< Žalmy 118 >
1 Oslavujte Hospodina, nebo jest dobrý, nebo na věky trvá milosrdenství jeho.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Rciž nyní, Izraeli, že na věky milosrdenství jeho.
Israeli na aseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
3 Rciž nyní, dome Aronův, že na věky milosrdenství jeho.
Nyumba ya Aroni na iseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
4 Rcetež nyní bojící se Hospodina, že na věky milosrdenství jeho.
Wote wamchao Bwana na waseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
5 V úzkosti vzýval jsem Hospodina, a vyslyšev, uprostrannil mi Hospodin.
Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6 Hospodin se mnou, nebudu se báti. Co mi může učiniti člověk?
Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7 Hospodin se mnou jest mezi pomocníky mými, pročež já podívám se těm, kteříž mne mají v nenávisti.
Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
8 Lépe jest doufati v Hospodina, než naději skládati v člověku.
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
9 Lépe jest doufati v Hospodina, nežli naději skládati v knížatech.
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
10 Všickni národové obklíčili mne, ale ve jménu Hospodinovu vyplénil jsem je.
Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
11 Mnohokrát obklíčili mne, ale ve jménu Hospodinovu vyplénil jsem je.
Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
12 Ssuli se na mne jako včely, však zhasli jako oheň z trní: nebo ve jménu Hospodinovu vyplénil jsem je.
Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
13 Velmi jsi ztuha na mne dotíral, abych padl, ale Hospodin spomohl mi.
Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
14 Síla má a písnička má jest Hospodin, on byl můj vysvoboditel.
Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
15 Hlas prokřikování a spasení v staních spravedlivých. Pravice Hospodinova dokázala síly,
Sauti za shangwe na ushindi zinavuma hemani mwa wenye haki: “Mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!
16 Pravice Hospodinova vyvýšila se, pravice Hospodinova dokázala síly.
Mkono wa kuume wa Bwana umeinuliwa juu, mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!”
17 Neumruť, ale živ budu, abych vypravoval skutky Hospodinovy.
Sitakufa, bali nitaishi, nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
18 Trestaltě mne přísně Hospodin, ale smrti mne nevydal.
Bwana ameniadhibu vikali, lakini hakuniacha nife.
19 Otevřetež mi brány spravedlnosti, a vejda do nich, oslavovati budu Hospodina.
Nifungulie malango ya haki, nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
20 Tať jest brána Hospodinova, kterouž spravedliví vcházejí.
Hili ni lango la Bwana ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
21 Tuť já tě oslavovati budu, nebo jsi mne vyslyšel, a byls můj vysvoboditel.
Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, umekuwa wokovu wangu.
22 Kámen, kterýž zavrhli stavitelé, učiněn jest v hlavu úhelní.
Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni.
23 Od Hospodina stalo se to, a jest divné před očima našima.
Bwana ametenda hili, nalo ni la kushangaza machoni petu.
24 Tentoť jest den, kterýž učinil Hospodin, a protož radujme se a veselme se v něm.
Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, tushangilie na kufurahi ndani yake.
25 Prosím, Hospodine, zachovávejž již; prosím, Hospodine, dávej již šťastný prospěch.
Ee Bwana, tuokoe, Ee Bwana, utujalie mafanikio.
26 Požehnaný, jenž se béře ve jménu Hospodinovu; dobrořečíme vám z domu Hospodinova.
Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
27 Bůh silný Hospodin, onť se zasvítil nám, važte beránky až k rohům oltáře.
Bwana ndiye Mungu, naye ametuangazia nuru yake. Mkiwa na matawi mkononi, unganeni kwenye maandamano ya sikukuu hadi kwenye pembe za madhabahu.
28 Bůh silný můj ty jsi, protož slaviti tě budu, Bože můj, vyvyšovati tě budu.
Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
29 Oslavujtež Hospodina, neboť jest dobrý, nebo na věky milosrdenství jeho.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.