< 2 Mojžišova 18 >

1 Uslyšel pak Jetro, kníže Madianské, test Mojžíšův, o všech věcech, kteréž učinil Bůh Mojžíšovi a Izraelovi, lidu svému, že vyvedl Hospodin Izraele z Egypta.
Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
2 A vzal Jetro, test Mojžíšův, Zeforu manželku Mojžíšovu, kterouž byl odeslal,
Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
3 A dva syny její, z nichž jméno jednoho Gerson; nebo řekl: Příchozí jsem byl v zemi cizí;
pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
4 Jméno pak druhého Eliezer; nebo řekl: Bůh otce mého spomocník můj byl, a vytrhl mne od meče Faraonova.
Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
5 I přišel Jetro, test Mojžíšův, s syny jeho i s ženou jeho k Mojžíšovi na poušť, kdež se byl položil při hoře Boží.
Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
6 A vzkázal Mojžíšovi: Já, test tvůj Jetro, jdu k tobě, i žena tvá a oba synové její s ní.
Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
7 I vyšel Mojžíš proti testi svému, a pokloniv se, políbil ho. I ptal se jeden druhého, jak se má; potom vešli do stanu.
Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
8 A vypravoval Mojžíš testi svému všecko, což učinil Hospodin Faraonovi a Egyptským pro Izraele, a o všech nevolech, kteréž přicházely na ně na cestě, a jak je vysvobodil Hospodin.
Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
9 I radoval se Jetro ze všeho dobrého, což učinil Hospodin Izraelovi, a že vytrhl jej z ruky Egyptských.
Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
10 A řekl Jetro: Požehnaný Hospodin, kterýž vytrhl vás z ruky Egyptských a z ruky Faraonovy, kterýž vytrhl ten lid z poroby Egyptské.
Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
11 Nyní jsem poznal, že větší jest Hospodin nade všecky bohy; nebo touž věcí, kterouž se vyvyšovali, on je převýšil.
Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
12 A vzal Jetro, test Mojžíšův, zápal a oběti, kteréž obětoval Bohu. Potom přišel Aron a všickni starší Izraelští, aby jedli chléb s tchánem Mojžíšovým před Bohem.
Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
13 Nazejtří pak posadil se Mojžíš, aby soudil lid; a stál lid před Mojžíšem od jitra až do večera.
Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
14 Vida pak test Mojžíšův všecku práci jeho při lidu, řekl: Co jest to, což děláš s lidem? Proč ty sám sedíš, a všecken lid stojí před tebou od jitra až do večera?
Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
15 Odpověděl Mojžíš tchánu svému: Přichází ke mně lid raditi se s Bohem.
Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
16 Když mají o nějakou věc činiti, přicházejí ke mně, a soud činím mezi stranami, a oznamuji rady Boží a ustanovení jeho.
Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
17 I řekl jemu test Mojžíšův: Nedobře děláš.
Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
18 Tudíž tak ustaneš i ty i lid, kterýž s tebou jest. Nad možnost tvou těžká jest tato věc, nebudeš jí moci sám dosti učiniti.
Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
19 Protož nyní uposlechni řeči mé; poradím tobě, a bude Bůh s tebou. Stůj ty za lid před Bohem, a donášej věci nesnadné k Bohu.
Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
20 A vysvětluj jim řády a zákony, a oznamuj jim cestu, po níž by šli, a co by dělati měli.
Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
21 Vyhledej také ze všeho lidu muže statečné, bohabojné, muže pravdomluvné, kteříž v nenávisti mají lakomství, a ustanov z nich knížata nad tisíci, setníky, padesátníky a desátníky.
Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
22 Oni ať soudí lid každého času. Což bude většího, vznesou na tebe, a menší pře sami nechť soudí; a tak lehčeji bude tobě, když jiní ponesou břímě s tebou.
Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
23 Jestliže to učiníš a rozkážeť Bůh, budeš moci trvati; také i všecken lid tento navracovati se bude k místům svým pokojně.
Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
24 Tedy uposlechl Mojžíš řeči tchána svého, a učinil všecko, což on řekl.
Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
25 A vybral Mojžíš muže statečné ze všeho Izraele, a ustanovil je hejtmany nad lidem, knížata nad tisíci, setníky, padesátníky a desátníky,
Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
26 Kteříž soudili lid každého času. Nesnadnější věci vznášeli na Mojžíše, všecky pak menší pře sami soudili.
Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
27 Potom propustil Mojžíš tchána svého; i odšel do země své.
Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.

< 2 Mojžišova 18 >