< 1 Mojžišova 10 >

1 Tito jsou pak rodové synů Noé, Sema, Chama a Jáfeta, jimž se tito synové zrodili po potopě.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 Synové Jáfetovi: Gomer a Magog, a Madai, a Javan, a Tubal, a Mešech, a Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 Synové pak Gomerovi: Ascenez, Rifat, a Togorma.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 Synové pak Javanovi: Elisa a Tarsis, Cetim a Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 Od těch rozděleni jsou ostrovové národů po krajinách jejich, každý podlé jazyku svého, vedlé čeledi své, v národech svých.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 Synové pak Chamovi: Chus a Mizraim a Put a Kanán.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 A synové Chusovi: Sába, Evila, a Sabata, a Regma, a Sabatacha. Synové pak Regmovi: Sába a Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 Zplodil také Chus Nimroda; onť jest počal býti mocným na zemi.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 To byl silný lovec před Hospodinem; protož se říká: Jako Nimrod silný lovec před Hospodinem.
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Počátek pak jeho království byl Babylon a Erech, Achad a Chalne, v zemi Sinear.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 Z země té vyšel do Assur, kdežto vystavěl Ninive, a Rohobot město, a Chále,
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 A Rezen mezi Ninive a mezi Chále; toť jest město veliké.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 Mizraim pak zplodil Ludim a Anamim, a Laabim, a Neftuim,
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 A Fetruzim, a Chasluim, (odkudž pošli Filistinští) a Kafturim.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Kanán pak zplodil Sidona prvorozeného svého, a Het,
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 A Jebuzea, a Amorea, a Gergezea,
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 A Hevea, a Aracea, a Sinea,
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 A Aradia, a Samarea, a Amatea; a potom odtud rozprostřely se čeledi Kananejských.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 A bylo pomezí Kananejských od Sidonu, když jdeš k Gerar až do Gázy; a odtud když jdeš k Sodomě a Gomoře, a Adama a Seboim až do Lázy.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Ti jsou synové Chamovi po čeledech svých, vedlé jazyků svých, po krajinách svých, v národech svých.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Semovi také, otci všech synů Heber, bratru Jáfeta staršího zrozeni jsou synové.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 A tito jsou synové Semovi: Elam, a Assur, a Arfaxad, a Lud, a Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 Synové pak Aramovi: Hus, a Hul, a Geter, a Mas.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 Potom Arfaxad zplodil Sále; a Sále zplodil Hebera.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 Heberovi také narodili se dva synové; jméno jednoho Peleg, proto že za dnů jeho rozdělena byla země, a jméno bratra jeho Jektan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Jektan pak zplodil Elmodada, a Salefa, a Azarmota, a Járe,
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 A Adoráma, a Uzala, a Dikla,
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 A Obale, a Abimahele, a Sebai,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 A Ofira, a Evila, a Jobaba; všickni ti jsou synové Jektanovi.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 A bylo bydlení jejich od Mesa, když jdeš k Sefar hoře na východ slunce.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 Tiť jsou synové Semovi po čeledech svých, vedlé jazyků svých, po krajinách svých, v národech svých.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 Ty jsou čeledi synů Noé po rodech svých, v národech svých; a od těch rozdělili se národové na zemi po potopě.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< 1 Mojžišova 10 >