< 1 Mojžišova 29 >

1 Tedy Jákob vstav, odšel do země východní.
Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika katika nchi ya watu wa mashariki.
2 A pohleděv, uzřel studnici v poli a tři stáda ovcí, ana se složila při ní; nebo z té studnice napájeli stáda; a kámen veliký byl navrchu studnice.
Hata alipotazama, akaona kisima kondeni, na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake. Kwani kutoka katika hicho wangeyanywesha makundi, na jiwe juu ya mdomo wa kisima lilikuwa kubwa.
3 Shánívána pak tam bývala všecka stáda, a teprv odvalovali kámen ten od vrchu té studnice, a napájeli dobytky; potom zas přivalovali kámen na vrch studnice, na místo jeho.
Wakati makundi yote yangekusanyika pale, wachungaji wangevingirisha jiwe kutoka katika mdomo wa kisima na kuwanywesha kondoo, na kisha kurudisha jiwe juu ya mdomo wa kisima, mahali pake.
4 Tedy řekl jim Jákob: Bratří moji, odkud jste? Kteřížto odpověděli: Jsme z Cháran.
Yakobo akawambia, “Ndugu zangu, ninyi mnatokea wapi?” nao wakasema, “Tunatoka Harani.”
5 I řekl jim: Znáte-li Lábana, syna Náchorova? A oni řekli: Známe.
Akawambia, “Mnamfahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakasema, “Tunamfahamu.”
6 I dí opět k nim: Dobře-li se má? Odpověděli: Dobře, a aj, Ráchel dcera jeho tamto jde s dobytkem.
Akawambia, “Je hajambo?” Wakasema, “Hajambo, na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo.”
7 Tedy řekl: Však ještě daleko do večera, aniž ještě čas, aby dobytek byl sehnán; napojte stáda, a jděte, paste.
Yakobo akasema, “Tazama, ni mchana. Siyo wakati wa kukusanya kondoo pamoja. Mnapaswa kuwanywesha kondoo na kisha mkaenda na kuwaacha wachunge.”
8 A oni odpověděli: Nemůžeme, než až se všecka stáda seženou, a odvalen bude kámen od svrchku studnice, abychom napojili ovce.
Wakamwambia, “Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja. Ndipo wanaume watakapovingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na ndipo tutakapowanywesha kondoo.”
9 Když on ještě mluvil s nimi, přišla k tomu Ráchel s stádem otce svého; neb ona pásla stádo.
Wakati bado Yakobo anaongea nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa babaye, kwani alikuwa akiwachunga.
10 Tedy Jákob uzřev Ráchel, dceru Lábana ujce svého, a stádo jeho, přistoupil a odvalil ten kámen od vrchu studnice, a napojil stádo Lábana ujce svého.
Yakobo alipomwona Raheli, binti wa Labani, kaka wa mamaye, na kondoo wa Labani, kaka wa mama yake, Yakobo akaja juu, akalivingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na akawanywesha kondoo wa Labani, kaka wa mama yake.
11 A políbil Jákob Ráchel, a povýšiv hlasu svého, plakal.
Yakobo akambusu Raheli na akalia kwa sauti.
12 Oznámil jí pak byl Jákob, že jest bratr otce jejího, a že jest syn Rebeky; a ona přiběhši, oznámila to otci svému.
Yakobo akamwambia Raheli kwamba alikuwa ni ndugu wa baba yake, na kwamba alikuwa mwana wa Rebeka. Kisha yeye akakimbia kumwambia baba yake.
13 I stalo se, když Lában uslyšel pověst o Jákobovi, synu sestry své, že vyběhl proti němu, a objav ho, políbil, a uvedl do domu svého; on pak vypravoval Lábanovi o všech těch věcech.
Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akaenda kukutana naye, akamkumbatia, akambusu, na kumleta nyumbani kwake. Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote.
14 Jemužto odpověděl Lában: Jistě kost má a tělo mé jsi. I zůstal s ním přes celý měsíc.
Labani akamwambia, “Kwa hakika wewe ni mfupa wangu na nyama yangu.” Kisha Yakobo akakaa naye kama mwezi mmoja.
15 Tedy řekl Lában Jákobovi: Zdali proto, že jsi bratr můj, darmo mi sloužiti budeš? Pověz mi, jaká má býti mzda tvá?
Kisha Labani akamwambia Yakobo, “Je unitumikie bure kwa kuwa wewe ni ndugu yangu? Niambie, ujira wako utakuwaje?
16 (Měl pak Lában dvě dcery; jméno starší Lía, a jméno mladší Ráchel.
Basi Labani alikuwa na binti wawili. Jina la mkubwa lilikuwa ni Lea, na jina la mdogo lilikuwa Raheli.
17 Než Lía měla oči mdlé, ale Ráchel byla pěkné postavy a krásné tváři.
Macho ya Lea yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo na mwonekano.
18 I miloval Jákob Ráchel.) Řekl tedy: Buduť sloužiti sedm let za Ráchel, dceru tvou mladší.
Yakobo alimpenda Raheli, hivyo akasema, “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Raheli, binti yako mdogo.”
19 Odpověděl Lában: Lépeť jest, abych ji tobě dal, nežli bych ji dal muži jinému; zůstaniž se mnou.
Labani akasema, Itakuwa vema kukupa wewe, kuliko kumpa mtu mwingine. Kaa nami.”
20 Takž Jákob sloužil za Ráchel sedm let; a bylo před očima jeho jako něco málo dnů, proto že laskav byl na ni.
Hivyo Yakobo akamtumikia kwa miaka saba kwa ajili ya Raheli; nayo ilionekana kwake kama siku chache tu, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake.
21 Potom řekl Jákob k Lábanovi: Dejž mi ženu mou; nebo vyplněni jsou dnové moji, abych všel k ní.
Kisha Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia - ili kwamba nimwoe!
22 Tedy sezval Lában všecky muže místa toho, a učinil hody.
Hivyo Labani akawaalika watu wa mahali hapo na kuandaa sherehe.
23 U večer pak vzav Líu, dceru svou, uvedl ji k němu; a on všel k ní.
Wakati wa jioni, Labani akamchukua Lea binti yake mkubwa na kumleta kwa Yakobo, aliyelala naye.
24 Dal také Lában Zelfu děvku svou Líe, dceři své, za služebnici.
Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa kuwa mjakazi wa Lea.
25 A když bylo ráno, poznal, že jest Lía. I řekl k Lábanovi: Což jsi mi to učinil? Zdaliž jsem za Ráchel nesloužil u tebe? Pročežs mne tedy oklamal?
Ilipofika asubuhi, tazama, kumbe ni Lea! Yakobo akamwambia Labani, “Ni nini hiki ulichonifanyia? Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Kwa nini basi umenihadaa?
26 Odpověděl Lában: Nebývá toho v kraji našem, aby vdávána byla mladší dříve, než prvorozená.
Labani akamwambia, “Siyo utamaduni wetu kumtoa bindi mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza.
27 Vyplň týden této; dámeť potom i tuto za službu, kterouž sloužiti budeš u mne ještě sedm let jiných.
Timiza juma la bibi arusi, na tutakupa yule mwingine pia kwa mbadala wa kunitumikia miaka mingine saba.”
28 I udělal tak Jákob, a vyplnil týden její. Potom dal mu Ráchel dceru svou za manželku.
Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea. Kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
29 Dal také Lában Ráchel, dceři své, Bálu, děvku svou za služebnici.
Lakini pia Labani akampa Raheli binti yake Bilha, kuwa mjakazi wake.
30 Tedy všel také k Ráchel, a miloval ji více než Líu; i sloužil u něho ještě sedm let jiných.
Hivyo Yakobo akalala na Raheli, pia, lakini akampenda Raheli zaidi ya Lea. Hivyo Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka saba mingine.
31 Vida pak Hospodin, že Lía nemá lásky, otevřel život její; a Ráchel nechal neplodné.
Yahwe akaona kwamba Lea hakupendwa, hivyo akalifungua tumbo lake, lakini Raheli hakuwa na mtoto.
32 Tedy počala Lía a porodila syna, a nazvala jméno jeho Ruben; nebo řekla: Jistě viděl Hospodin trápení mé; jižť nyní milovati mne bude muž můj.
Lea akashika mimba na kuzaa mwana, naye akamwita Rubeni. Kwani alisema, “Kwa sababu Yahwe ameliangalia teso langu; bila shaka mme wangu sasa atanipenda.”
33 I počala opět a porodila syna, a řekla: Jistě uslyšel Hospodin, že jsem v nenávisti, protož dal mi i tohoto. A nazvala jméno jeho Simeon.
Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Kwa sababu Yahwe amesikia kwamba sipendwi, kwa hiyo amenipa mwana mwingine,” na akamwita Simoni.
34 A opět počala a porodila syna, a řekla: Již nyní připojí se ke mně muž můj, nebo jsem mu porodila tři syny. Z té příčiny nazváno jest jméno jeho Léví.
Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu mme wangu ataungana nami, kwa kuwa nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akaitwa Lawi.
35 I počala ještě a porodila syna, a řekla: Již nyní chváliti budu Hospodina. Pročež nazvala jméno jeho Juda; i přestala roditi.
Akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu nitamsifu Yahwe.” Kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; kisha akaacha kuzaa watoto.

< 1 Mojžišova 29 >