< 2 Královská 10 >

1 Měl pak Achab sedmdesáte synů v Samaří. I napsal Jéhu list, a poslal jej do Samaří k knížatům Jezreelským, starším, a kteříž chovali syny Achabovy, s tímto poručením:
Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
2 Hned jakž vás dojde list tento, poněvadž u vás jsou synové pána vašeho, jsou i vozové u vás, i koni, i město hrazené a zbroj,
“Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
3 Vybeřte nejlepšího a nejzpůsobnějšího z synů pána svého, a posaďte na stolici otce jeho, a bojujte za dům pána svého.
mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
4 Kteříž bojíce se náramně, pravili: Aj, dva králové neostáli před ním, a kterak my ostojíme?
Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
5 A tak poslal ten, kterýž byl ustanoven nad domem, a kterýž ustanoven byl nad městem, i starší, a kteříž chovali syny Achabovy, k Jéhu, řkouce: Služebníci tvoji jsme, a všecko, což nám rozkážeš, učiníme. Neustanovíme žádného krále; což se tobě dobře líbí, učiň.
Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
6 I napsal k nim list po druhé, řka: Jste-li moji a hlasu mého posloucháte-li, vezmouce hlavy všech synů pána svého, přiďte ke mně zítra o tomto času do Jezreel. (Synů pak králových bylo sedmdesáte mužů u nejpřednějších v městě, kteříž chovali je.)
Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
7 Tedy stalo se, jakž jich došel list ten, že zjímali syny královské, a zbili sedmdesáte mužů, a vkladše hlavy jejich do košů, poslali je k němu do Jezreel.
Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
8 A přišed posel, oznámil jemu, řka: Přinesli hlavy synů královských. A on řekl: Sklaďte je na dvě hromady u vrat brány až do jitra.
Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
9 Potom ráno vyšed, postavil se a řekl všemu lidu: Spravedliví jste vy. Aj, já spuntoval jsem se proti pánu svému a zabil jsem jej; kdo by pobil tyto všecky?
Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
10 Věztež nyní, žeť nepochybilo nižádné slovo Hospodinovo, kteréž mluvil Hospodin proti domu Achabovu, ale vykonal Hospodin to, což byl mluvil skrze služebníka svého Eliáše.
Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
11 A tak pobil Jéhu všecky, kteříž pozůstali z domu Achabova v Jezreel, i všecky nejpřednější jeho, i známé jeho, i kněží jeho, tak že nezůstalo z nich žádného živého.
Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
12 Potom vstav, odebral se a jel do Samaří, a již byl v Betekedu pastýřů na cestě.
Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
13 I nalezl tam Jéhu bratří Ochoziáše, krále Judského, a řekl: Kdo jste vy? Odpověděli: Jsme bratří Ochoziášovi a jdeme, abychom pozdravili synů králových a synů královny.
Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
14 Tedy řekl: Zjímejte je živé. I zjímali je živé, a pobili je u čisterny v Betekedu, čtyřidceti a dva muže, a nezůstal z nich žádný.
Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
15 Potom bera se odtud, nalezl Jonadaba syna Rechabova, kterýž se s ním potkal, a pozdravil ho. I řekl jemu: Jest-liž srdce tvé přímé, jako jest srdce mé s srdcem tvým? Odpověděl Jonadab: Jest, arci jest. Řekl Jéhu: Podejž mi ruky své. I podal mu ruky své. A on kázal mu vsednouti k sobě na vůz,
Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
16 A řekl: Pojeď se mnou, a viz horlivost mou pro Hospodina. A tak vezli jej na voze jeho.
Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
17 Když pak přijel do Samaří, pobil všecky, kteříž byli pozůstali z domu Achabova v Samaří, a vyhladil jej vedlé řeči Hospodinovy, kterouž byl mluvil k Eliášovi.
Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
18 Zatím shromáždiv Jéhu všecken lid, řekl jim: Achab málo sloužil Bálovi, Jéhu bude mu více sloužiti.
Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
19 Protož nyní všecky proroky Bálovy, všecky služebníky jeho, a všecky kněží jeho svolejte ke mně, ať žádný tam nezůstává; nebo velikou obět budu obětovati Bálovi. Kdož by koli nebyl přítomen, nezůstane živ. Ale Jéhu činil to chytře, aby vyhladil ctitele Bálovy.
Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
20 Řekl také Jéhu: Zasvěťte svátek Bálovi. I prohlásili jej.
Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
21 Rozeslal zajisté Jéhu po vší zemi Izraelské. I sešli se všickni ctitelé Bálovi, tak že nezůstalo ani jednoho, ješto by nepřišel. A když vešli do domu Bálova, naplněn jest dům Bálův, od jednoho konce až do druhého.
Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
22 Tedy řekl tomu, kterýž vládl rouchem: Vynes roucha všechněm ctitelům Bálovým. I přinesl jim roucha.
Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
23 Potom všel i Jéhu a Jonadab syn Rechabův do domu Bálova, a řekl ctitelům Bálovým: Vyhledejte a vizte, ať není zde s vámi někdo z ctitelů Hospodinových, kromě samých ctitelů Bálových.
Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
24 A tak vešli, aby obětovali oběti a zápaly. Jéhu pak postavil sobě vně osmdesáte mužů, jimž byl řekl: Jestliže kdo uteče z lidí těch, kteréž já uvozuji vám v ruce vaše, život váš za život jeho.
Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
25 I stalo se, když kněz dokonal obětování zápalu, řekl Jéhu drabantům a hejtmanům: Vejdětež a zbíte je, ať žádný neuchází. Kteřížto pobili je ostrostí meče, a rozmetali těla jejich drabanti a hejtmané. Potom šli dále do každého města, kdež byl dům Bálův,
Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
26 A vymítajíce modly z domu Bálova, pálili je.
Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
27 Zkazili také modlu Bálovu, a zbořivše dům jeho, nadělali z něho záchodů až do dnešního dne.
Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
28 A tak vyplénil Jéhu Bále z lidu Izraelského.
Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
29 A však proto od hříchů Jeroboáma syna Nebatova, kterýž přivedl k hřešení Izraele, neodstoupil Jéhu, totiž od těch telat zlatých, kteráž byla v Bethel a v Dan.
Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
30 Tedy řekl Hospodin Jéhu: Poněvadž jsi snažně vykonal to, což dobrého jest před očima mýma, a všecky věci, kteréž jsem měl v srdci svém, učinil jsi domu Achabovu, synové tvoji až do čtvrtého pokolení seděti budou na stolici Izraelské.
Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
31 Ale Jéhu nebyl toho pilen, aby chodil v zákoně Hospodina, Boha Izraelského, celým srdcem svým, aniž odstoupil od hříchů Jeroboáma, kterýž byl uvedl v hříchy lid Izraelský.
Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
32 Za těch dnů počal Hospodin zmenšovati Izraele; nebo je porazil Hazael po všech končinách Izraelských,
Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
33 Od Jordánu, proti východu slunce, všecku zemi Galád, Gádovu a Rubenovu i Manassesovu, od Aroer, kteréž jest při potoku Arnon, tak Galád jako Bázan.
mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
34 O jiných věcech Jéhu, a cožkoli činil, i o vší síle jeho, sepsáno jest v knize o králích Izraelských.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
35 I usnul Jéhu s otci svými, a pochovali jej v Samaří, a kraloval Joachaz syn jeho místo něho.
Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
36 Dnů pak, v nichž kraloval Jéhu nad lidem Izraelským v Samaří, bylo let osmmecítma.
Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.

< 2 Královská 10 >