< Matouš 14 >
1 V tom čase uslyšel Heródes čtvrták pověst o Ježíšovi.
Wakati huo, Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za Yesu,
2 I řekl služebníkům svým: To jest Jan Křtitel. Onť jest vstal z mrtvých, a protož se divové dějí skrze něho.
akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji; amefufuka kutoka kwa wafu! Hii ndiyo sababu nguvu za kutenda miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
3 Nebo jav Heródes Jana, svázal jej byl a dal do žaláře, pro Herodiadu manželku Filipa bratra svého.
Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake,
4 Nebo byl řekl jemu Jan: Nesluší tobě míti jí.
kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia Herode: “Si halali kwako kuwa na huyo mwanamke.”
5 A chtěv zabiti jej, bál se lidu; nebo za proroka jej měli.
Herode alitaka sana kumuua Yohana, lakini akaogopa watu, kwa maana walimtambua kuwa ni nabii.
6 Když pak slaven byl den narození Heródesova, tancovala dcera Herodiady u prostřed, i zalíbila se Heródesovi.
Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza mbele ya watu waliohudhuria, akamfurahisha sana Herode,
7 Pročež s přísahou zaslíbil jí dáti, zač by ho jen požádala.
kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kumpa huyo binti chochote angeomba.
8 A ona jsuci prvé navedena od mateře své, řekla: Dej mi zde na mise hlavu Jana Křtitele.
Huyo binti, akiwa amechochewa na mama yake, akasema, “Nipe kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.”
9 I zarmoutil se král, ale pro přísahu a pro ty, kteříž spolu s ním stolili, rozkázal dáti.
Mfalme akasikitika, lakini kwa sababu ya viapo alivyoapa mbele ya wageni, akaamuru kwamba apatiwe ombi lake.
10 A poslav kata, sťal Jana v žaláři.
Hivyo akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani.
11 I přinesena jest hlava jeho na mise, a dána té děvečce. I nesla mateři své.
Kichwa chake kikaletwa kwenye sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea mama yake.
12 A přišedše učedlníci jeho, vzali tělo a pochovali je; a šedše, pověděli Ježíšovi.
Wanafunzi wa Yohana wakaja na kuuchukua mwili wake kwenda kuuzika. Kisha wakaenda wakamwambia Yesu.
13 To uslyšev Ježíš, plavil se odtud na lodičce na místo pusté soukromí. Což uslyševše zástupové, šli za ním pěšky z měst.
Yesu aliposikia yaliyokuwa yametukia, aliondoka kwa chombo akaenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini watu walipopata habari, wakamfuata kwa miguu kupitia nchi kavu kutoka miji.
14 A vyšed Ježíš, uzřel zástup mnohý. I slitovalo mu se jich, a uzdravoval nemocné jejich.
Yesu alipofika kando ya bahari, aliona makutano makubwa ya watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa wao.
15 A když bylo k večerou, přistoupili k němu učedlníci jeho, řkouce: Pusté jest místo toto, a čas již pominul. Propusť zástupy, ať jdouce do městeček, nakoupí sobě pokrmů.
Ilipofika jioni, wanafunzi wake walienda kwake, wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na muda sasa umekwisha. Waage makutano ili waende zao vijijini wakajinunulie chakula.”
16 Ježíš pak řekl jim: Není jim potřebí odcházeti, dejte vy jim jísti.
Yesu akawaambia, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.”
17 A oni řkou jemu: Nemáme zde, než pět chlebů a dvě rybě.
Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na samaki wawili tu.”
18 On pak dí jim: Přinestež mi je sem.
Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.”
19 A rozkázav zástupu posaditi se na trávě, a vzav těch pět chlebů a dvě rybě, vzhléd v nebe, požehnal, a lámaje, dával učedlníkům ty chleby, a učedlníci zástupům.
Yesu akaagiza makutano wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia makutano.
20 I jedli všickni a nasyceni jsou. I sebrali, což zbylo drobtů, dvanácte košů plných.
Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21 Těch pak, kteříž jedli, bylo okolo pěti tisíců mužů, kromě žen a dětí.
Idadi ya watu waliokula walikuwa wanaume wapatao 5,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22 A i hned přinutil Ježíš učedlníky své, aby vstoupili na lodí a předešli jej na druhou stranu, dokudž by nepropustil zástupů.
Mara Yesu akawaambia wanafunzi wake waingie kwenye mashua watangulie kwenda ngʼambo ya bahari, wakati yeye alikuwa akiwaaga wale makutano.
23 A propustiv zástupy, vstoupil na horu soukromí, aby se modlil. A když byl večer, sám byl tam.
Baada ya kuwaaga, akaenda zake mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa huko peke yake.
24 Lodí pak již byla u prostřed moře, zmítající se vlnami, nebo byl vítr odporný.
Wakati huo ile mashua ilikuwa mbali kutoka nchi kavu ikisukwasukwa na mawimbi, kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
25 Při čtvrtém pak bdění nočním bral se k nim Ježíš, jda po moři.
Wakati wa zamu ya nne ya usiku, Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji.
26 A vidouce jej učedlníci po moři jdoucího, zlekali se, řkouce: Obluda jest. A strachem křičeli.
Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu, wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga yowe kwa kuogopa.
27 Ale i hned Ježíš promluvil k nim, řka: Doufejtež, jáť jsem, nebojte se.
Lakini mara Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Msiogope.”
28 I odpověděv jemu Petr, řekl: Pane, jestliže jsi ty, rozkaž mi k sobě přijíti po vodě.
Petro akamjibu, “Bwana, ikiwa ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.”
29 On pak řekl: Poď. A vystoupiv Petr z lodí, šel po vodě, aby přišel k Ježíšovi.
Yesu akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka kwenye chombo, akatembea juu ya maji kumwelekea Yesu.
30 Ale vida vítr tuhý, bál se. A počav tonouti, zkřikl, řka: Pane, pomoz mi.
Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”
31 A i hned Ježíš vztáh ruku, ujal jej a řekl jemu, Ó malé víry, pročežs pochyboval?
Mara Yesu akaunyoosha mkono wake na kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?”
32 A jakž oni vstoupili na lodí, utišil se vítr.
Nao walipoingia ndani ya mashua, upepo ukakoma.
33 Ti pak, kteříž na lodí byli, přistoupivše, klaněli se jemu, řkouce: Jistě Syn Boží jsi.
Ndipo wote waliokuwa ndani ya ile mashua wakamwabudu Yesu, wakisema, “Hakika, wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
34 A přeplavivše se, přišli do země Genezaretské.
Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya Genesareti.
35 A poznavše jej muži místa toho, rozeslali po vší té krajině vůkol, a shromáždili k němu všecky neduživé.
Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani. Watu wakamletea wagonjwa wao wote,
36 A prosili ho, aby se aspoň podolka roucha jeho dotkli. A kteřížkoli dotkli se, uzdraveni jsou.
wakamsihi awaruhusu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake, nao wote waliomgusa, wakaponywa.