< Jeremiáš 16 >

1 I stalo se slovo Hospodinovo ke mně, řkoucí:
Kisha neno la Bwana likanijia:
2 Nepojímej sobě ženy, aniž měj synů neb dcer na místě tomto.
“Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
3 Nebo takto praví Hospodin o synech i dcerách zplozených v místě tomto, a o matkách jejich, kteréž zrodily je, i o jejich otcích, kteříž zplodili je v zemi této:
Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
4 Smrtmi přebolestnými pomrou, nebudou oplakáni, ani pochováni; místo hnoje na svrchku země budou, a mečem i hladem do konce zhubeni budou. I budou mrtvá těla jejich za pokrm ptactvu nebeskému a šelmám zemským.
“Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
5 Nebo takto praví Hospodin: Nevcházej do domu smutku, aniž choď kvíliti, aniž jich lituj; odjal jsem zajisté pokoj svůj od lidu tohoto, dobrotivost i slitování, dí Hospodin.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
6 Když pomrou velicí i malí v zemi této, nebudou pochováni, aniž kvíliti budou nad nimi, aniž se zřeží, aniž sobě lysiny zdělají pro ně.
“Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
7 Aniž jim dadí jísti, aby v truchlosti potěšovali jich nad mrtvým, aniž jich napojí z číše potěšení po otci jejich neb matce jejich.
Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
8 Tolikéž do domu hodování nechoď, abys sedati měl s nimi při jídle a pití.
“Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
9 Nebo takto praví Hospodin zástupů, Bůh Izraelský: Aj, já způsobím, aby nebývalo na místě tomto před očima vašima a za dnů vašich hlasu radosti, ani hlasu veselé, hlasu ženicha, ani hlasu nevěsty.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
10 Když pak oznámíš lidu tomuto všecka slova tato, a řeknou-liť: Proč vyřkl Hospodin proti nám všecko zlé veliké toto, a jaká jest nepravost naše, aneb jaký hřích náš, jímž jsme hřešili proti Hospodinu Bohu svému?
“Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
11 Tedy rci jim: Proto že opustili mne otcové vaši, dí Hospodin, a chodíce za bohy cizími, sloužili jim, a klaněli se jim, mne pak opustili, a zákona mého neostříhali.
Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
12 Vy pak mnohem jste hůře činili nežli otcové vaši; nebo aj, vy chodíte jeden každý podlé zdání srdce svého zlého, neposlouchajíce mne.
‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
13 Pročež hodím vámi z země této do země, o níž nevíte vy, ani otcové vaši, a sloužiti budete tam bohům cizím dnem i nocí, dokudž neučiním vám milosti.
Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
14 Protož aj, dnové jdou, dí Hospodin, v nichž nebude říkáno více: Živť jest Hospodin, kterýž vyvedl syny Izraelské z země Egyptské,
“Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
15 Ale: Živť jest Hospodin, kterýž vyvedl syny Izraelské z země půlnoční a ze všech zemí, do nichž je byl rozehnal, když je zase přivedu do země jejich, kterouž jsem dal otcům jejich.
bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
16 Aj, já pošli k rybářům mnohým, dí Hospodin, aby je vylovili; potom pošli i k mnohým lovcům, aby je zlapali na všeliké hoře, a na všelikém pahrbku, i v děrách skalních.
“Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
17 Hledím na všecky cesty jejich, nejsouť tajné přede mnou, aniž jest skryta nepravost jejich před očima mýma.
Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
18 I odplatím jim prvé dvojnásobně za nepravost jejich a hřích jejich, proto že zemi mnou poškvrnili těly mrtvými ohyzdnými, a ohavnostmi svými naplnili dědictví mé.
Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
19 Hospodine, sílo má a hrade můj, i útočiště mé v den ssoužení, k toběť přijdou národové od končin země, a řeknou: Jistě žeť se falše drželi otcové naši, marnosti a právě neužitečných věcí.
Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
20 Zdaliž udělá sobě člověk bohy, poněvadž sami nejsou bohové?
Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
21 Protož aj, já způsobím to, aby poznali té chvíle, způsobím, aby poznali ruku mou i moc mou, a zvědít, že jméno mé jest Hospodin.
“Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.

< Jeremiáš 16 >