< Joel 2 >

1 Trubte trubou na Sionu, a křičte na hoře svaté mé, nechť se třesou všickni obyvatelé této země, nebo přichází den Hospodinův, nebo blízký jest,
Pigeni tarumbeta katika Sayuni; pigeni mbiu katika mlima wangu mtakatifu. Wote waishio katika nchi na watetemeke, kwa kuwa siku ya Bwana inakuja. Iko karibu,
2 Den temnosti a mračna, den oblaku a mrákoty, jako záře jitřní rozprostřená po horách: Lid mnohý a silný, jemuž rovného nebylo od věků, aniž po něm kdy bude až do let národů i pronárodů.
siku ya giza na huzuni, siku ya mawingu na utusitusi. Kama mapambazuko yasambaavyo toka upande huu wa milima hata upande mwingine jeshi kubwa na lenye nguvu linakuja. Jambo kama hili halijakuwepo tangu zamani wala halitakuwepo tena kamwe kwa vizazi vijavyo.
3 Před tváří jeho oheň zžírati bude, a za ním plamen plápolati; před ním země tato jako zahrada Eden, ale po něm bude poušť přehrozná, a aniž bude, což by ušlo před ním.
Mbele yao moto unateketeza, nyuma yao miali ya moto inawaka kwa nguvu. Mbele yao nchi iko kama bustani ya Edeni, nyuma yao ni jangwa lisilofaa: hakuna kitu kinachowaepuka.
4 Způsob jeho bude jako způsob koní, a jako jízdní, tak poběhnou.
Wanaonekana kama farasi; wanakwenda mbio kama askari wapanda farasi.
5 Jako s hřmotem vozů po vrších hor skákati budou, jako hluk plamene ohně zžírajícího strniště, jako lid silný zšikovaný k bitvě.
Wanatoa sauti kama magari ya vita, wanaporukaruka juu ya vilele vya milima, kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua, kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.
6 Tváři jeho děsiti se budou lidé, všecky tváře zčernají jako hrnec.
Wanapoonekana, mataifa yanakuwa katika maumivu makuu; kila uso unabadilika rangi.
7 Jako rekové poběhnou, jako muži váleční vstoupí na zed, a jeden každý cestou svou půjde, aniž se uchýlí z stezek svých.
Wanashambulia kama wapiganaji wa vita; wanapanda kuta kama askari. Wote wanatembea katika safu, hawapotoshi safu zao.
8 Jeden druhého nebude tlačiti, každý silnicí svou půjde, a byť i na meč upadli, nebudou raněni.
Hakuna anayemsukuma mwenzake; kila mmoja anakwenda mbele moja kwa moja. Wanapita katika vizuizi bila kuharibu safu zao.
9 Po městě těkati budou, po zdech běhati, na domy vstupovati, a okny polezou jako zloděj.
Wanaenda kasi kuingia mjini; wanakimbia ukutani. Wanaingia ndani ya nyumba; kwa kuingilia madirishani kama wevi.
10 Před tváří jeho třásti se bude země, pohnou se nebesa, slunce i měsíc se zatmí, a hvězdy potratí blesk svůj.
Mbele yao dunia inatikisika, anga linatetemeka, jua na mwezi vinatiwa giza, na nyota hazitoi mwanga wake tena.
11 Hospodin pak sám vydá hlas svůj před vojskem svým, proto že velmi veliký bude tábor jeho, proto že silný ten, kdož vykoná slovo jeho. (Nebo veliký bude den Hospodinův a hrozný náramně), i kdož jej bude moci snésti?
Bwana anatoa mshindo wa ngurumo mbele ya jeshi lake; majeshi yake hayana idadi, ni wenye nguvu nyingi wale ambao hutii agizo lake. Siku ya Bwana ni kuu, ni ya kutisha. Ni nani anayeweza kuistahimili?
12 A protož ještě nyní dí Hospodin: Obraťte se ke mně samému celým srdcem svým, a to s postem a s pláčem i s kvílením.
“Hata sasa,” asema Bwana, “nirudieni kwa mioyo yenu yote, kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza.”
13 A roztrhněte srdce vaše, a ne roucha vaše, a navraťte se k Hospodinu Bohu vašemu; neboť jest on milostivý a lítostivý, dlouhočekající a hojný v milosrdenství, a kterýž lituje zlého.
Rarueni mioyo yenu na siyo mavazi yenu. Mrudieni Bwana, Mungu wenu, kwa maana yeye ndiye mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo, huona huruma, hujizuia kuleta maafa.
14 Kdo ví, neobrátí-li se a nebude-li želeti, a nezůstaví-li po něm požehnání, oběti suché a mokré Hospodinu Bohu vašemu.
Ni nani ajuaye? Yeye aweza kugeuka na kuwa na huruma na kuacha baraka nyuma yake: sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji kwa ajili ya Bwana Mungu wenu.
15 Trubte trubou na Sionu, uložte půst, svolejte shromáždění.
Pigeni tarumbeta katika Sayuni, tangazeni saumu takatifu, liiteni kusanyiko takatifu.
16 Shromažďte lid, posvěťte shromáždění, shromažďte starce, shromažďte maličké i ty, jenž prsí požívají; nechť vyjde ženich z pokojíka svého a nevěsta z schrany své.
Wakusanyeni watu, wekeni wakfu kusanyiko; waleteni pamoja wazee, wakusanyeni watoto, wale wanyonyao maziwa. Bwana arusi na atoke chumbani mwake na bibi arusi naye atoke katika chumba chake.
17 Kněží, služebníci Hospodinovi, ať plačí mezi síňcí a oltářem, a řeknou: Odpusť, ó Hospodine, lidu svému, a nevydávej dědictví svého v pohanění, tak aby nad nimi panovati měli pohané. Proč mají říkati mezi národy: Kde jest Bůh jejich?
Makuhani, ambao wanahudumu mbele za Bwana, na walie katikati ya ukumbi wa Hekalu na madhabahu. Waseme, “Wahurumie watu wako, Ee Bwana. Usifanye urithi wako kitu cha kudharauliwa, neno la dhihaka kati ya mataifa. Kwa nini wasemezane miongoni mwao, ‘Yuko wapi Mungu wao?’”
18 I bude horlivou milostí zažžen Hospodin k zemi své, a slituje se nad lidem svým.
Kisha Bwana atakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake na kuwa na huruma juu ya watu wake.
19 A ohlásí se Hospodin, a řekne lidu svému: Aj, já pošli vám obilé, mest a olej, i budete jím nasyceni, aniž vás vydám více v pohanění mezi pohany.
Bwana atawajibu: “Ninawapelekea nafaka, mvinyo mpya na mafuta, vya kuwatosha ninyi hadi mridhike kabisa; kamwe sitawafanya tena kitu cha kudharauliwa na mataifa.
20 Nebo půlnoční vojsko vzdálím od vás, a zaženu je do země vyprahlé a pusté, přední houf jeho k moři východnímu, konec pak jeho k moři nejdalšímu; i vzejde z něho smrad a puch, jakžkoli sobě mocně počíná.
“Nitafukuza jeshi la kaskazini likae mbali nanyi, nikilisukuma ndani ya jangwa, askari wa safu za mbele wakienda ndani ya bahari ya mashariki na wale wa safu za nyuma katika bahari ya magharibi. Uvundo wake utapaa juu; harufu yake itapanda juu.” Hakika ametenda mambo makubwa.
21 Neboj se země, plésej a vesel se; neboť mocně dělati bude Hospodin dílo své.
Usiogope, ee nchi; furahi na kushangilia. Hakika Bwana ametenda mambo makubwa.
22 Nebojtež se zvířátka polí mých; neboť se zotaví pastviska na poušti, a stromoví přinese ovoce své, fík i vinný kmen vydadí moc svou.
Msiogope, enyi wanyama pori, kwa kuwa mbuga za malisho yenu zinarudia ubichi. Miti nayo inazaa matunda, mtini na mzabibu inatoa utajiri wake.
23 I vy, synové Sionští, plésejte a veselte se v Hospodinu Bohu vašem; nebo vám dá déšť příhodný, a sešle vám déšť hojný, podzimní i jarní, v čas.
Furahini, enyi watu wa Sayuni, shangilieni katika Bwana Mungu wenu, kwa kuwa amewapa mvua za vuli kwa kipimo cha haki. Anawapelekea mvua nyingi, mvua ya vuli na ya masika, kama mwanzoni.
24 I budou naplněny stodoly obilím, a oplývati budou presové mstem a olejem.
Sakafu za kupuria zitajaa nafaka, mapipa yatafurika mvinyo mpya na mafuta.
25 A tak nahradím vám léta, kteráž sežraly kobylky, brouci, chroustové a housenky, vojsko mé veliké, kteréž jsem posílal na vás.
“Nitawalipa kwa ajili ya miaka ile iliyoliwa na nzige: parare, madumadu na tunutu, jeshi langu kubwa ambalo nililituma katikati yenu.
26 Budete zajisté míti co jísti, a nasyceni jsouce, chváliti budete jméno Hospodina Boha svého, kterýž učinil s vámi divné věci, aniž zahanben bude lid můj na věky.
Mtakuwa na wingi wa vyakula mpaka mshibe, na mtalisifu jina la Bwana Mungu wenu, ambaye amefanya maajabu kwa ajili yenu; kamwe watu wangu hawataaibishwa tena.
27 A poznáte, že já jsem u prostřed Izraele, a že já Hospodin jsem Bohem vaším, a že není žádného jiného; neboť nebude zahanben lid můj na věky.
Ndipo mtakapojua kwamba mimi niko katika Israeli kwamba mimi ndimi Bwana Mungu wenu, na kwamba hakuna mwingine; kamwe watu wangu hawataaibika tena.
28 I stane se potom, že vyleji Ducha svého na všeliké tělo, a budou prorokovati synové vaši i dcery vaše; starci vaši sny mívati budou, mládenci vaši vidění vídati budou.
“Hata itakuwa, baada ya hayo, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono.
29 Nýbrž i na služebníky a na služebnice v těch dnech vyleji Ducha svého,
Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu.
30 A ukáži zázraky na nebi i na zemi, krev a oheň a sloupy dymové.
Nami nitaonyesha maajabu katika mbingu na duniani: damu, moto na mawimbi ya moshi.
31 Slunce obrátí se v tmu a měsíc v krev, prvé než přijde den Hospodinův veliký a hrozný,
Jua litageuzwa kuwa giza na mwezi kuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ya Bwana ile kuu na ya kutisha.
32 A však stane se, že kdož by koli vzýval jméno Hospodinovo, vysvobozen bude; nebo na hoře Sion a v Jeruzalémě bude vysvobození, jakož pověděl Hospodin, totiž v ostatcích, kterýchž povolá Hospodin.
Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa. Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu kutakuwepo wokovu, kama Bwana alivyosema, miongoni mwa walionusurika ambao Bwana awaita.

< Joel 2 >