< Ezechiel 5 >

1 Potom ty synu člověčí, vezmi sobě nůž ostrý, totiž břitvu holičů, vezmi jej sobě, a ohol ním hlavu i bradu svou. Potom vezma sobě váhu, rozděl to.
“Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
2 Třetinu ohněm spal u prostřed města, když se vyplní dnové obležení; zatím vezma druhou třetinu, posekej mečem okolo něho; ostatní pak třetinu rozptyl u vítr. Nebo mečem dobytým budu je stihati.
Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
3 A však odejmi odtud něco málo, a zavaž do křídel svých.
Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
4 A i z těch ještě vezma, uvrz je do prostřed ohně, a spal je ohněm, odkudž vyjde oheň na všecken dům Izraelský.
Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
5 Takto praví Panovník Hospodin: Tento Jeruzalém, kterýž jsem postavil u prostřed pohanů, a vůkol otočil krajinami,
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
6 Změnil soudy mé v bezbožnost více než pohané, a ustanovení má více než jiné země, kteréž jsou vůkol něho; nebo soudy mými pohrdli, a v ustanoveních mých nechodili.
Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
7 Protož takto praví Panovník Hospodin: Proto že mnohem více než pohané, kteříž jsou vůkol vás, v ustanoveních mých nechodili jste, a soudů mých nečinili jste, nýbrž ani tak jako pohané, kteříž jsou vůkol vás, soudů nekonali jste:
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
8 Protož takto praví Panovník Hospodin: Aj, já na tebe, aj já, a vykonám u prostřed tebe soudy před očima pohanů.
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
9 Nebo učiním při tobě to, čehož jsem prv neučinil, a čehož podobně neučiním více pro všecky ohavnosti tvé,
Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
10 Tak že otcové jísti budou syny u prostřed tebe, a synové jísti budou otce své, a vykonám proti tobě soudy, a rozptýlím všecky ostatky tvé na všecky strany.
Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
11 Protož živť jsem já, praví Panovník Hospodin, že poněvadž jsi ty svatyně mé poškvrnil všelikými mrzkostmi svými, a všelikými ohavnostmi svými, i já také zlehčím tebe, a neodpustíť oko mé, a nikoli se neslituji.
Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
12 Třetina tebe morem zemře a hladem zhyne u prostřed tebe, a třetina druhá mečem padne vůkol tebe, ostatní pak třetinu na všecky stany rozptýlím, a mečem dobytým stihati je budu.
Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
13 A tak do konce vylit bude hněv můj, a dotru prchlivostí svou na ně, i potěším se. I zvědíť, že já Hospodin mluvil jsem v horlivosti své, když vykonám prchlivost svou na nich,
“Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
14 A obrátím tě v poušť, a dám tě v útržku mezi národy, kteříž jsou vůkol tebe, před očima každého tudy jdoucího.
“Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
15 A tak budeš k útržce, posměchu, k hroznému příkladu a k užasnutí národům, kteříž jsou vůkol tebe, tehdáž když vykonám proti tobě soudy v hněvě a v prchlivosti a v žehrání zůřivém. Já Hospodin mluvil jsem.
Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
16 Tehdáš když vystřelím jízlivé střely hladu k záhubě vaší, kteréž vystřelím, abych vás vyhubil, a hlad shromáždě proti vám, zlámi vám hůl chleba.
Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
17 Pošli zajisté na vás hlad a zvěř lítou, kteráž tě na sirobu přivede; i mor a krev přijde na tebe, když uvedu na tě meč. Já Hospodin mluvil jsem.
Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”

< Ezechiel 5 >