< 2 Královská 8 >
1 Mluvil pak Elizeus k ženě té, jejíhož byl syna vzkřísil, řka: Vstaň a jdi, ty i čeled tvá, a buď pohostinu, kdežkoli budeš moci byt míti; nebo zavolal Hospodin hladu, a přijdeť na zemi za sedm let.
Wakati huu, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa, “Ondoka wewe na jamaa yako ukaishi mahali popote unapoweza kwa kitambo kidogo, kwa sababu Bwana ameamuru njaa katika nchi hii ambayo itadumu kwa miaka saba.”
2 Vstavši tedy žena, učinila vedlé řeči muže Božího, a odešla s čeledí svou, a bydlila pohostinu v zemi Filistinských sedm let.
Yule mwanamke akafanya kama vile yule mtu wa Mungu alivyosema. Yeye na jamaa yake wakaondoka na kwenda kuishi katika nchi ya Wafilisti kwa miaka saba.
3 I stalo se, že když pominulo těch sedm let, navrátila se ta žena z země Filistinské, a šla, aby prosila krále za dům svůj a za pole své.
Baada ya miaka saba, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti, akaenda kwa mfalme kumsihi kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.
4 Mezi tím král mluvil s Gézi, služebníkem muže Božího, řka: Vypravuj mi medle o všech věcech velikých, kteréž činil Elizeus.
Mfalme alikuwa anazungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, naye alikuwa amesema, “Hebu niambie mambo yote makuu yaliyofanywa na Elisha.”
5 A když on vypravoval králi, kterak obživil mrtvého, aj žena, jejíhož syna vzkřísil, prosila krále za dům svůj a za pole své. I řekl Gézi: Pane můj králi, to jest ta žena, a tento syn její, kteréhož vzkřísil Elizeus.
Wakati Gehazi alipokuwa akimweleza mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtu, yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa na Elisha akaja ili amsihi mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. Gehazi akasema, “Huyu ndiye huyo mwanamke, bwana wangu mfalme, na huyu ndiye mwanawe ambaye Elisha alimfufua.”
6 Tedy tázal se král ženy, kteráž vypravovala jemu. I poručil král komorníku jednomu, řka: Ať jsou navráceny všecky věci, kteréž byly její, i všecky užitky pole, ode dne, v němž opustila zemi, až po dnes.
Mfalme akamuuliza yule mwanamke kuhusu mambo hayo, naye akamweleza. Ndipo akaamuru afisa ashughulikie shauri lake na kumwambia, “Mrudishie huyu mwanamke kila kitu kilichokuwa mali yake, pamoja na mapato yote yaliyotokana na shamba lake tangu siku alipoondoka nchini hadi sasa.”
7 Potom přišel Elizeus do Damašku, král pak Syrský Benadad stonal. I oznámeno jemu těmito slovy: Přišel muž Boží sem.
Elisha akaenda Dameski, naye Ben-Hadadi mfalme wa Aramu alikuwa mgonjwa. Mfalme alipoambiwa, “Mtu wa Mungu ametoka mbali akapanda hadi hapa,”
8 I řekl král Hazaelovi: Vezmi v ruce své dar, a jdi vstříc muži Božímu, a zeptej se Hospodina skrze něho, řka: Povstanu-li z nemoci této?
mfalme akamwambia Hazaeli. “Chukua zawadi na uende kumlaki huyo mtu wa Mungu. Muulize Bwana kupitia yeye, kwamba, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
9 A tak šel Hazael vstříc jemu, vzav s sebou dar, a všeliké věci výborné Damašské, břemena na čtyřidcíti velbloudích, a přišed, stál před ním a řekl: Syn tvůj Benadad, král Syrský, poslal mne k tobě, řka: Povstanu-li z nemoci této?
Hazaeli akaenda kumlaki Elisha, akiwa amechukua zawadi ya kila kitu kizuri kilichopatikana Dameski, mizigo iliyobebwa na ngamia arobaini. Akaingia ndani na kusimama mbele yake, akasema, “Mwanao Ben-Hadadi mfalme wa Aramu amenituma niulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
10 Odpověděl mu Elizeus: Jdi, pověz jemu: Zajisté mohl bys živ zůstati. Ale Hospodin mi ukázal, že jistotně umře.
Elisha akajibu, “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona’; lakini Bwana amenifunulia kwamba kweli atakufa.”
11 V tom proměniv muž Boží tvář svou, ukázal se k němu neochotně a plakal.
Elisha akamkazia Hazaeli macho kwa nguvu mpaka akaona aibu. Kisha mtu wa Mungu akaanza kulia.
12 Jemuž řekl Hazael: Proč pán můj pláče? Odpověděl: Proto že vím, co zlého ty učiníš synům Izraelským. Pevnosti jejich spálíš a mládence jejich zmorduješ mečem, a nemluvňátka jejich rozrážeti budeš, a těhotné jejich zroztínáš.
Hazaeli akauliza “Kwa nini bwana wangu analia?” Elisha akajibu, “Kwa sababu najua mabaya utakayowatendea Waisraeli. Utachoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, kuwatupa chini kwa nguvu watoto wachanga, na kuwatumbua wanawake wenye mimba.”
13 I řekl Hazael: I což jest služebník tvůj pes, aby učiniti mohl věc tak velikou? Odpověděl Elizeus: Ukázal tě mi Hospodin, že budeš králem Syrským.
Hazaeli akasema, “Itawezekanaje mtumishi wako, aliye mbwa tu, kufanya tendo la ajabu namna hiyo?” Elisha akamjibu, “Bwana amenionyesha kuwa utakuwa mfalme wa Aramu.”
14 A odšed od Elizea, přišel ku pánu svému. Kterýž řekl jemu: Cožť řekl Elizeus? Odpověděl: Pravil mi, že bys mohl živ zůstati.
Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kumrudia bwana wake. Ben-Hadadi akamuuliza, “Elisha alikuambia nini?” Hazaeli akajibu, “Aliniambia kwamba hakika utapona.”
15 I stalo se nazejtří, že vzal koberec, a namočiv jej v vodě, prostřel jej na tvář jeho. I umřel, a kraloval Hazael místo něho.
Lakini kesho yake Hazaeli akachukua nguo nzito, akailoweka ndani ya maji, akaitandaza juu ya uso wa mfalme, hivyo akafa. Kisha Hazaeli akaingia mahali pake kuwa mfalme wa Aramu.
16 Léta pak pátého Jorama, syna Achabova krále Izraelského, a Jozafata krále Judského, počal kralovati Jehoram, syn Jozafatův král Judský.
Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, wakati huo Yehoshafati akiwa mfalme wa Yuda, Yehoramu mwana wa Yehoshafati akaanza kutawala kama mfalme wa Yuda.
17 Ve dvou a třidcíti letech byl, když počal kralovati, a kraloval osm let v Jeruzalémě.
Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
18 A chodil po cestě králů Izraelských, tak jako činil dům Achabův; nebo měl dceru Achabovu za manželku. Takž činil zlé věci před očima Hospodinovýma.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
19 Hospodin však nechtěl zahladiti Judy pro Davida služebníka svého, jakž mu byl zaslíbil, že dá jemu svíci i synům jeho po všecky dny.
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, Bwana hakutaka kuiangamiza Yuda. Alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili ya Daudi na wazao wake milele.
20 Ve dnech jeho odstoupil Edom od království Judského, a ustanovili nad sebou krále.
Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
21 Tou příčinou táhl Jehoram do Seir, i všickni vozové s ním. A vstav v noci, porazil Idumejské, kteříž jej byli obklíčili, i hejtmany vozů, a lid utekl do stanů svých.
Basi Yehoramu akaenda Sairi pamoja na magari yake yote ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu. Hata hivyo, jeshi lake likatorokea nyumbani mwao.
22 Však předce odstoupil Edom od království Judského až do tohoto dne. Takž odstoupilo i Lebno téhož času.
Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo.
23 O jiných pak věcech Jehoramových, a o všem, cožkoli činil, psáno jest v knize o králích Judských.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
24 I usnul Jehoram s otci svými, a pochován jest s otci svými v městě Davidově, kraloval pak Ochoziáš syn jeho místo něho.
Yehoramu akalala pamoja na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Léta dvanáctého Jorama syna Achabova, krále Izraelského, počal kralovati Ochoziáš syn Jehorama, krále Judského.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
26 Ve dvamecítma letech byl Ochoziáš, když počal kralovati, a kraloval jeden rok v Jeruzalémě. Jméno matky jeho bylo Atalia, dcera Amri krále Izraelského.
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri mfalme wa Israeli.
27 A chodil cestou domu Achabova, čině, což jest zlého před očima Hospodinovýma, jako i dům Achabův, nebo byl zetěm domu Achabova.
Akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, na kutenda maovu machoni pa Bwana, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alikuwa ameoa kutoka nyumba ya Ahabu.
28 Pročež vycházel s Joramem synem Achabovým, na vojnu proti Hazaelovi králi Syrskému, do Rámot Galád; ale porazili Syrští Jorama.
Ahazia akaenda vitani na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
29 A tak navrátil se král Joram, aby se hojil v Jezreel na rány, kterýmiž ho ranili Syrští v Ráma, když bojoval s Hazaelem králem Syrským. Ochoziáš pak syn Jehorama, krále Judského, přijel, aby navštívil Jorama syna Achabova v Jezreel; nebo tam nemocen byl.
Hivyo Mfalme Yoramu akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa na Waaramu huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.