< Lukáš 1 >

1 Poněvadž mnozí usilovali sepsati pořádně vypravování těch věcí, kteréž u nás jisté jsou,
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 Jakž nám vydali ti, kteříž od počátku sami viděli, a služebníci toho Slova byli:
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 Vidělo se i mně, kterýž jsem toho všeho pravé povědomosti z gruntu bedlivě došel, tobě o tom pořádně vypsati, výborný Teofile,
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 Abys zvěděl jistotu těch věcí, jimž jsi vyučován.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 Byl za dnů Heródesa krále Judského kněz nějaký, jménem Zachariáš, z třídy Abiášovy, a manželka jeho ze dcer Aronových, a jméno její Alžběta.
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 Byli pak oba spravedliví před oblíčejem Božím, chodíce ve všech přikázaních a spravedlnostech Páně bez ouhony.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 A neměli plodu, proto že Alžběta byla neplodná, a oba se byli zstarali ve dnech svých.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 I stalo se, když on úřad kněžský konal v pořádku třídy své před Bohem,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 Že vedlé obyčeje úřadu kněžského los naň přišel, aby položil zápal, vejda do chrámu Páně.
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 A všecko množství lidu bylo vně, modlíce se v hodinu zápalu.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 Tedy ukázal se jemu anděl Páně, stoje na pravé straně oltáře zápalu.
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 A uzřev jej Zachariáš, zstrašil se, a bázeň připadla na něj.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 I řekl jemu anděl: Neboj se, Zachariáši, neboť jest uslyšána modlitba tvá, a Alžběta manželka tvá porodí tobě syna, a nazůveš jméno jeho Jan.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 Z čehož budeš míti radost a veselé, a mnozí se z jeho narození budou radovati.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 Bude zajisté veliký před oblíčejem Páně, a vína i nápoje opojného nebude píti, a Duchem svatým bude naplněn hned od života matky své.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 A mnohé z synů Izraelských obrátí ku Pánu Bohu jejich.
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 Neboť on předejde před oblíčejem jeho v duchu a v moci Eliášově, aby obrátil srdce otců k synům, a nevěřící k opatrnosti spravedlivých, aby postavil Pánu lid hotový.
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 I řekl Zachariáš andělu: Po čemž to poznám? Nebo já starý jsem, a manželka má zstarala se ve dnech svých.
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 I odpověděv anděl, řekl jemu: Jáť jsem Gabriel, kterýž stojím před oblíčejem Božím, a poslán jsem, abych mluvil s tebou, a tyto věci veselé tobě zvěstoval.
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 A aj, budeš němý, a nebudeš moci mluviti až do dne, v kterémž se tyto věci stanou, proto že jsi neuvěřil řečem mým, kteréž se naplní časem svým.
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 Lid pak očekával Zachariáše, a divili se, že on tak prodléval v chrámě.
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 Vyšed pak, nemohl mluviti k nim. I srozuměli, že vidění viděl v chrámě. Nebo on návěští jim dával, a zůstal němý.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 I stalo se, když se vyplnili dnové konání úřadu jeho, odšel do domu svého.
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 A po těch dnech počala Alžběta manželka jeho, a tajila se za pět měsíců, řkuci:
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 Že tak mi učinil Pán ve dnech, v nichž vzezřel, aby odjal mé pohanění mezi lidmi.
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 V měsíci pak šestém poslán jest anděl Gabriel od Boha do města Galilejského, kterémuž jméno Nazarét,
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 Ku panně zasnoubené muži, kterémuž jméno bylo Jozef, z domu Davidova, a jméno panny Maria.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 I všed k ní anděl, dí: Zdráva buď milostí obdařená, Pán s tebou, požehnaná ty mezi ženami.
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 Ona pak uzřevši ho, zarmoutila se nad řečí jeho, a myslila, jaké by to bylo pozdravení.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 I řekl jí anděl: Neboj se, Maria, nebo jsi nalezla milost u Boha.
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 A počneš v životě, a porodíš syna, a nazůveš jméno jeho Ježíš.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 Tenť bude veliký, a Syn Nejvyššího slouti bude, a dáť jemu Pán Bůh stolici Davida otce jeho.
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 A kralovati bude v domě Jákobově na věky, a království jeho nebude konce. (aiōn g165)
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 I řekla Maria andělu: Kterak se to stane, poněvadž já muže nepoznávám?
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 A odpověděv anděl, řekl jí: Duch svatý sstoupí v tě, a moc Nejvyššího zastíní tobě; a protož i to, což se z tebe svatého narodí, slouti bude Syn Boží.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 A aj, Alžběta, přítelkyně tvá, i ona počala syna v starosti své, a tento jest jí šestý měsíc, kteráž sloula neplodná.
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 Neboť nebude nemožné u Boha žádné slovo.
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 I řekla Maria: Aj, děvka Páně, staniž mi se podlé slova tvého. I odšel od ní anděl.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 Tedy povstavši Maria v těch dnech, odešla na hory s chvátáním do města Judova.
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 I vešla do domu Zachariášova, a pozdravila Alžběty.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 I stalo se, jakž uslyšela Alžběta pozdravení Marie, zplésalo nemluvňátko v životě jejím, a naplněna jest Duchem svatým Alžběta.
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 I zvolala hlasem velikým a řekla: Požehnaná ty mezi ženami, a požehnaný plod života tvého.
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 A odkud mi to, aby přišla matka Pána mého ke mně?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 Nebo aj, jakž se stal hlas pozdravení tvého v uších mých, zplésalo radostně nemluvňátko v životě mém.
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 A blahoslavená, kteráž uvěřila, neboť dokonány budou ty věci, kteréž jsou povědíny jí ode Pána.
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 Tedy řekla Maria: Velebí duše má Hospodina,
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 A veselí se duch můj v Bohu, spasiteli svém,
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 Že vzezřel na ponížení děvky své; neb aj, od této chvíle blahoslaviti mne budou všickni národové.
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 Neboť mi učinil veliké věci ten, kterýž mocný jest, a svaté jméno jeho,
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 A jehož milosrdenství od pokolení až do pokolení bojícím se jeho.
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 Dokázal moci ramenem svým, rozptýlil pyšné myšlením srdce jejich.
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 Sházel mocné s stolic, a povýšil ponížených.
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 Lačné nakrmil dobrými věcmi, a bohaté pustil prázdné.
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 Přijal Izraele, služebníka svého, byv pamětliv na milosrdenství,
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 Jakož mluvil otcům našim, Abrahamovi a semeni jeho na věky. (aiōn g165)
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
56 I zůstala Maria s ní asi za tři měsíce, a navrátila se do domu svého.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 Alžbětě pak naplnil se čas, aby porodila, i porodila syna.
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 A uslyšeli sousedé a přátelé její, že Hospodin veliké učinil s ní milosrdenství své, i radovali se spolu s ní.
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 Stalo se pak v den osmý, přišli obřezovati dítěte, a nazývali jej jménem otce jeho Zachariášem.
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 Ale odpověděvši matka jeho, řekla: Nikoli, ale slouti bude Jan.
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 I řekli jí: Však žádného není v rodu tvém, kterýž by sloul jménem tím.
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 I dávali návěští otci jeho, jak by ho chtěl nazývati.
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 A on požádav deštičky, napsal, řka: Jan jest jméno jeho. I divili se všickni.
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 A hned otevřela se ústa jeho a jazyk jeho, i mluvil, velebě Boha.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 Tedy přišla bázeň na všecky sousedy jejich, a po všech horách Judských rozhlásána jsou všecka ta slova.
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 A všickni, kteříž o tom slyšeli, skládali to v srdci svém, řkouce: I jaké dítě toto bude? A ruka Páně byla s ním.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 Zachariáš pak otec jeho naplněn jest Duchem svatým, a prorokoval, řka:
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 Požehnaný Pán Bůh Izraelský, že navštívil a učinil vykoupení lidu svému.
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 A vyzdvihl nám roh spasení v domě Davida, služebníka svého,
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 Jakož mluvil skrze ústa proroků svých svatých, kteříž byli od věků, (aiōn g165)
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
71 O vysvobození z nepřátel našich, a z ruky všech, kteříž nás nenáviděli,
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 Aby učinil milosrdenství s otci našimi, a rozpomenul se na smlouvu svou svatou,
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 Na přísahu, kterouž přisáhl Abrahamovi, otci našemu, žeť nám to dá,
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 Abychom bez strachu, z ruky nepřátel svých jsouce vysvobozeni, sloužili jemu,
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 V svatosti a v spravedlnosti před oblíčejem jeho, po všecky dny života svého.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 Ty pak, dítě, prorokem Nejvyššího slouti budeš, nebo předejdeš před tváří Páně připravovati cesty jeho,
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 Aby dáno bylo umění spasitelné lidu jeho na odpuštění hříchů jejich,
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 Skrze střeva milosrdenství Boha našeho, v nichž navštívil nás, vyšed z výsosti,
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 Aby se ukázal sedícím v temnostech a v stínu smrti, k spravení noh našich na cestu pokoje.
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 Dítě pak rostlo, a posilovalo se v duchu, a bylo na poušti až do dne zjevení svého lidu Izraelskému.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

< Lukáš 1 >