< 2 Samuelova 2 >

1 I stalo se potom, že se David tázal Hospodina, řka: Mám-li jíti do některého města Judského? Jemuž odpověděl Hospodin: Jdi. I řekl David: Kam mám jíti? Odpověděl: Do Hebronu.
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 A protož bral se tam David, ano i obě manželky jeho, Achinoam Jezreelská, a Abigail žena někdy Nábale Karmelského.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 Muže také své, kteříž s ním byli, pojal David, jednoho každého s čeledí jeho, a bydlili v městech Hebronských.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 I přišli muži Judští, a pomazali tam Davida za krále nad domem Judským. Oznámili také Davidovi, řkouce: Muži Jábes Galád, oni pochovali Saule.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 Tedy poslav David posly k mužům Jábes Galád, řekl jim: Požehnaní jste vy před Hospodinem, že jste učinili to milosrdenství pánu svému Saulovi, pochovavše ho.
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Protož nyní učiniž s vámi Hospodin milosrdenství a pravdu; ano i jáť s vámi učiním milost, kteříž jste to učinili.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 A tak tedy posilňtež rukou svých a buďtež stateční; nebo ač umřel pán váš Saul, však již mne pomazali dům Judův za krále nad sebou.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 Abner pak syn Nerův, hejtman vojska Saulova, vzal Izbozeta syna Saulova a uvedl ho do Mahanaim.
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 A ustavil ho králem nad Galád a nad Assur, a nad Jezreel, a nad Efraimem, a nad Beniaminem, i nade vším Izraelem.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Ve čtyřidcíti letech byl Izbozet syn Saulův, když počal kralovati nad Izraelem, a kraloval dvě létě. (Toliko dům Judův přídržel se Davida.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 A byl počet dnů, v nichž byl David králem v Hebronu nad domem Judovým, sedm let a šest měsíců.)
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Potom vytáhl Abner syn Nerův, a služebníci Izbozeta syna Saulova z Mahanaim do Gabaon.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 Joáb také syn Sarvie a služebníci Davidovi vytáhše, potkali se s nimi právě u rybníka Gabaon. I pozůstali tito u rybníka s strany jedné, oni pak u rybníka s druhé strany.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Tedy řekl Abner Joábovi: Nechť vystoupí nyní mládenci a pohrají před námi. I řekl Joáb: Nechť vystoupí.
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 A tak vystoupili a vyšli v rovném počtu, dvanácte z Beniamina, z strany Izbozeta syna Saulova, a dvanácte z služebníků Davidových.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Kteřížto ujavše jeden každý za hlavu bližního svého, vrazil meč svůj v bok tovaryše svého, i padli spolu. Protož nazváno jest místo to Helkat Hassurim, a jest v Gabaon.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 I byla bitva velmi veliká v ten den, a poražen jest Abner i muži Izraelští od služebníků Davidových.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 Byli tu také tři synové Sarvie: Joáb, Abizai a Azael. Azael pak byl čerstvý na nohy své jako srna v poli.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 I honil Azael Abnera, a neuhnul se na pravo ani na levo, běže za Abnerem.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 Ohlédl se pak Abner zpátkem a řekl: Ty-li jsi Azael? Odpověděl: Jsem.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Tedy řekl mu Abner: Uchyl se na pravo aneb na levo, a jmi sobě jednoho z mládenců těch, a vezmi sobě kořisti jeho. Ale nechtěl Azael uchýliti se od něho.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 Ještě znovu Abner řekl Azaelovi: Uchyl se ode mne, sic jináč přirazím tě až k zemi, a jak bych směl pohleděti na Joába bratra tvého?
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 Když pak nechtěl ustoupiti, uhodil ho Abner kopím pod páté žebro, tak že vyniklo kopí hřbetem jeho; a padl tu na tom místě, na kterémž i umřel. A kdožkoli přicházeli k místu, na němž padl Azael a umřel, zastavovali se.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Ale Joáb a Abizai honili Abnera. Slunce pak již bylo zapadlo, když oni přišli ku pahrbku Amma, jenž jest naproti Giach, cestou k poušti Gabaon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 Tedy sešli se synové Beniamin za Abnerem, a jsouce spolu v houfu, postavili se na vrchu pahrbku jednoho.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Odkudž zavolal Abner na Joába, řka: Zdaliž bez přestání sžírati bude meč tvůj? Nevíš-liž, že hořkost bývá naposledy? Dokudž tedy nerozkážeš lidu navrátiti se od honění bratří svých?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 I řekl Joáb: Živť jest Bůh, že kdybys byl nemluvil, hned ráno byl by odšel lid, jeden každý nechaje honění bratra svého.
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 Tedy zatroubil Joáb v troubu, a zastavil se všecken lid, a nehonili více Izraele, aniž více bojovali.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 A tak Abner i lid jeho šli přes pole celou tu noc, a přepravili se přes Jordán, a prošedše všecku Betoron, přišli do Mahanaim.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Ale Joáb navrátiv se od honění Abnera, shromáždil všecken lid, a nedostávalo se z služebníků Davidových devatenácti mužů a Azaele.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 Služebníci pak Davidovi zbili z Beniaminských a z mužů Abnerových tři sta a šedesáte mužů, kteříž tu zahynuli.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 A vzavše Azaele, pohřbili jej v hrobě otce jeho, kterýž byl v Betlémě. Potom šli celou tu noc Joáb a muži jeho; i rozednilo se, když přicházeli do Hebronu.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.

< 2 Samuelova 2 >