< Matouš 9 >

1 A vstoupiv na lodí, přeplavil se, a přišel do města svého.
Yesu akaingia kwenye chombo, akavuka na kufika katika mji wa kwao.
2 A aj, přinesli mu šlakem poraženého, ležícího na loži. A viděv Ježíš víru jejich, dí šlakem poraženému: Doufej, synu, odpuštěniť jsou tobě hříchové tvoji.
Wakati huo huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelazwa kwenye mkeka. Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, jipe moyo mkuu. Dhambi zako zimesamehewa.”
3 A aj, někteří z zákonníků řekli sami v sobě: Tento se rouhá.
Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa sheria wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”
4 A viděv Ježíš myšlení jejich, řekl: Proč vy myslíte zlé věci v srdcích svých?
Lakini Yesu akiyafahamu mawazo yao, akawaambia, “Kwa nini mnawaza maovu mioyoni mwenu?
5 Nebo co jest snáze říci: Odpuštěniť jsou tobě hříchové, čili říci: Vstaň a choď?
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
6 Ale abyste věděli, žeť má moc Syn člověka na zemi odpouštěti hříchy, tehdy dí šlakem poraženému: Vstana, vezmi na sebe lože své, a jdi do domu svého.
Lakini, ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Ndipo akamwambia yule aliyepooza, “Inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
7 Tedy vstav, odšel do domu svého.
Yule mtu akasimama, akaenda nyumbani kwake.
8 A vidouce to zástupové, divili se a velebili Boha, kterýž dal takovou moc lidem.
Makutano walipoyaona haya, wakajawa na hofu ya Mungu, wakamtukuza Mungu ambaye alikuwa ametoa mamlaka kama haya kwa wanadamu.
9 A jda odtud Ježíš, uzřel člověka sedícího na cle, jménem Matouše. I dí mu: Poď za mnou. I vstav, šel za ním.
Yesu alipokuwa akienda kutoka huko, alimwona mtu mmoja jina lake Mathayo akiwa ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru. Yesu akamwambia, “Nifuate.” Mathayo akaondoka, akamfuata.
10 Stalo se pak, když seděl Ježíš za stolem v domě, a aj, mnozí celní a hříšníci přišedše, stolili s Ježíšem a s učedlníky jeho.
Yesu alipokuwa akila chakula ndani ya nyumba ya Mathayo, watoza ushuru wengi na “wenye dhambi” wakaja kula pamoja naye na wanafunzi wake.
11 A vidouce to farizeové, řekli učedlníkům jeho: Proč s celnými a hříšníky jí mistr váš?
Mafarisayo walipoona mambo haya, wakawauliza wanafunzi wake, “Kwa nini Mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
12 Ježíš pak uslyšev to, řekl jim: Nepotřebujíť zdraví lékaře, ale nemocní.
Lakini Yesu aliposikia hayo, akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, lakini wale walio wagonjwa ndio wanaohitaji tabibu.
13 Jdouce pak, učte se, co jest to: Milosrdenství chci a ne oběti. Nebo nepřišel jsem volati spravedlivých, ale hříšných ku pokání.
Nendeni mkajifunze maana ya maneno haya: ‘Nataka rehema, wala si dhabihu.’ Kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
14 Tehdy přistoupili k němu učedlníci Janovi, řkouce: Proč my a farizeové postíme se často, učedlníci pak tvoji se nepostí?
Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakaja na kumuuliza Yesu, “Imekuwaje kwamba sisi na Mafarisayo tunafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”
15 I řekl jim Ježíš: Zdaliž mohou synové ženichovi rmoutiti se, dokudž s nimi jest ženich? Ale přijdou dnové, když bude od nich odjat ženich, a tehdyť se budou postiti.
Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kuomboleza wakati angali pamoja nao? Wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.
16 Žádný zajisté nepřišívá záplaty sukna nového k rouchu vetchému; nebo ta záplata jeho odtrhla by díl od roucha, a větší by díra byla.
“Hakuna mtu anayeshonea kiraka kipya kwenye nguo iliyochakaa, kwa maana kile kiraka kitachanika kutoka kwenye hiyo nguo, nayo hiyo nguo itachanika zaidi.
17 Aniž lejí vína nového do nádob starých; sic jinak rozpuknou se sudové, a víno se vyleje, a sudové se zkazí. Ale víno nové lejí do nových nádob, a bývá obé zachováno.
Wala watu hawaweki divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama wakifanya hivyo, viriba vitapasuka nayo divai itamwagika, navyo viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya, na hivyo divai na viriba huwa salama.”
18 A když on to k nim mluvil, aj, kníže přistoupivši, klanělo se jemu, řkuc: Dcera má nyní umřela. Ale poď, vlož na ni ruku svou, a budeť živa.
Yesu alipokuwa akiwaambia mambo haya, mara akaingia kiongozi wa sinagogi akapiga magoti mbele yake, akamwambia, “Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini njoo uweke mkono wako juu yake, naye atakuwa hai.”
19 A vstav Ježíš, šel za ním, i učedlníci jeho.
Yesu akaondoka akafuatana naye, nao wanafunzi wake pia wakaandamana naye.
20 (A aj žena, kteráž nemocí svou trápena byla ode dvanácti let, přistoupivši po zadu, dotkla se podolka roucha jeho.
Wakati huo huo, mwanamke mmoja, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, akaja nyuma ya Yesu, akagusa upindo wa vazi lake,
21 Nebo řekla sama v sobě: Dotknu-li se jen toliko roucha jeho, uzdravena budu.
kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikigusa tu vazi lake, nitaponywa.”
22 Ježíš pak obrátiv se, a uzřev ji, řekl: Doufej, dcero, víra tvá tě uzdravila. I ozdravěla ta žena té chvíle.)
Yesu akageuka, naye alipomwona akamwambia, “Binti, jipe moyo mkuu, imani yako imekuponya.” Naye yule mwanamke akapona kuanzia saa ile ile.
23 Přišed pak Ježíš do domu knížete, a uzřev trubače i zástup hlučící,
Yesu alipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi na kuwaona waombolezaji wakipiga filimbi za maombolezo na watu wengi wakipiga kelele,
24 Řekl jim: Odejdětež; nebo neumřela děvečka, ale spí. I posmívali se jemu.
akawaambia, “Ondokeni! Kwa maana binti huyu hakufa, bali amelala.” Wakamcheka kwa dhihaka.
25 A když byl vyhnán zástup, všed tam, ujal ji za ruku její. I vstala ta děvečka.
Lakini watu walipokwisha kutolewa nje, akaingia mle ndani na kumshika yule binti mkono, naye akaamka.
26 A roznesla se pověst ta po vší té zemi.
Habari hizi zikaenea katika maeneo yale yote.
27 A když šel odtud Ježíš, šli za ním dva slepí, volajíce a řkouce: Smiluj se nad námi, Synu Davidův.
Yesu alipokuwa akiondoka mahali pale, vipofu wawili wakamfuata wakipiga kelele kwa nguvu na kusema, “Mwana wa Daudi, tuhurumie!”
28 A když všel do domu, přistoupili k němu ti slepí. I dí jim Ježíš: Věříte-li, že to mohu učiniti? Řekli jemu: Ovšem, Pane.
Alipoingia mle nyumbani wale vipofu wakamjia. Naye Yesu akawauliza, “Mnaamini kwamba ninaweza kufanya jambo hili?” Wakamjibu, “Ndiyo, Bwana.”
29 Tedy dotekl se očí jejich, řka: Podlé víry vaší staň se vám.
Ndipo Yesu akagusa macho yao na kusema, “Iwe kwenu sawasawa na imani yenu.”
30 I otevříny jsou oči jejich. Zapověděl jim pak tuze Ježíš, řka: Viztež, ať nižádný nezví.
Macho yao yakafunguka. Yesu akawaonya vikali, akisema, “Angalieni mtu yeyote asijue kuhusu jambo hili.”
31 Ale oni vyšedše, rozhlásali jej po vší té zemi.
Lakini wao wakaenda na kueneza habari zake katika eneo lile lote.
32 A když oni vycházeli, aj, přivedli mu člověka němého, majícího ďábelství.
Walipokuwa wanatoka, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu na ambaye hakuweza kuongea aliletwa kwa Yesu.
33 A když vyvrženo bylo ďábelství, mluvil němý. I divili se zástupové, řkouce: Že nikdy nic nebylo vídáno takového v Izraeli.
Yule pepo mchafu alipotolewa, yule mtu aliyekuwa bubu akaongea. Ule umati wa watu ukastaajabu na kusema, “Jambo kama hili kamwe halijapata kuonekana katika Israeli.”
34 Farizeové pak pravili: Mocí knížete ďábelského vymítá ďábly.
Lakini Mafarisayo wakasema, “Huyo anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa mkuu wa pepo wachafu.”
35 I obcházel Ježíš všecka města i městečka, uče v školách jejich a káže evangelium království, a uzdravuje všelikou nemoc i všeliký neduh v lidu.
Yesu akazunguka katika miji yote na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi.
36 A když hleděl na zástupy, slitovalo se mu jich, že byli opuštěni a rozptýleni jako ovce, nemajíce pastýře.
Alipoona makutano, aliwahurumia kwa sababu walikuwa wanasumbuka bila msaada, kama kondoo wasiokuwa na mchungaji.
37 Tehdy řekl učedlníkům svým: Žeň zajisté jest mnohá, ale dělníků málo.
Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Mavuno ni mengi lakini watendakazi ni wachache.
38 Protož proste Pána žně, ať vypudí dělníky na žeň svou.
Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.”

< Matouš 9 >