< Lukáš 13 >

1 Byli pak tu přítomní času toho někteří, vypravujíce jemu o Galilejských, kterýchž krev Pilát smísil s obětmi jejich.
Wakati huo huo, kulikuwa na watu waliomwambia Yesu habari za Wagalilaya ambao Pilato aliwaua, na damu ya hao watu akaichanganya na dhabihu yao waliyokuwa wanatoa.
2 I odpověděv Ježíš, řekl jim: Co mníte, že ti Galilejští byli větší hříšníci nežli všickni Galilejští, že takové věci trpěli?
Yesu akawauliza, “Mnadhani kwamba hawa Wagalilaya ambao walikufa kifo cha namna hiyo walikuwa na dhambi kuwazidi Wagalilaya wengine wote?
3 Nikoli, pravím vám. Nýbrž nebudete-li pokání činiti, všickni též zahynete.
La hasha! Ninyi nanyi msipotubu, mtaangamia vivyo hivyo.
4 Aneb oněch osmnácte, na kteréž upadla věže v Siloe, a zbila je, zdali se domníváte, že by oni vinni byli nad všecky lidi, přebývající v Jeruzalémě?
Au wale watu kumi na wanane waliokufa walipoangukiwa na mnara huko Siloamu: mnadhani wao walikuwa waovu kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Yerusalemu?
5 Nikoli, pravím vám. Nýbrž nebudete-li pokání činiti, všickni též zahynete.
Nawaambia, la hasha! Ninyi nanyi msipotubu, wote mtaangamia vivyo hivyo.”
6 Pověděl pak toto podobenství: Člověk jeden měl strom fíkový štípený na vinici své. I přišel, hledaje ovoce na něm, ale nenalezl.
Kisha Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu, akaja ili kutafuta tini kwenye mti huo, lakini hakupata hata moja.
7 I řekl vinaři: Aj, po tři léta přicházím, hledaje ovoce na tom fíku, ale nenalézám. Vytniž jej. Proč i tu zemi darmo kazí?
Hivyo akamwambia mtunza shamba: ‘Tazama, kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda kwenye mtini huu, nami sikupata hata moja. Ukate! Kwa nini uendelee kuharibu ardhi?’
8 On pak odpověděv, řekl jemu: Pane, ponechejž ho i tohoto léta, ažť jej okopám a ohnojím,
“Yule mtunza shamba akamjibu, ‘Bwana, uache tena kwa mwaka mmoja zaidi, nami nitaupalilia na kuuwekea mbolea.
9 Zdali by nesl ovoce. Pakliť neponese, potom vytneš jej.
Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vyema, la sivyo uukate.’”
10 Učil pak v jedné škole v sobotu.
Basi Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo siku ya Sabato.
11 A aj, byla tu žena, kteráž měla ducha nemoci osmnáct let, a byla sklíčena, a nijakž se nemohla zpřímiti.
Wakati huo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na minane, wala alikuwa hawezi kunyooka wima.
12 A uzřev ji Ježíš, zavolal jí k sobě, a řekl jí: Ženo, zproštěna jsi od nemoci své.
Yesu alipomwona, akamwita, akamwambia, “Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako.”
13 I vložil na ni ruce, a i hned zdvihla se, a velebila Boha.
Yesu alipomwekea mikono yake, mara akasimama wima akaanza kumtukuza Mungu.
14 Tedy kníže školní odpověděv, hněvaje se proto, že v den sobotní uzdravoval Ježíš, řekl zástupu: Šest dní jest, v nichž náleží dělati; protož v těch přicházejíce, buďte uzdravováni, a ne v den sobotní.
Lakini kiongozi wa sinagogi akakasirika kwa sababu Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya Sabato. Akaambia ule umati wa watu, “Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi. Katika siku hizo, njooni mponywe, lakini si katika siku ya Sabato.”
15 I odpověděv jemu Pán, řekl: Pokrytče, zdali jeden každý z vás v sobotu neodvazuje vola svého neb osla od jeslí, a nevodí napájeti?
Lakini Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Je, kila mmoja wenu hamfungulii ngʼombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya Sabato?
16 Tato pak dcera Abrahamova, kterouž byl svázal satan, aj, již osmnácte let, což neměla býti rozvázána z svazku tohoto v den sobotní?
Je, huyu mwanamke, ambaye ni binti wa Abrahamu, aliyeteswa na Shetani akiwa amemfunga kwa miaka yote hii kumi na minane, hakustahili kufunguliwa kutoka kifungo hicho siku ya Sabato?”
17 A když on to pověděl, zastyděli se všickni protivníci jeho, ale všecken lid radoval se ze všech těch slavných skutků, kteříž se dáli od něho.
Aliposema haya, wapinzani wake wakaaibika, lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya.
18 I řekl: Čemu podobno jest království Boží, a k čemu je přirovnám?
Kisha Yesu akauliza, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaufananisha na nini?
19 Podobno jest zrnu horčičnému, kteréž vzav člověk, uvrhl do zahrady své. I rostlo, a učiněno jest v strom veliký, a ptactvo nebeské hnízda sobě dělali na ratolestech jeho.
Umefanana na punje ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake. Nayo ikakua, ikawa mti nao ndege wa angani wakatengeneza viota vyao kwenye matawi yake.”
20 A opět řekl: K čemu připodobním království Boží?
Yesu akauliza tena, “Nitaufananisha Ufalme wa Mungu na nini?
21 Podobno jest kvasu, kterýž vzavši žena, zadělala ve třech měřicích mouky, až zkysalo všecko.
Unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
22 I chodil po městech a městečkách, uče, bera se do Jeruzaléma.
Yesu akapita katika miji na vijiji, akifundisha wakati alisafiri kwenda Yerusalemu.
23 I řekl jemu jeden: Pane, co nemnozí jsou ti, kteří spaseni býti mají? On pak řekl jim:
Mtu mmoja akamuuliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?”
24 Snažujte se vcházeti těsnou branou; neboť (pravím vám, ) mnozí usilovati budou vjíti, ale nebudou moci.
Yesu akawaambia, “Jitahidini sana kuingia kupitia mlango mwembamba, kwa maana nawaambia wengi watajaribu kuingia, lakini hawataweza.
25 Když vstane hospodář, a zavře dvéře, a počnete vně státi a tlouci na dvéře, řkouce: Pane, Pane, otevři nám, a on odpovídaje, díť vám: Neznám vás, odkud jste:
Wakati mwenye nyumba atakapoondoka na kufunga mlango, mtasimama nje mkibisha mlango na kusema, ‘Bwana! Tufungulie mlango!’ “Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako.’
26 Tedy počnete říci: Jídali jsme a píjeli před tebou, a na ulicech našich jsi učíval.
“Ndipo mtamjibu, ‘Tulikula na kunywa pamoja nawe, tena ulifundisha katika mitaa yetu.’
27 I dí: Pravím vám, neznám vás, odkud jste. Odejdětež ode mne všickni činitelé nepravosti.
“Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
28 Tamť bude pláč a škřipení zubů, když uzříte Abrahama, a Izáka, a Jákoba, a všecky proroky v království Božím, sami pak sebe vyhnané ven.
“Ndipo kutakuwako kilio na kusaga meno, mtakapowaona Abrahamu, Isaki, Yakobo na manabii wote wakiwa katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi mkiwa mmetupwa nje.
29 I přijdouť od východu, a od západu, a od půlnoci, i od poledne, a budou stoliti v království Božím.
Watu watatoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, nao wataketi kwenye sehemu walizoandaliwa karamuni katika Ufalme wa Mungu.
30 A aj, jsouť poslední, kteříž budou první, a jsou první, kteříž budou poslední.
Tazama, kunao walio wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, nao wa kwanza watakaokuwa wa mwisho.”
31 A v ten den přistoupili někteří z farizeů, řkouce jemu: Vyjdi, a odejdi odsud, nebo Heródes chce tě zamordovati.
Wakati huo huo baadhi ya Mafarisayo wakamwendea Yesu na kumwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine kwa maana Herode anataka kukuua.”
32 I řekl jim: Jdouce, povězte lišce té: Aj, vymítám ďábly, a uzdravuji dnes a zítra, a třetího dne dokonám.
Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, ‘Ninafukuza pepo wachafu na kuponya wagonjwa leo na kesho, nami siku ya tatu nitaikamilisha kazi yangu.’
33 Ale však musím dnes a zítra i po zejtří choditi; neboť nelze proroku zahynouti kromě Jeruzaléma.
Sina budi kuendelea na safari yangu leo, kesho na kesho kutwa: kwa maana haiwezekani nabii kufa mahali pengine isipokuwa Yerusalemu.
34 Jeruzaléme, Jeruzaléme, ješto morduješ proroky, a kamenuješ ty, kteříž k tobě bývají posláni, kolikrát jsem chtěl shromážditi dítky tvé, jako slepice kuřátka svá pod křídla? Ale nechtěli jste.
“Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka!
35 Aj, zanechán bude vám dům váš pustý. Ale jistě pravím vám, že nikoli mne neuzříte, ažť přijde, když díte: Požehnaný, kterýž se béře ve jménu Páně.
Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa. Ninawaambia, hamtaniona tena mpaka wakati ule mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana.’”

< Lukáš 13 >