne poslal Mojžíš, služebník Hospodinův, z Kádesbarne k spatření země, a oznámil jsem jemu tu věc, jakž bylo v srdci mém.
Nilikuwa na umri wa miaka arobani wakati Musa mtumishi wa Yahweh aliponituma kutoka Kadeshi Barnea kuipeleleza nchi. Nilimletea taarifa tena kama nilivyotakiwa kufanya katika moyo wangu.
8 Ale bratří moji, kteříž šli se mnou, zkormoutili srdce lidu, já pak cele kráčel jsem za Hospodinem Bohem svým.
Lakini ndugu zangu walioenda pamoja nami waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa woga. Lakini mimi nilimfuata Yahweh kabisa.
9 I přisáhl Mojžíš toho dne, řka: Jistě že země, po kteréž jsi chodil nohama svýma, bude v dědictví tobě i synům tvým až na věky, proto že jsi cele následoval Hospodina Boha mého.
Musa aliapa katika siku hiyo akisema, “Hakika nchi ambayo miguu yako imetembea juu yake itakuwa urithi wako na kwa watoto wako milele, kwasababu umemfuata kabisa Yahweh Mungu wangu.
10 A nyní, aj, propůjčil mi Hospodin života, jakož zaslíbil. Již čtyřidceti a pět let jest od toho času, jakž toto mluvil Hospodin k Mojžíšovi, a jakž chodil Izrael po poušti, a aj, již dnes jsem v osmdesáti pěti letech,
Tazama! sasa, Yahweh amenihifadhi hai kwa miaka hii arobaini na tano, kama alivyosema - tangu kipindi kile Yahweh alivyomwambia Musa neno hili, wakati huo Waisraeli walikuwa wakitembea jangwani. Tazama! sasa katika siku hii ya leo nina miaka themanini na mitano.
11 A ještě nyní jsem při síle jako tehdáž, když poslal mne Mojžíš. Jaká byla síla má tehdáž, taková i nyní síla má jest k boji, a k vycházení i k vcházení.
Bado hata siku hii ya leo nina nguvu kama nilivyokuwa katika siku ile ambayo Musa alinituma. Nguvu zangu za sasa ni sawa na nguvu zangu za kipindi kile, kwa ajili ya vita na kwa kwenda na kwa kuja.
12 Protož nyní dej mi horu tuto, o níž mluvil Hospodin onoho dne, nebo ty slyšel jsi toho dne, že Enakim jsou tam, a města veliká a pevně hrazená. Bude-li Hospodin se mnou, vyhladím je, jakož mluvil Hospodin.
Sasa basi, nipe nchi hii ya milima, ambayo Yahweh aliniahidi katika siku hiyo. Kwa kuwa ulisikia katika siku hiyo kuwa Wanakimu walikuwa huko katika miji yenye ngome. Itakuwa kwamba Yahweh atakuwa pamoja nami na ya kwamba nitawafukuzia mbali, kama vile Yahweh alivyosema.”
13 I požehnal mu Jozue, a dal Hebron Kálefovi, synu Jefone, v dědictví.
Kisha Yoshua alimbariki Kalebu mwana wa Yefune na alimpa Hebroni kama urithi wake.
14 Protož dostal se Hebron Kálefovi, synu Jefona Cenezejského, v dědictví až do tohoto dne, proto že cele kráčel za Hospodinem Bohem Izraelským.
Hivyo Hebroni ikawa urithi wa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi hata leo, kwasababu alimfuata kabisa Yahweh, Mungu wa Israeli.
15 Sloulo pak Hebron prvé město Arbe, kterýžto Arbe byl člověk veliký mezi Enakim. I odpočinula země od bojů.
Basi, jina la Hebroni hapo mwanzo lilikuwa ni Kiriathi Arba ( Arba ambaye alikuwa ni mtu mkuu miongoni mwa Wanakim). Kisha nchi ikawa na raha bila vita.

< Józua 14 >