< 2 Samuelova 13 >
1 I stalo se potom, že Absolon syn Davidův měl sestru krásnou, jménem Támar; i zamiloval ji Amnon syn Davidův.
Ikawa baada ya hayo, Amnoni mwana wa Daudi akampenda Tamari, umbu lake Absalomu mwana wa Daudi, ambaye alikuwa mzuri wa sura.
2 A tak se o to trápil Amnon, že i v nemoc upadl pro Támar sestru svou; nebo panna byla, a viděl Amnon, že nesnadně bude jí moci co učiniti.
Amnoni akasumbuka sana kuhusu Tamari hata akaugua, kwa kuwa Tamari alikuwa bikira, na ilionekana kwamba haiwezekani Amnoni kumfanyia jambo lolote.
3 Měl pak Amnon přítele, jehož jméno bylo Jonadab, syn Semmaa bratra Davidova, kterýžto Jonadab byl muž velmi chytrý.
Basi Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi. Yonadabu alikuwa mtu wa hila nyingi sana.
4 I řekl jemu: Proč tak chřadneš, synu králův, den ode dne? Neoznámíš-liž mi? I řekl mu Amnon: Támar sestru Absolona bratra svého miluji.
Akamuuliza Amnoni, “Wewe ni mtoto wa mfalme; kwa nini siku baada ya siku unaonekana kukonda? Hutaniambia?” Amnoni akamwambia, “Ninampenda Tamari, dada yake Absalomu ndugu yangu.”
5 Tedy řekl jemu Jonadab: Polož se na lůže své a udělej se nemocným, a když přijde otec tvůj, aby tě navštívil, díš jemu: Nechť přijde, prosím, Támar sestra má a dá mi jísti, připravíc před očima mýma pokrm, abych viděl a jedl z ruky její.
Yonadabu akamwambia, “Nenda ukalale kitandani na ujifanye kuwa mgonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona mwambie, ‘Ningependa Tamari dada yangu aje kunipatia chochote ili nile. Tafadhali mruhusu aje na kuniandalia chakula mbele yangu ningali ninamwona, ili nipate kula kutoka mkononi mwake.’”
6 A tak složil se Amnon, dělaje se nemocným. A když přišel král, aby ho navštívil, řekl Amnon králi: Nechť přijde, prosím, Támar sestra má a připraví před očima mýma asi dvě krmičky, abych pojedl z ruky její.
Kwa hiyo Amnoni akalala kitandani kujifanya mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia, “Ningependa dada yangu Tamari aje na kuniandalia mikate maalum mbele yangu, ili nipate kula toka mkononi mwake.”
7 Protož poslal David k Támar do domu, řka: Jdi hned do domu Amnona bratra svého a připrav mu krmičku.
Daudi akampelekea Tamari ujumbe huko kwenye jumba la kifalme, kusema: “Nenda katika nyumba ya ndugu yako Amnoni ukamwandalie chakula.”
8 I šla Támar do domu Amnona bratra svého; on pak ležel. A vzavši mouky, zadělala ji, a připravivši krmičku před očima jeho, uvařila ji.
Kwa hiyo Tamari akaenda nyumbani kwa nduguye Amnoni, ndugu ambaye alikuwa amelala. Tamari akachukua unga uliotiwa chachu akaukanda, akaiandaa mikate mbele yake na kuioka.
9 Potom vzavši pánvici, vyložila před něj, a on nechtěl jísti. (I řekl Amnon: Spravte to, ať vyjdou všickni ven. I vyšli od něho všickni.
Tamari akaondoa mikate kwenye kikaango ili ampatie Amnoni, lakini akakataa kula. Amnoni akamwambia, “Mtoe nje kila mtu aliyeko hapa.” Kwa hiyo kila mmoja akaondoka.
10 Řekl pak Amnon k Támar: Přines tu krmičku do pokojíka, abych pojedl z ruky tvé. A vzavši Támar krmičku, kterouž připravila, přinesla ji před Amnona bratra svého do pokojíka.)
Ndipo Amnoni akamwambia Tamari, “Leta mkate hapa ndani ya chumba changu ili nipate kula kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua mikate aliyoiandaa na kumletea Amnoni ndugu yake ndani ya chumba chake.
11 Ale když mu podávala, aby jedl, uchopil ji a řekl jí: Poď, lež se mnou, sestro má.
Lakini alipompelekea ili ale, akamkamata kwa nguvu na kumwambia, “Njoo ulale nami, dada yangu.”
12 Kterážto řekla jemu: Nikoli, bratře můj, nečiň mi násilí, nebo ne tak se má díti v Izraeli. Neprovoď nešlechetnosti této.
Akamwambia, “Usifanye hivyo, ndugu yangu! Usinitende jeuri! Jambo la namna hii halistahili kufanyika katika Israeli! Usitende jambo hili ovu.
13 Nebo já na koho svedu pohanění své? Ty pak budeš jako jeden z nejnešlechetnějších v Izraeli. Raději tedy mluv medle s králem, nebo neodepřeť mne tobě.
Kwa upande wangu je, itakuwaje? Nitaipeleka wapi aibu yangu? Pia kwa upande wako, itakuwaje? Utakuwa kama mmoja wa wapumbavu waovu katika Israeli. Tafadhali zungumza na mfalme; hatakukatalia wewe kunioa,”
14 Ale nechtěl uposlechnouti hlasu jejího, nýbrž zmocniv se jí, učinil jí násilí a ležel s ní.
Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza, na kwa kuwa alikuwa na nguvu kuliko Tamari, akamtenda jeuri.
15 Potom vzal ji Amnon v nenávist velikou velmi, tak že větší byla nenávist, kterouž nenáviděl jí, než milost, kterouž ji miloval. I řekl jí Amnon: Vstaň a jdi pryč.
Kisha Amnoni akamchukia Tamari, kwa machukio makuu sana. Kwa kweli, Amnoni alimchukia kuliko alivyokuwa amempenda. Amnoni akamwambia, “Inuka na utoke nje!”
16 Kterážto odpověděla jemu: Za příčinou převelmi zlé věci té, kterouž jsi při mně spáchal, druhé horší se dopouštíš, že mne vyháníš. On pak nechtěl jí slyšeti.
Tamari akamwambia, “Hapana! Kunifukuza itakuwa vibaya zaidi kuliko yale uliyonitendea.” Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza.
17 Ale zavolav mládence, kterýž mu přisluhoval, řekl: Vyveď hned tuto ode mne ven, a zamkni dvéře po ní.
Akamwita mtumishi wake mahsusi na kumwambia, “Mtoe huyu mwanamke hapa na ufunge mlango nyuma yake.”
18 (Měla pak na sobě sukni proměnných barev, nebo v takových sukních chodívaly dcery královské panny.) A tak vyvedl ji ven služebník jeho a zamkl dvéře po ní.
Kwa hiyo, mtumishi wake akamtoa nje na kufunga mlango nyuma yake. Tamari alikuwa amevaa joho lililopambwa vizuri, kwa maana lilikuwa aina ya mavazi yaliyovaliwa na binti za mfalme waliokuwa mabikira.
19 Tedy posypala Támar hlavu svou popelem, a sukni proměnných barev, kterouž měla na sobě, roztrhla; a vložila ruku na hlavu svou, a jduc, křičela s naříkáním.
Tamari akajitia majivu kichwani mwake na kurarua lile joho alilokuwa amevaa. Akaweka mkono wake kichwani, akaenda zake akilia kwa sauti.
20 I řekl jí Absolon bratr její: Nebyl-liž Amnon bratr tvůj s tebou? Ale nyní, sestro má mlč; bratr tvůj jest, nepřipouštěj toho k srdci. A tak zůstala Támar, jsuc opuštěná, v domě Absolona bratra svého.
Absalomu nduguye akamuuliza, “Je, huyo Amnoni ndugu yako, amekutana nawe kimwili? Sasa nyamaza umbu langu, yeye ni ndugu yako. Usilitie jambo hili moyoni.” Naye Tamari akaishi nyumbani kwa Absalomu nduguye, akiwa mwanamke mwenye huzuni.
21 A uslyšev král David o těch všech věcech, rozhněval se náramně.
Mfalme Daudi aliposikia mambo haya yote, akakasirika sana.
22 Absolon pak nic nemluvil s Amnonem, ani dobrého ani zlého; nebo nenáviděl Absolon Amnona, proto že učinil násilí Támar sestře jeho.
Absalomu hakusema neno lolote na Amnoni, likiwa zuri au baya, kwa kuwa alimchukia Amnoni kwa sababu alikuwa amemtia aibu Tamari, dada yake.
23 I stalo se po celých dvou letech, když střihli ovce Absolonovi v Balazor, jenž jest podlé Efraim, že pozval Absolon všech synů královských.
Miaka miwili baadaye, wakati wakata manyoya ya kondoo wa Absalomu walipokuwa huko Baal-Hasori karibu na mpaka wa Efraimu, alialika wana wote wa mfalme kuja huko.
24 Nebo přišel Absolon k králi a řekl: Aj, nyní služebník tvůj má střižce; nechť, prosím, jde král a služebníci jeho s služebníkem tvým.
Absalomu akaenda kwa mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako ninao wakata manyoya ya kondoo waliokuja. Tafadhali, je, mfalme na maafisa wake wanaweza kuungana nami?”
25 I řekl král Absolonovi: Nechť, synu můj, nechť nyní nechodíme všickni, abychom tě neobtěžovali. A ačkoli nutkal ho, však nechtěl jíti, ale požehnal mu.
Mfalme akajibu, “La hasha, mwanangu si lazima sisi sote tuje, tutakuwa tu mzigo kwako.” Ingawa Absalomu alimsihi sana, mfalme alikataa kwenda, lakini alimbariki.
26 Řekl ještě Absolon: Nechť aspoň s námi jde, prosím, Amnon bratr můj. Odpověděl jemu král: Proč by s tebou šel?
Basi Absalomu akasema, “Kama hutakuja, tafadhali mruhusu ndugu yangu Amnoni twende pamoja naye.” Mfalme akamuuliza, “Kwa nini aende pamoja nawe?”
27 A když vždy dotíral Absolon, poslal s ním Amnona i všecky syny královské.
Lakini Absalomu alimsihi, kwa hiyo mfalme akamtuma Amnoni pamoja na wana wengine wa mfalme waliobaki.
28 Přikázal pak byl Absolon služebníkům svým, řka: Šetřte medle, když se rozveselí srdce Amnonovo vínem, a řeknu vám: Bíte Amnona, tedy zabíte jej. Nebojte se nic, nebo zdaliž jsem já nerozkázal vám? Posilňte se a mějte se zmužile.
Absalomu aliagiza watu wake, “Sikilizeni! Wakati Amnoni atakapokuwa amekunywa mvinyo na kulewa sana nami nikiwaambia, ‘Mpigeni Amnoni,’ basi muueni. Msiogope. Je, si mimi niliyewapa amri hii? Kuweni hodari na wenye ushujaa.”
29 I učinili Amnonovi služebníci Absolonovi, jakž jim byl přikázal Absolon. Pročež vstavše všickni synové královi, vsedli jeden každý na mezka svého a utekli.
Kwa hiyo watu wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa amewaagiza. Ndipo wana wote wa mfalme wakainuka, wakapanda nyumbu zao, wakakimbia.
30 V tom když ještě byli na cestě, přišla taková pověst k Davidovi: Pobil Absolon všecky syny královské, tak že z nich ani jednoho nezůstalo.
Wakati wakiwa njiani, taarifa ilimjia Daudi, kusema: “Absalomu amewaua wana wote wa mfalme; hakuna hata mmoja aliyesalia.”
31 Tedy vstav král, roztrhl roucha svá a ležel na zemi; všickni také služebníci jeho stáli, roztrhše roucha.
Mfalme akasimama, akararua nguo zake, akalala chini ardhini; nao watumishi wake wote wakasimama kando yake na nguo zao zikiwa zimeraruliwa.
32 Ozval se pak Jonadab, syn Semmaa bratra Davidova, a řekl: Nepraviž toho, pane můj, jako by všecky mládence syny královy zbili, ale Amnon toliko zabit; nebo tak v úmysle Absolonově složeno bylo od toho dne, jakž on byl učinil násilí Támar sestře jeho.
Lakini Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akasema, “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme; ni Amnoni peke yake ndiye alikufa. Hili limekuwa kusudi la moyo wa Absalomu tangu siku ile Amnoni alipomtendea jeuri Tamari, dada yake.
33 Protož nechať nepřipouští toho nyní pán můj král k srdci svému, mysle, že by všickni synové královi zbiti byli; nebo Amnon toliko umřel.
Mfalme bwana wangu asisumbuliwe na taarifa kwamba wamewaua wana wote wa mfalme. Ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
34 Absolon pak utekl. Tedy pozdvih služebník hlásný očí svých, uzřel, an mnoho lidu jde odtud, kudyž se chodilo k němu cestou pod horami.
Wakati huo, Absalomu akawa amekimbia. Basi mlinzi akaangalia, naye akaona watu wengi barabarani magharibi yake, wakishuka kutoka upande wa kilima. Mlinzi akaenda akamwambia mfalme, “Naona watu wakitokea upande wa Horonaimu, huko upande wa kilimani.”
35 I řekl Jonadab králi: Aj, synové královští přijíždějí. Vedlé řeči služebníka tvého tak se stalo.
Yonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wako hapa; imekuwa kama vile mtumishi wako alivyosema.”
36 A když přestal mluviti, aj, synové královští přišli, a pozdvihše hlasu svého, plakali; též také král i všickni služebníci jeho plakali pláčem velmi velikým.
Mara alipomaliza kusema, wana wa mfalme wakaingia ndani wakiomboleza kwa makelele. Pia mfalme na watumishi wake wote wakalia sana kwa uchungu.
37 Absolon pak utekl a ušel k Tolmai synu Amiudovu, králi Gessur. I plakal David syna svého po všecky ty dny.
Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Lakini Mfalme Daudi akaomboleza kwa ajili ya mwanawe kila siku.
38 Absolon tedy utíkaje, přišel do Gessur, a byl tam tři léta.
Baada ya Absalomu kukimbia na kwenda Geshuri, akakaa huko miaka mitatu.
39 Potom žádal David vyjíti k Absolonovi, nebo již byl oželel smrti Amnonovy.
Roho ya Mfalme Daudi ikatamani kumwendea Absalomu, kwa maana mfalme alikuwa amefarijika kuhusu kifo cha Amnoni.