< 2 Kronická 22 >

1 Tedy ustanovili krále obyvatelé Jeruzalémští Ochoziáše, syna jeho nejmladšího, místo něho; nebo všecky starší byl pobil houf lotříků, kteříž přitáhli s Arabskými do ležení. A tak kraloval Ochoziáš syn Jehorama krále Judského.
Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
2 Ve čtyřidcíti a dvou letech byl Ochoziáš, když kralovati počal, a jediný rok kraloval v Jeruzalémě. Jméno pak matky jeho Atalia dcera Amri.
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
3 I on také chodil po cestách domu Achabova, nebo matka jeho nabádala jej k nepobožnosti.
Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
4 Protož činil zlé věci před očima Hospodinovýma, jako dům Achabův; ty on měl zajisté rádce po smrti otce svého, k zahynutí svému.
Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
5 Nebo radou jejich se spravoval, a táhl s Joramem synem Achabovým, králem Izraelským, na vojnu proti Hazaelovi králi Syrskému do Rámot Galád, kdežto ranili Syrští Jorama.
Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
6 Kterýž navrátil se, aby se hojil v Jezreel; nebo měl rány, kteréž mu učinili v Ráma, když bojoval s Hazaelem králem Syrským. V tom Azariáš syn Jehorama krále Judského sstoupil, aby navštívil Jorama syna Achabova v Jezreel, kterýž tam nemocen byl.
Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
7 Bylo pak to ku pádu od Boha Ochoziášovi, že přišel k Joramovi. Nebo jakž přišel, vyjel s Joramem proti Jéhu synu Namsi, kteréhož byl pomazal Hospodin, aby vyplénil dům Achabův.
Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
8 Tedy stalo se, když mstil Jéhu nad domem Achabovým, že našel knížata Judská, a syny bratří Ochoziášových, kteříž sloužili Ochoziášovi, i zmordoval je.
Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
9 Potom hledajíce i Ochoziáše, jali jej, an se pokrýval v Samaří, a přivedše ho k Jéhu, zabili jej a pochovali; nebo řekli: Synť jest Jozafatův, kterýž hledal Hospodina celým srdcem svým. A tak nebylo žádného více z domu Ochoziášova, kterýž by měl moc k obdržení království.
Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
10 Pročež Atalia matka Ochoziášova viduci, že umřel syn její, vstavši, pomordovala všecko símě královské domu Judského.
Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
11 Ale Jozabat dcera králova vzala Joasa syna Ochoziášova, a tajně ho uchvátivši z prostředku synů královských, kteříž mordováni byli, schovala jej s chůvou jeho v pokoji, kdež lůže byla. I skryla ho Jozabat dcera krále Jorama, manželka Joiady kněze, (nebo ona byla sestra Ochoziášova), před Atalií, aby ho nezamordovala.
Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
12 I byl s nimi v domě Božím, skryt jsa za šest let, v nichž Atalia kralovala v té zemi.
Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

< 2 Kronická 22 >