< 2 Královská 25 >

1 Stalo se pak léta devátého kralování jeho, měsíce desátého, v desátý den téhož měsíce, že přitáhl Nabuchodonozor král Babylonský se vším vojskem svým k Jeruzalému, a položil se u něho, a vzdělali proti němu hradbu vůkol.
Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
2 A bylo město obleženo, až do jedenáctého léta krále Sedechiáše.
Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
3 V kterémžto, devátého dne čtvrtého měsíce, rozmohl se hlad v městě, a neměl chleba lid země.
Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
4 I protrženo jest město, a všickni muži bojovní utekli noci té skrze bránu mezi dvěma zdmi u zahrady královské; Kaldejští pak leželi okolo města. Ušel také král cestou pouště.
Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
5 I honilo vojsko Kaldejské krále, a postihli ho na rovinách Jerišských, a všecko vojsko jeho rozprchlo se od něho.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
6 A tak javše krále, přivedli jej k králi Babylonskému do Ribla, kdež učinili o něm soud.
naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa.
7 Syny pak Sedechiášovy zmordovali před očima jeho. Potom Sedechiáše oslepili, a svázavše ho řetězy ocelivými, zavedli jej do Babylona.
Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
8 Potom měsíce pátého, sedmý den téhož měsíce, léta devatenáctého kralování Nabuchodonozora krále Babylonského, přitáhl Nebuzardan hejtman nad žoldnéři, služebník krále Babylonského, do Jeruzaléma.
Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
9 A zapálil dům Hospodinův i dům královský, i všecky domy v Jeruzalémě, a tak všecky domy veliké vypálil.
Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
10 Zdi také Jeruzalémské vůkol pobořilo všecko vojsko Kaldejské, kteréž bylo s tím hejtmanem nad žoldnéři.
Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu.
11 Ostatek pak lidu, kterýž byl zůstal v městě, i poběhlce, kteříž se byli obrátili k králi Babylonskému, a jiný obecný lid, zavedl Nebuzardan hejtman nad žoldnéři.
Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
12 Toliko něco chaterného lidu země zanechal hejtman nad žoldnéři, aby byli vinaři a oráči.
Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
13 Nadto sloupy měděné, kteříž byli v domě Hospodinově, i podstavky, i moře měděné, kteréž bylo v domě Hospodinově, ztloukli Kaldejští, a měď z nich odvezli do Babylona.
Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli.
14 Též hrnce, lopaty a nástroje hudebné, a kadidlnice i všecky nádoby měděné, jimiž sloužili, pobrali.
Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
15 I nádoby k oharkům a kotlíky, a cokoli zlatého a stříbrného bylo, pobral hejtman nad žoldnéři,
Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
16 Sloupy dva, moře jedno a podstavky, jichž byl nadělal Šalomoun do domu Hospodinova. Nebylo váhy mědi všech těch nádob.
Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
17 Osmnácti loket byla výška sloupu jednoho, a makovice na něm měděná, kterážto makovice tří loket zvýší byla, a mřežování i jablka zrnatá na té makovici vůkol; všecko bylo měděné. Takovýž byl i druhý sloup s mřežováním.
Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.
18 Vzal také týž hejtman nad žoldnéři Saraiáše kněze předního, a Sofoniáše kněze nižšího, a tři strážné prahu.
Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
19 A z města vzal komorníka jednoho, kterýž byl hejtmanem nad muži bojovnými, a pět mužů z těch, jenž bývali při králi, kteříž nalezeni byli v městě, a předního spisovatele vojska, kterýž popisoval vojsko z lidu země, a šedesáte mužů z lidu země, kteříž se nalezli v městě.
Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
20 Zjímav tedy je Nebuzardan hejtman nad žoldnéři, přivedl je k králi Babylonskému do Ribla.
Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
21 I pobil je král Babylonský, a zmordoval je v Ribla, v zemi Emat, a tak zaveden jest Juda z země své.
Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
22 Lidu pak, kterýž zůstal v zemi Judské, jehož byl zanechal Nabuchodonozor král Babylonský, představil Godoliáše syna Achikama, syna Safanova.
Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda.
23 I uslyšeli všickni hejtmané vojska, oni i lid jejich, že postavil za správce král Babylonský Godoliáše, a přišli k Godoliášovi do Masfa, totiž Izmael syn Netaniášův, a Jochanan syn Kareachův, a Saraiáš syn Tanchumeta Netofatského, a Jazaniáš syn Machatův, oni i lid jejich.
Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
24 Tedy přisáhl jim Godoliáš i lidu jejich, a řekl jim: Nebojte se služby Kaldejských, zůstaňte v zemi, a služte králi Babylonskému, a dobře vám bude.
Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”
25 I stalo se měsíce sedmého, přišel Izmael syn Netaniáše, syna Elisamova, z semene královského, a deset mužů s ním. I zabili Godoliáše, a umřel; takž i Židy i Kaldejské, kteříž s ním byli v Masfa.
Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa.
26 Pročež zdvih se všecken lid, od malého až do velikého, i hejtmané vojsk, ušli do Egypta; nebo se báli Kaldejských.
Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.
27 Stalo se také léta třidcátého sedmého po zajetí Joachina krále Judského, dvanáctého měsíce, dvadcátého sedmého dne téhož měsíce, povýšil Evilmerodach král Babylonský toho léta, když počal kralovati, Joachina krále Judského, pustiv ho z žaláře.
Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili.
28 A mluvil s ním dobrotivě, i stolici jeho postavil nad stolice jiných králů, kteříž s ním byli v Babyloně.
Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
29 Změnil též roucho jeho, kteréž měl v žaláři. I jídal vždycky před ním po všecky dny života svého.
Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
30 Nebo vyměřený pokrm ustavičně dáván byl jemu od krále, a to na každý den po všecky dny života jeho.
Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.

< 2 Královská 25 >