< 1 Mojžišova 46 >

1 Tedy bral se Izrael se vším, což měl; a přišed do Bersabé, obětoval oběti Bohu otce svého Izáka.
Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
2 I mluvil Bůh Izraelovi u vidění nočním, řka: Jákobe, Jákobe! Kterýžto odpověděl: Aj, teď jsem.
Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
3 I řekl: Já jsem ten Bůh silný, Bůh otce tvého. Neboj se sstoupiti do Egypta, nebo v národ veliký tam tebe učiním.
Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
4 Já sstoupím s tebou do Egypta, a já tě také i zase přivedu; a Jozef položí ruku svou na oči tvé.
Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
5 Vstal tedy Jákob z Bersabé; a synové Izraelovi vzali Jákoba otce svého, a děti své s ženami svými na vozy, kteréž poslal pro něho Farao.
Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
6 Pobrali také dobytek svůj, a zboží své, kteréhož nabyli v zemi Kananejské; a přišli do Egypta, Jákob i všecko símě jeho s ním.
Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
7 Syny i vnuky, dcery i vnučky své, a všecku rodinu svou uvedl s sebou do Egypta.
Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
8 A tato jsou jména synů Izraelových, kteříž vešli do Egypta: Jákob a synové jeho. Prvorozený Jákobův Ruben.
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
9 A synové Rubenovi: Enoch, Fallu, Ezron a Charmi.
Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
10 Synové pak Simeonovi: Jamuel, Jamin, Ahod, Jachin, Sohar a Saul, syn jedné ženy Kananejské.
Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
11 Synové Léví: Gerson, Kahat a Merari.
Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
12 Synové Judovi: Her, Onan, Séla, Fáres a Zára. (Ale umřel Her a Onan v zemi Kananejské.) Fáres pak měl syny: Ezrona a Hamule.
Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
13 Synové Izacharovi: Tola, Fua, Job a Simron.
Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
14 A synové Zabulonovi: Sared, Elon a Jahelel.
Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
15 Tiť jsou synové Líe, kteréž porodila Jákobovi v Pádan Syrské, a Dínu, dceru jeho. Všech duší synů i dcer jeho bylo třidceti a tři.
Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
16 Synové Gád: Sefon, Aggi, Suni, Esebon, Heri, Arodi a Areli.
Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
17 Synové Asser: Jemna, Jesua, Jesui, Beria, a Serach sestra jejich. Synové pak Beriovi: Heber a Melchiel.
Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
18 To jsou synové Zelfy, kterouž Lában dal Líe dceři své; a ty porodila Jákobovi, šestnácte duší.
Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
19 Synové pak Ráchel, manželky Jákobovy: Jozef a Beniamin.
Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
20 A Jozefovi narodili se v zemi Egyptské z Asenat, dcery Putifera knížete On, Manasses a Efraim.
Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
21 Ale synové Beniaminovi: Béla, Becher, Asbel, Gera, Náman, Echi, Roz, Mufim, Chuppim a Ared.
Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
22 Tiť jsou synové Ráchel, kteréž porodila Jákobovi; všech duší čtrnáct.
Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
23 A syn Danův: Chusim.
Mwana wa Dani ni: Hushimu.
24 Synové pak Neftalím: Jaziel, Guni, Jezer a Sallem.
Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
25 Ti jsou synové Bály, kterouž Lában dal Ráchel dceři své, a ty porodila Jákobovi; všech duší sedm.
Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
26 Všech duší, kteréž vešly s Jákobem do Egypta, což jich pošlo z bedr jeho, kromě žen synů Jákobových, všech duší bylo šedesáte a šest.
Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
27 K tomu synové Jozefovi, kteříž se jemu narodili v Egyptě, dva. A tak všech duší domu Jákobova, kteréž vešly do Egypta, bylo sedmdesáte.
Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
28 Poslal pak Judu napřed k Jozefovi, aby oznámil jemu prvé, než přišel do Gesen. A tak přišli do země Gesen.
Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
29 Jozef pak zapřáh do svého vozu, vyjel vstříc Izraelovi otci svému do Gesen; a jakž ho Jákob uzřel, padl na jeho šíji, a plakal dlouho na šíji jeho.
gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
30 I řekl Izrael Jozefovi: Nechť již umru, když jsem viděl tvář tvou; nebo ty ještě jsi živ.
Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
31 Jozef pak řekl bratřím svým a domu otce svého: Pojedu a zvěstuji Faraonovi, a dím jemu: Bratří moji a dům otce mého, kteříž bydlili v zemi Kananejské, přišli ke mně.
Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
32 Ale jsou pastýři stáda, nebo s dobytkem se obírají; protož ovce své a voly, i cožkoli mají, přihnali.
Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
33 A když by povolal vás Farao, a řekl: Jaký jest obchod váš?
Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
34 Odpovíte: Dobytkem se živili služebníci tvoji od mladosti své až do této chvíle, i my i otcové naši; abyste bydlili v zemi Gesen; nebo v mrzkosti mají Egyptští všecky pastýře stáda.
Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”

< 1 Mojžišova 46 >