< 2 Timoteovi 2 >

1 Protož ty, synu můj, zmocniž se v milosti, kteráž jest v Kristu Ježíši.
Kwa hiyo, wewe mwanangu, utiwe nguvu katika neema iliyondani ya Kristo Yesu.
2 A což jsi slyšel ode mne před mnohými svědky, svěřujž to lidem věrným, kteříž by způsobní byli i jiné učiti.
Na mambo uliyoyasikia kwangu miongoni mwa mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu waaminifu ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
3 A tak ty snášej protivenství, jako ctný rytíř Ježíše Krista.
Shiriki mateso pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu.
4 Žádný, kdož rytěřuje, neplete se v obecné živnosti, aby se svému hejtmanu líbil.
Hakuna askari atumikae wakati huo huo akijihusisha na shughuli za kawaida za maisha haya, ili kwamba ampendeze ofisa wake mkuu.
5 A jestliže by kdo i bojoval, nebudeť korunován, leč by řádně bojoval.
Pia kama mtu akishindana kama mwanariadha, hatapewa taji asiposhindana kwa kufuata kanuni.
6 Pracovati musí i oráč, prve nežli užitku okusí.
Ni Muhimu kwamba mkulima mwenye bidii awe wa kwanza kupokea mgao wa mazao yake.
7 Rozuměj, coť pravím, a dejž tobě Pán ve všem smysl pravý.
Tafakari kuhusu nisemacho, kwa maana Bwana atakupa uelewa katika mambo yote.
8 Pamatujž na to, že Ježíš Kristus vstal z mrtvých, jenž jest z semene Davidova, podle evangelium mého.
Mkumbuke Yesu Kristo, kutoka uzao wa Daudi, ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu. Hii ni kulingana na ujumbe wangu wa Injili,
9 V kterémžto protivenství trpím, až i vězení, jako bych zločinec byl, ale slovo Boží není u vězení.
ambao kwa sababu ya huo ninateswa hata kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi kwa minyororo.
10 Protož všecko to snáším pro vyvolené Boží, aby i oni spasení došli, kteréžto jest v Kristu Ježíši, s slavou věčnou. (aiōnios g166)
Kwa hiyo, navumilia mambo yote kwa ajili ya wale ambao Mungu amekwishawachagua, ili kwamba nao pia waupate wokovu ulio katika Kristo Yesu pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
11 Věrná jest tato řeč. Nebo jestližeť jsme s ním zemřeli, tedy také spolu s ním živi budeme.
Usemi huu ni wakuaminika: “Ikiwa tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia,
12 A trpíme-liť, budeme také spolu s ním kralovati; pakli ho zapíráme, i onť nás zapře.
kama tukivumilia, tutatawala pamoja naye pia, kama tukimkana yeye, naye pia atatukana sisi.
13 A jsme-liť nevěrní, onť zůstává věrný; zapříti sám sebe nemůže.
kama hatutakuwa waaminifu, yeye atabaki kuwa mwaminifu, maana hawezi kujikana mwenyewe.”
14 Tyto věci připomínej, s osvědčováním před obličejem Páně, a ať se o slova nevadí, nebo to k ničemu není užitečné, ale jest ku podvrácení posluchačů.
Endelea kuwakumbusha juu ya mambo haya. Waonye mbele za Mungu waache kubishana kuhusu maneno. Kwa sababu hakuna manufaa katika jambo hili. Kutokana na hili kuna uharibifu kwa wale wanaosikiliza.
15 Pilně se snažuj vydati sebe Bohu milého dělníka, za nějž by se nebylo proč styděti, a kterýž by právě slovo pravdy rozděloval.
Fanya bidii kujionesha kuwa umekubalika kwa Mungu kama mtenda kazi asiye na sababu ya kulaumiwa. Litumie neno la kweli kwa usahihi.
16 Bezbožných pak těch křiků daremních varuj se, neboť velmi rozmnožují bezbožnost,
Jiepushe na majadiliano ya kidunia, ambayo huongoza kwa zaidi na zaidi ya uasi.
17 A řeč jejich jako rak rozjídá se. Z nichžto jest Hymeneus a Filétus,
Majadiliano yao yatasambaa kama donda ndugu. Miongoni mwao ni Himenayo na Fileto.
18 Kteříž při pravdě pobloudili od cíle, pravíce, že by se již stalo vzkříšení, a převracejí víru některých.
Hawa ni watu walioukosa ukweli. Wanasema ya kuwa ufufuo tayari umishatokea. Wanapindua imani ya baadhi ya watu.
19 Ale pevný základ Boží stojí, maje znamení toto: Znáť Pán ty, kteříž jsou jeho, a opět: Odstup od nepravosti každý, kdož vzývá jméno Kristovo.
Hata hivyo, msingi imara wa Mungu unasimama, wenye uandishi huu, “Bwana anawajua walio wake, na kila alitajaye jina la Bwana ni lazima ajitenge na udhalimu.”
20 V domu pak velikém netoliko jsou nádoby zlaté a stříbrné, ale také dřevěné i hliněné, a některé zajisté ke cti, některé pak ku potupě.
Kwenye nyumba ya kitajiri, siyo kwamba vimo vyombo vya dhahabu na shaba tu. Pia kuna vyombo vya miti na udongo. Baadhi ya hivi ni kwa ajili ya matumizi ya heshima na baadhi yake ni kwa matumizi yasiyo ya heshima.
21 Protož jestliže by se kdo očistil od těch věcí, bude nádobou ke cti, posvěcenou, a užitečnou Pánu, ke všelikému skutku dobrému hotovou.
Ikiwa mtu atajitakasa mwenyewe kutoka kwenye matumizi yasiyo ya heshima, yeye ni chombo chenye kuheshimika. Ametengwa maalumu, mwenye manufaa kwa Bwana, na ameandaliwa kwa kila kazi njema.
22 Mládenčích pak žádostí utíkej, ale následuj spravedlnosti, víry, lásky, pokoje, s těmi, kteříž vzývají Pána z srdce čistého.
Zikimbie tamaa za ujanani. Ukifuata haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
23 Bláznivých pak a nevzdělavatelných otázek varuj se, věda, že plodí sváry.
Lakini ukatae upumbavu na maswali ya kipuuzi. Kwani unajua ya kuwa huzaa ugomvi.
24 Na služebníka pak Božího nesluší vaditi se, ale aby byl přívětivý ke všem, způsobný k učení, trpělivý,
Mtumishi wa Bwana hapaswi kugombana, badala yake inampasa kuwa mpole kwa watu wote, awezaye kufundisha, na mvumilivu.
25 Kterýž by v tichosti vyučoval ty, jenž se pravdě protiví, zda by někdy dal jim Bůh pokání ku poznání pravdy,
Ni lazima awaelimishe kwa upole wale wampingao. Yamkini Mungu aweze kuwapatia toba kwa kuifahamu kweli.
26 Aby sami k sobě přijdouce, dobyli se z osidla ďáblova, od něhož jsou zjímáni k vykonávání jeho vůle.
Waweze kupata ufahamu tena na kuepuka mtego wa Shetani, baada ya kuwa wametekwa na yeye kwa ajili ya mapenzi yake.

< 2 Timoteovi 2 >