< 2 Královská 8 >
1 Mluvil pak Elizeus k ženě té, jejíhož byl syna vzkřísil, řka: Vstaň a jdi, ty i čeled tvá, a buď pohostinu, kdežkoli budeš moci byt míti; nebo zavolal Hospodin hladu, a přijdeť na zemi za sedm let.
Basi, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye alimfufulia mtoto wake. Akamwambia, “Inuka na uenede pamoja na nyumba yako, na uishi popote uwezapo katika nchi nyingine, kwa sababu Yahwe ameiita njaa ambayo itakuja katika hii nchi kwa miaka saba.”
2 Vstavši tedy žena, učinila vedlé řeči muže Božího, a odešla s čeledí svou, a bydlila pohostinu v zemi Filistinských sedm let.
Basi yule mwanamke akainuka na akatii lile neno la mtumishi wa Mungu. Akaenda na nyumba yake na kuishi kwenye nchi ya Wafilisti miaka saba.
3 I stalo se, že když pominulo těch sedm let, navrátila se ta žena z země Filistinské, a šla, aby prosila krále za dům svůj a za pole své.
Ikafika kama mwishoni mwa miaka saba yule mwanamke akarudi kutoka kwenye ile nchi ya Wafilisti, na kwenda kwa mfalme kumuomba nyumba yake na kwa ajili ya nchi yake.
4 Mezi tím král mluvil s Gézi, služebníkem muže Božího, řka: Vypravuj mi medle o všech věcech velikých, kteréž činil Elizeus.
Basi mfalme alikuwa anaongea na Gehazi yule mtumishi wa Mungu, akisema, “Tafadhali niambie yale mambo makubwa ambayo Elisha ameyafanya.”
5 A když on vypravoval králi, kterak obživil mrtvého, aj žena, jejíhož syna vzkřísil, prosila krále za dům svůj a za pole své. I řekl Gézi: Pane můj králi, to jest ta žena, a tento syn její, kteréhož vzkřísil Elizeus.
Basi alipokuwa akimwambia yule mfalme jinsi gani Elisha alivyomfufua yule mtoto aliyekufa, huyo mwanamke ambaye mtoto wake aliyekuwa amefufuliwa akaja kumuomba yule mfalme kwa ajili ya nyumba yake na nchi yake. Gehazi akasema, “Bwana wangu, mfalme, huyu ndiye yule mwanamke, na huyu ndiye mtoto wake, ambaye Elisha amemfufua.”
6 Tedy tázal se král ženy, kteráž vypravovala jemu. I poručil král komorníku jednomu, řka: Ať jsou navráceny všecky věci, kteréž byly její, i všecky užitky pole, ode dne, v němž opustila zemi, až po dnes.
Wakati yule mfalme alipomuuliza yule mwanamke kuhusu mtoto wake, alimwelezea yule mfalme. Ndipo mfalme akamwagizia ofisa makini, akisema, “Mrudishie vyote vilivyokuwa vyake na mavuno yake yote ya kwenye mashamba tangu siku alipoondoka hadi sasa.”
7 Potom přišel Elizeus do Damašku, král pak Syrský Benadad stonal. I oznámeno jemu těmito slovy: Přišel muž Boží sem.
Elisha akaja Damaskasi ambako Ben Hadadi yule mfalme wa Shamu alikuwa anaumwa. Yule mfalme aliambiwa, “Yule mtu wa Mungu amekuja hapa.”
8 I řekl král Hazaelovi: Vezmi v ruce své dar, a jdi vstříc muži Božímu, a zeptej se Hospodina skrze něho, řka: Povstanu-li z nemoci této?
Mfalme akamwambia Hazaeli, “Chukua zawadi kwenye mkono wako na uende ukakutane na mtu wa Mungu, na ukazungumze na Yahwe kupitia yeye, ukisema, “Je nitapona huu ugonjwa wangu?”
9 A tak šel Hazael vstříc jemu, vzav s sebou dar, a všeliké věci výborné Damašské, břemena na čtyřidcíti velbloudích, a přišed, stál před ním a řekl: Syn tvůj Benadad, král Syrský, poslal mne k tobě, řka: Povstanu-li z nemoci této?
Basi Hazaeli akaenda kuonana naye na kuchukua zawadi zake za kila kitu kizuri cha Damskasi, akabeba ngamia arobaini. Hivyo Hazaeli akaja na kusimama mbele ya Elisha na kusema, “Mtoto wako Ben Hadadi mfalme wa Shamu amenituma kwako, kusema, “Je nitapona huu ugonjwa?”
10 Odpověděl mu Elizeus: Jdi, pověz jemu: Zajisté mohl bys živ zůstati. Ale Hospodin mi ukázal, že jistotně umře.
Elisha akamwambia, “Nenda, kwa Ben Hadadi, 'Utapona hakika,' lakini Yahwe amenionyesha kwamba atakufa hahkika.”
11 V tom proměniv muž Boží tvář svou, ukázal se k němu neochotně a plakal.
Basi Elisha akamtumbulia macho Hazaeli hadi alipojisikia aibu, na yule mtu wa Mungu akalia machozi.
12 Jemuž řekl Hazael: Proč pán můj pláče? Odpověděl: Proto že vím, co zlého ty učiníš synům Izraelským. Pevnosti jejich spálíš a mládence jejich zmorduješ mečem, a nemluvňátka jejich rozrážeti budeš, a těhotné jejich zroztínáš.
Hazaeli akauliza, kwa nini unalia, bwana wangu?” Akajibu, “Kwa sababu najua uovu ambao utakaoufanya kwa watu wa Israeli. Utazichoma moto ngome zao kwa moto, na utawaua vijana wao kwa upanga, kuwaseta vipande vipande watoto wao wachanga, na kuwapasua mimba zao wanawake wenye mimba.”
13 I řekl Hazael: I což jest služebník tvůj pes, aby učiniti mohl věc tak velikou? Odpověděl Elizeus: Ukázal tě mi Hospodin, že budeš králem Syrským.
Hazaeli akajibu, Ni nani mtumwa wako, ambaye atafanya jambo hili kubwa? Yeye ni mbwa tu.” Elisha akajibu, “Yahwe amenionyesha kwamba utakuwa mfalme juu ya Shamu.”
14 A odšed od Elizea, přišel ku pánu svému. Kterýž řekl jemu: Cožť řekl Elizeus? Odpověděl: Pravil mi, že bys mohl živ zůstati.
Ndipo Hazaeli akamwacha Elisha na kuja kwa bwana wake, ambaye alimwambia, “Je Elisha alikwambiaje?” Akajibu, “Ameniambia kwamba utapona bila shaka.”
15 I stalo se nazejtří, že vzal koberec, a namočiv jej v vodě, prostřel jej na tvář jeho. I umřel, a kraloval Hazael místo něho.
Basi siku ya pili yake Hazaeli akachukua blangeti na kulichovya kwenye maji, na kulitandaza kwenye uso wa Ben Hadadi hivyo akafa. Basi Hazaeli akawa mfalme katika sehemu sehemu yake.
16 Léta pak pátého Jorama, syna Achabova krále Izraelského, a Jozafata krále Judského, počal kralovati Jehoram, syn Jozafatův král Judský.
Katika mwaka wa kumi na tano wa Yoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Yehoramu akaanza kutawala. Alikuwa mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda. Alianza wakati Yehoshafati alikuwa mfalme wa Yuda.
17 Ve dvou a třidcíti letech byl, když počal kralovati, a kraloval osm let v Jeruzalémě.
Yoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na mbili alipoanza kutawala, na alitawala kwa mda wa miaka minane katika Yerusalemu.
18 A chodil po cestě králů Izraelských, tak jako činil dům Achabův; nebo měl dceru Achabovu za manželku. Takž činil zlé věci před očima Hospodinovýma.
Yoramu akatembea kwenye njia ya huyo mfalme wa Israeli, kama walivyokuwa wakifanya kwenye nyumba ya Ahabu; kwa kuwa alikuwa na binti wa Ahabu kama mke wake, na alifanya uovu usoni kwa Yahwe.
19 Hospodin však nechtěl zahladiti Judy pro Davida služebníka svého, jakž mu byl zaslíbil, že dá jemu svíci i synům jeho po všecky dny.
Walakini, kwa sababu ya mtumishi wake Daudi, Yahwe hakutaka kuiharibu Yuda, tangu alipomwambia kwamba atampatia wazao.
20 Ve dnech jeho odstoupil Edom od království Judského, a ustanovili nad sebou krále.
Katika siku za Yoramu, Edomu akaasi kutoka chini ya mkono wa Yuda, na wakamfanya mfalme juu yao wenyewe.
21 Tou příčinou táhl Jehoram do Seir, i všickni vozové s ním. A vstav v noci, porazil Idumejské, kteříž jej byli obklíčili, i hejtmany vozů, a lid utekl do stanů svých.
Basi Yehoramu akaenda na maamri jeshi na magari ya farasi yote. Ilitokea kwamba akaamka usiku na kushambulia na kuwazunguka Waedomu, waliokuwa wamemzunguka na wale maamri jeshi wa magari ya farasi. Ndipo wanajeshi wa Yehoramu wakakimbilia wajumbani kwao.
22 Však předce odstoupil Edom od království Judského až do tohoto dne. Takž odstoupilo i Lebno téhož času.
Hivyo Edomu aliasi dhidi ya utawala wa Yuda katika siku hizi. Libna pia aliasi katika kipindi hicho hicho.
23 O jiných pak věcech Jehoramových, a o všem, cožkoli činil, psáno jest v knize o králích Judských.
Kwa mambo mengine yamhusuyo Yehoramu, yote aliyoyafanya, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Yuda?
24 I usnul Jehoram s otci svými, a pochován jest s otci svými v městě Davidově, kraloval pak Ochoziáš syn jeho místo něho.
Yehoramu akafa na kuzikwa pamoja na baba zake, na akalala pamoja na baba zake katika mji wa Daudi. Ndipo Ahazi mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.
25 Léta dvanáctého Jorama syna Achabova, krále Izraelského, počal kralovati Ochoziáš syn Jehorama, krále Judského.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa Yohoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.
26 Ve dvamecítma letech byl Ochoziáš, když počal kralovati, a kraloval jeden rok v Jeruzalémě. Jméno matky jeho bylo Atalia, dcera Amri krále Izraelského.
Ahazi alikuwa ana umri wa miaka ishirini na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala kwa mda wa mwaka mmoja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Athalia; alikuwa mtoto wa Omri, mfalme wa Israeli.
27 A chodil cestou domu Achabova, čině, což jest zlého před očima Hospodinovýma, jako i dům Achabův, nebo byl zetěm domu Achabova.
Ahazia alitembelea katika nyumba ya Ahabu; alifanya yale yaliyo maovu katika uso wa Yahwe, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa ikifanya, kwa kuwa Ahazia alikuwa mkwe kwenye nyumba ya Aabu.
28 Pročež vycházel s Joramem synem Achabovým, na vojnu proti Hazaelovi králi Syrskému, do Rámot Galád; ale porazili Syrští Jorama.
Ahazia akaenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu, kupigana dhidi ya Hazaeli, mfalme wa Shamu, katika Ramath Geleadi. Washami wakamjeruhi Yoramu.
29 A tak navrátil se král Joram, aby se hojil v Jezreel na rány, kterýmiž ho ranili Syrští v Ráma, když bojoval s Hazaelem králem Syrským. Ochoziáš pak syn Jehorama, krále Judského, přijel, aby navštívil Jorama syna Achabova v Jezreel; nebo tam nemocen byl.
Mfalme Yoramu akarudi ili auguzwe huko Yezreeli kwenye yale majeraha ambayo Washami walimpatia huko Rama. Wakati alipopigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Hivyo Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme Yuda, akashuka kwa Yezreeli kumuona Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu Yoramu alikuwa amejeruhiwa.