< Izaiáš 49 >

1 Poslouchejte mne ostrovové, a pozorujte národové dalecí: Hospodin hned z života povolal mne, od života matky mé v pamět uvedl jméno mé,
Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
2 A učinil ústa má podobná meči ostrému. V stínu ruky své skryl mne, a učiniv ze mne střelu vypulerovanou, v toule svém schoval mne.
Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
3 A řekl mi: Služebník můj jsi, v Izraeli skrze tebe oslaven budu.
Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
4 Já pak řekl jsem: Nadarmo jsem pracoval, daremně a marně sílu svou jsem strávil. Ale však soud můj jestiť u Hospodina, a práce má u Boha mého.
Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
5 A nyní dí Hospodin, kterýž mne sformoval hned od života za služebníka svého, abych zase přivedl k němu Jákoba; (byť pak i nebyl sebrán Izrael, slávu však mám před očima Hospodinovýma; nebo Bůh můj jest síla má);
Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
6 I to řekl Hospodin: Máloť by to bylo, abys mi byl služebníkem ku pozdvižení pokolení Jákobových, a k navrácení ostatků Izraelských; protož dal jsem tě za světlo pohanům, abys byl spasení mé až do končin země.
yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
7 Toto praví Hospodin vykupitel Izraelův, Svatý jeho, tomu, jímž pohrdá každý, a jehož sobě oškliví národové, služebníku panujících: Králové, vidouce tě, povstanou, a knížata klaněti se budou pro Hospodina, kterýž věrný jest, Svatého Izraelského, jenž tě vyvolil.
Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
8 Toto praví Hospodin: V čas milosti vyslyším tě, a ve dni spasení spomohu tobě. Nadto ostříhati tě budu, a dám tě v smlouvu lidu, abys utvrdil zemi, a v dědictví uvedl dědictví zpuštěná;
Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
9 Abys řekl vězňům: Vyjděte, těm, kteříž jsou ve tmách: Zjevte se. I budou se pásti podlé cest, a na všech místech vysokých bude pastva jejich.
kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
10 Nebudou lačněti ani žízniti, nebude na ně bíti horko ani slunce; nebo slitovník jejich zprovodí je, a podlé pramenů vod povede je.
Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
11 Přes to způsobím na všech horách svých cesty, a silnice mé vyvýšeny budou.
Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
12 Aj, tito zdaleka přijdou, aj, onino od půlnoci a od moře, a jiní z země Sinim.
Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
13 Prozpěvujte nebesa, a plésej země, a zvučně prokřikujte hory; neboť jest potěšil Hospodin lidu svého, a nad chudými svými slitoval se.
Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
14 Ale řekl Sion: Opustiltě mne Hospodin, a Pán zapomenul se na mne.
Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
15 I zdaliž se může zapomenouti žena nad nemluvňátkem svým, aby se neslitovala nad plodem života svého? A byť se pak ony zapomněly, já však nezapomenu se na tě.
“Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
16 Aj, na dlaních vyryl jsem tě, zdi tvé jsou vždycky přede mnou.
Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
17 Pospíšíť k tobě synové tvoji, ti pak, kteříž tě bořili a kazili, odejdou od tebe.
Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
18 Pozdvihni vůkol očí svých, a pohleď, všickni ti shromáždíce se, přijdou k tobě. Živť jsem já, praví Hospodin, že se jimi všemi jako okrasou přioděješ, a otočíš se jimi jako halží nevěsta,
Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
19 Proto že pustiny tvé, a pouště tvé, a zbořeniny země tvé že tehdáž těsné budou, příčinou obyvatelů, když vzdáleni budou ti, kteříž tě zžírali;
“Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
20 Tak že řeknou před tebou synové siroby tvé: Těsné mi jest toto místo, ustup mi, abych bydliti mohl.
Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
21 I díš v srdci svém: Kdo mi naplodil těchto? Nebo jsem já byla osiřelá a osamělá, sem i tam přecházející a odcházející. Tyto, pravím, kdo vychoval? Aj, pozůstala jsem byla sama jediná. Kdež tito byli?
Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
22 Toto praví Panovník Hospodin: Aj, já pozdvihnu k národům ruky své, a k lidem vyzdvihnu korouhev svou, aby přinesli syny tvé na rukou, a dcery tvé aby na plecech neseny byly.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
23 I budou králové pěstounové tvoji, a královny jejich chovačky tvé. Tváří k zemi skláněti se budou před tebou, a prach noh tvých lízati budou, a poznáš, že jsem já Hospodin, a že nebývají zahanbeni, kteříž na mne očekávají.
Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
24 Ale díš: Zdaliž odjato bude reku udatnému to, což uchvátil? A zdaž zajatý lid spravedlivého vyproštěn bude?
Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
25 Anobrž tak praví Hospodin: I zajatý lid reku udatnému odjat bude, a to, což uchvátil násilník, vyproštěno bude; nebo s tím, kterýž se s tebou nesnadní, já se nesnadniti budu, a syny tvé já vysvobodím.
Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
26 A nakrmím ty, kteříž tě utiskují, vlastním masem jejich, a jako mstem krví svou se zpijí. I poznáť všeliké tělo, že já Hospodin jsem spasitel tvůj, a vykupitel tvůj Bůh silný Jákobův.
Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

< Izaiáš 49 >