< Ester 4 >

1 Mardocheus pak zvěděv všecko to, což se bylo stalo, roztrhl roucho své, a vzal na sebe žíni a popel, a jda po městě, křičel křikem velikým a žalostným.
Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu.
2 A přišel až před bránu královskou; nebo žádný neměl vcházeti do brány královské v oděvu žíněném.
Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia.
3 V každé také krajině i místě, kamžkoli slovo královské a výpověd jeho došla, kvílení veliké bylo od Židů, a půst, pláč i úpění, a žíni s popelem podestřeli sobě mnozí.
Katika kila jimbo ambapo amri na agizo la mfalme lilifika, kulikuwa na maombolezo makuu miongoni mwa Wayahudi pamoja na kufunga, kulia na kuomboleza. Watu wengi wakalala juu ya nguo za magunia na majivu.
4 Pročež přišedše děvečky Estery a komorníci její, oznámili jí to. I zarmoutila se královna velmi, a poslala šaty, aby oblékli Mardochea, a aby vzali žíni jeho od něho. Ale on jich nepřijal.
Wajakazi wa Esta na matowashi walipokuja na kumwambia kuhusu Mordekai, alipatwa na huzuni kuu. Alimtumia nguo avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai hakuzikubali.
5 Tedy zavolavši Ester Hatacha, jednoho z komorníků královských, kteréhož jí byl dal za služebníka, poručila mu o Mardocheovi, aby přezvěděl, co a proč by to bylo.
Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmojawapo wa matowashi wa mfalme ambaye alikuwa amewekwa kumhudumia Esta, akamwagiza kutafuta ni nini kilikuwa kikimtaabisha Mordekai na ni kwa nini.
6 Takž vyšel Hatach k Mardocheovi na ulici města, kteráž jest před branou královskou.
Basi Hathaki alitoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanja ulio wazi wa mji mbele ya lango la mfalme.
7 I oznámil jemu Mardocheus všecko, co se mu přihodilo, i o té summě peněz, kterouž připověděl Aman dáti do komory královské proti Židům, k vyhlazení jich.
Mordekai akamwambia kila kitu ambacho kimempata, pamoja na hesabu kamili ya fedha ambazo Hamani aliahidi kulipa katika hazina ya mfalme kwa ajili ya maangamizi ya Wayahudi.
8 K tomu i přípis psané výpovědi, kteráž vyhlášena byla v Susan, aby zhubeni byli, dal jemu, aby ukázal Ester a oznámil jí, a aby jí rozkázal jíti k králi, a milosti hledati u něho, a prositi před tváří jeho za lid svůj.
Akampa nakala ya andiko la amri kwa ajili ya maangamizi yao, lililokuwa limechapishwa huko Shushani, kumwonyesha Esta na kumwelezea. Mordekai akamwambia towashi amshawishi Esta kwenda mbele ya mfalme kuomba rehema na kumsihi kwa ajili ya watu wake.
9 Tedy přišel Hatach, a oznámil Ester slova Mardocheova.
Hathaki akarudi kwa Esta na kumwarifu alilolisema Mordekai.
10 I řekla Ester Hatachovi, a poručila mu oznámiti Mardocheovi:
Kisha Esta akamwamuru Hathaki amweleze Mordekai,
11 Všickni služebníci královští i lid krajin královských vědí, že kterýž by koli muž neb žena všel před krále do síně vnitřní, nejsa povolán, jedno právo o něm jest, aby hrdlo propadl, kromě toho, k komuž by král vztáhl berlu zlatou, že živ zůstane. Já pak nebyla jsem povolána, abych vešla k králi již třidceti dnů.
“Maafisa wote wa mfalme na watu wa majimbo ya ufalme wanajua kuwa mwanaume au mwanamke yeyote ambaye ataingia kumwona mfalme katika ua wa ndani bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu: Atauawa. Njia pekee kinyume na hili ni mfalme kumnyooshea fimbo ya dhahabu ili aishi. Lakini siku thelathini zimepita tangu nilipoitwa kwenda kwa mfalme.”
12 Ale když oznámili Mardocheovi slova Estery,
Wakati Mordekai aliarifiwa maneno ya Esta,
13 Řekl Mardocheus, aby zase oznámeno bylo Esteře: Nemysl sobě, abys zachována býti mohla v domě královském ze všech Židů.
Mordekai alirudisha jibu hili: “Usifikiri kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mfalme wewe pekee katika Wayahudi wote utapona.
14 Nebo jestliže se umlčíš v tento čas, oddechnutí a vysvobození Židům přijde odjinud, ty pak a dům otce tvého zahynete. A kdo ví, ne pro tento-lis čas přišla k tomu království?
Kwa kuwa kama utakaa kimya wakati huu, msaada na ukombozi kwa Wayahudi utatoka mahali pengine, lakini wewe na jamaa ya baba yako mtaangamia. Nani ajuaye kwamba hukuja kwenye nafasi ya mamlaka kwa ajili ya wakati kama huu?”
15 I řekla Ester, aby zase oznámili Mardocheovi:
Kisha Esta alituma jibu hili kwa Mordekai:
16 Jdi a shromažď všecky Židy, což jest jich v Susan, a posťte se za mne, a nejezte ani píte za tři dni, v noci ani ve dne. Já podobně, i panny mé postiti se budou, a teprv vejdu k králi, což však neobyčejné jest, a jestližeť zahynu, nechť zahynu.
“Nenda, kusanya pamoja Wayahudi wote walioko Shushani, nanyi mfunge kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu, usiku na mchana. Mimi na wajakazi wangu tutafunga kama mnavyofanya. Baada ya kufanyika hili, nitakwenda kwa mfalme, hata ingawa ni kinyume cha sheria. Ikiwa ni kuangamia na niangamie.”
17 Tedy šel Mardocheus, a učinil všecko tak, jakž mu poručila Ester.
Kwa hiyo Mordekai alikwenda zake na kutekeleza maagizo yote ya Esta.

< Ester 4 >