< Římanům 2 >
1 Protož nemůžeš se vymluviti, ó člověče, každý potupující. Nebo tím, že jiného potupuješ, sám sebe odsuzuješ, poněvadž totéž činíš, což tupíš.
Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
2 Vímeť zajisté, že soud Boží jest podlé pravdy proti těm, kteříž takové věci činí.
Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
3 Zdali se domníváš, ó člověče, kterýž soudíš ty, kdož takové věci činí, a sám totéž čině, že ty ujdeš soudu Božího?
Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
4 Čili bohatstvím dobrotivosti jeho a snášelivosti i dlouhočekání pohrdáš, nevěda, že dobrotivost Boží ku pokání tebe vede?
Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
5 Ale podlé tvrdosti své a srdce nekajícího shromažďuješ sám sobě hněv ke dni hněvu a zjevení spravedlivého soudu Božího.
Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
6 Kterýž odplatí jednomu každému podlé skutků jeho,
Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
7 Těm zajisté, kteříž trvajíce v dobrém skutku, slávy a cti a nesmrtelnosti hledají, životem věčným, (aiōnios )
Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
8 Těm pak, kteříž jsou svárliví, a pravdě nepovolují, ale povolují nepravosti, prchlivostí a hněvem,
Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
9 Trápením a úzkostí, každé duši člověka činícího zlé, i Žida předně, i Řeka.
Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
10 Ale sláva a čest a pokoj každému, kdo činí dobré, i Židu předně, i Řeku.
bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
11 Neboť není přijímání osob u Boha.
Kwa maana Mungu hana upendeleo.
12 Kteřížkoli zajisté bez zákona hřešili, bez zákona i zahynou; a kteřížkoli pod zákonem hřešili, skrze zákon odsouzeni budou.
Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
13 (Nebo ne ti, kteříž slyší zákon, spravedlivi jsou před Bohem, ale činitelé zákona spravedlivi budou.
Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
14 Nebo když pohané zákona nemajíce, od přirození činí to, což přikazuje zákon, takoví zákona nemajíce, sami sobě zákonem jsou,
(Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
15 Jako ti, kteříž ukazují dílo zákona napsané na srdcích svých, když jim to osvědčuje svědomí jejich i myšlení, kteráž se vespolek obviňují, aneb také vymlouvají.)
Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
16 V ten den, když souditi bude Bůh tajné věci lidské, podlé evangelium mého skrze Jezukrista.
Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
17 Aj, ty sloveš Žid, a zpoléháš na zákon, a chlubíš se Bohem,
Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
18 A znáš vůli jeho, a rozeznáváš, co sluší, naučen jsa z zákona,
kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
19 A za to máš, že jsi ty vůdcím slepých, světlem těch, kteříž jsou ve tmě,
kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
20 Ředitelem nemoudrých, učitelem nemluvňat, majícím formu umění a pravdy v zákoně.
mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
21 Kterakž tedy jiného uče, sám sebe neučíš? Vyhlašuje, že nemá kradeno býti, kradeš?
basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
22 Pravě: Nezcizoložíš, cizoložství pácháš? V ohavnosti maje modly, svatokrádeže se dopouštíš?
Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
23 Zákonem se chlubě, přestupováním zákona Bohu neúctu činíš?
Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
24 Nebo jméno Boží pro vás v porouhání jest mezi pohany, jakož psáno jest.
Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
25 Obřezáníť zajisté prospěje, budeš-li zákon plniti; pakli budeš přestupitelem zákona, obřezání tvé učiněno jest neobřezáním.
Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
26 A protož jestližeť by neobřízka ostříhala práv zákona, zdaliž nebude počtena neobřízka jejich za obřízku?
Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
27 A ti, kteříž jsou z přirození neobřízka, zachovávajíce zákon, zdaliž nepotupí tebe, kterýž pod literou a obřízkou přestupník jsi zákona?
Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
28 Nebo ne ten jest Žid, kterýž jest zjevně; aniž to jest obřezání, kteréž bývá zjevně na těle;
Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
29 Ale ten jest Žid, kterýž vnitř jest Židem, obřezání maje srdečné v duchu, a ne podlé litery; jehož chvála ne z lidí jest, ale z Boha.
Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.