< Jób 34 >

1 Ještě mluvil Elihu, a řekl:
Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
2 Poslouchejte, moudří, řečí mých, a rozumní, ušima pozorujte.
“Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
3 Nebo ucho řečí zkušuje, tak jako dásně okoušejí pokrmu.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
4 Soud sobě zvolme, a vyhledejme mezi sebou, co by bylo dobrého.
Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
5 Nebo řekl Job: Spravedliv jsem, a Bůh silný zavrhl při mou.
Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
6 Své-liž bych pře ukrývati měl? Přeplněna jest bolestí rána má bez provinění.
Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
7 Který muž jest podobný Jobovi, ješto by pil posměch jako vodu?
Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
8 A že by všel v tovaryšství s činiteli nepravosti, a chodil by s lidmi nešlechetnými?
ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
9 Nebo řekl: Neprospívá to člověku líbiti se Bohu.
Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
10 A protož, muži rozumní, poslouchejte mne. Odstup od Boha silného nešlechetnost a od Všemohoucího nepravost.
Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
11 Nebo on podlé skutků člověka odplací, a podlé toho, jaká jest čí cesta, působí, aby to nalézal.
na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
12 A naprosto Bůh silný nečiní nic nešlechetně, a Všemohoucí nepřevrací soudu.
Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
13 Kdo svěřil jemu zemi? A kdo zpořádal všecken okršlek?
Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
14 Kdyby se na něj obrátil, a ducha jeho i duši jeho k sobě vzal,
Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
15 Umřelo by všeliké tělo pojednou, a tak by člověk do prachu se navrátil.
basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
16 Máš-li tedy rozum, poslyš toho, pusť v uši své hlas řečí mých.
Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
17 Ješto ten, kterýž by v nenávisti měl soud, zdaliž by panovati mohl? Èili toho, jenž jest svrchovaně spravedlivý, za nešlechetného vyhlásíš?
Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
18 Zdaliž sluší králi říci: Ó nešlechetný, a šlechticům: Ó bezbožní?
Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
19 Mnohem méně tomu, kterýž nepřijímá osob knížat, aniž u něho má přednost urozený před nuzným; nebo dílo rukou jeho jsou všickni.
Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
20 V okamžení umírají, třebas o půl noci postrčeni bývají lidé, a pomíjejí, a zachvácen bývá silný ne rukou lidskou.
Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
21 Nebo oči jeho hledí na cesty člověka, a všecky kroky jeho on spatřuje.
Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
22 Neníť žádných temností, ani stínu smrti, kdež by se skryli činitelé nepravosti.
Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
23 Aniž zajisté vzkládá na koho více, tak aby se s Bohem silným souditi mohl.
Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
24 Pyšné stírá bez počtu, a postavuje jiné na místa jejich.
Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
25 Nebo zná skutky jejich; pročež na ně obrací noc, a potříni bývají.
Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
26 Jakožto bezbožné rozráží je na místě patrném,
Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
27 Proto že odstoupili od něho, a žádných cest jeho nešetřili,
kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
28 Aby dokázal, že připouští k sobě křik nuzného, a volání chudých že vyslýchá.
Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
29 (Nebo když on spokojí, kdo znepokojí? A když skryje tvář svou, kdo jej spatří?) Tak celý národ, jako i každého člověka jednostejně,
Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
30 Aby nekraloval člověk pokrytý, aby nebylo lidem ourazu.
ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
31 Jistě žeť k Bohu silnému raději toto mluveno býti má: Ponesuť, nezruším.
Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
32 Mimo to, nevidím-li čeho, ty vyuč mne; jestliže jsem nepravost páchal, neučiním toho víc.
nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
33 Nebo zdali vedlé tvého zdání odplacovati má, že bys ty toho neliboval, že bys ono zvoloval, a ne on? Pakli co víš jiného, mluv.
Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
34 Muži rozumní se mnou řeknou, i každý moudrý poslouchaje mne,
Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
35 Že Job hloupě mluví, a slova jeho nejsou rozumná.
Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
36 Ó by zkušen byl Job dokonale, pro odmlouvání nám jako lidem nepravým,
Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
37 Poněvadž k hříchu svému přidává i nešlechetnost, mezi námi také jen chloubu svou vynáší, a rozmnožuje řeči své proti Bohu.
Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”

< Jób 34 >