< Ezechiel 29 >

1 Léta desátého, desátého měsíce, dvanáctého dne téhož měsíce, stalo se slovo Hospodinovo ke mně, řkoucí:
Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Synu člověčí, obrať tvář svou proti Faraonovi králi Egyptskému, a prorokuj proti němu i proti všemu Egyptu.
“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
3 Mluv a rci: Takto praví Panovník Hospodin: Aj, já proti tobě jsem, ó Faraone králi Egyptský, draku veliký, kterýž ležíš u prostřed řek svých, ješto říkáš: Já mám řeku svou, já zajisté jsem ji přivedl sobě.
Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
4 Protož dám udici do čelistí tvých, a učiním, že zváznou ryby řek tvých na tvých šupinách; i vyvleku tě z prostředku řek tvých, i všecky ryby řek tvých na šupinách tvých zvázlé.
Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
5 A nechám tě na poušti, tebe i všech ryb řek tvých. Na svrchku pole padneš, nebudeš sebrán ani shromážděn; šelmám zemským i ptactvu nebeskému dám tě k sežrání.
Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
6 I zvědí všickni obyvatelé Egyptští, že já jsem Hospodin, proto že jste holí třtinovou domu Izraelskému.
Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
7 Když se chytají tebe rukou, lámeš se, a roztínáš jim všecko rameno; a když se na tě zpodpírají, ztroskotána býváš, ačkoli nastavuješ jim všech bedr.
Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
8 Protož takto praví Panovník Hospodin: Aj, já přivedu na tě meč, a vypléním z tebe lidi i hovada.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
9 I bude země Egyptská pustinou a pouští, i zvědí, že já jsem Hospodin, proto že říkal: Řeka má jest, já zajisté jsem ji přivedl.
Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
10 Protož aj, já budu proti tobě i proti řece tvé, a obrátím zemi Egyptskou v pustiny, v poušť přehroznou od věže Sevéne až do pomezí Mouřenínského.
kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
11 Nepůjdeť přes ni noha člověka, ani noha dobytčete půjde přes ni, a nebude v ní bydleno za čtyřidceti let.
Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
12 A tak uvedu zemi Egyptskou v pustinu nad jiné země pusté, a města její nad jiná města zpuštěná pustá budou za čtyřidceti let, když rozptýlím Egyptské mezi národy, a rozženu je do rozličných zemí.
Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
13 A však takto praví Panovník Hospodin: Po skonání čtyřidceti let shromáždím Egyptské z národů, kamž rozptýleni budou.
“‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
14 A přivedu zase zajaté Egyptské, a uvedu je zase do země Patros, do země přebývání jejich, i budou tam královstvím sníženým.
Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
15 Mimo jiná království bude sníženější, aniž se bude vynášeti více nad jiné národy; zmenším je zajisté, aby nepanovali nad národy.
Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
16 I nebude více domu Izraelskému doufáním, kteréž by na pamět přivodilo nepravost, když by se obraceli za nimi; nebo zvědí, že já jsem Panovník Hospodin.
Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
17 Potom bylo dvadcátého sedmého léta, prvního měsíce, prvního dne, že se stalo slovo Hospodinovo ke mně, řkoucí:
Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
18 Synu člověčí, Nabuchodonozor král Babylonský podrobil vojsko své v službu velikou proti Týru. Každá hlava oblezla, a každé rameno odříno jest, mzdy pak nemá, on ani vojsko jeho, z Týru za tu službu, kterouž sloužili proti němu.
“Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
19 Z té příčiny takto praví Panovník Hospodin: Aj, já dávám Nabuchodonozorovi králi Babylonskému zemi Egyptskou, aby pobral zboží její, a rozebral loupeže její, i rozchvátal kořisti její, aby mělo mzdu vojsko jeho.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
20 Za práci jejich, kterouž mi sloužili, dám jim zemi Egyptskou, proto že mně pracovali, praví Panovník Hospodin.
Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
21 V ten den rozkáži vypučiti se rohu domu Izraelského. Tobě též způsobím, že otevřeš ústa u prostřed nich, i zvědí, že já jsem Hospodin.
“Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”

< Ezechiel 29 >