< 3 Mojžišova 6 >
1 Mluvil opět Hospodin k Mojžíšovi, řka:
Bwana akamwambia Mose:
2 Kdyby člověk zhřešil a přestoupením přestoupil proti Hospodinu, buď že by oklamal bližního svého v věci sobě svěřené, aneb v spolku nějakém, aneb mocí by vzal něco, aneb lstivě podvedl bližního svého,
“Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
3 Buď že nalezna ztracenou věc, zapřel by mu ji, buď že by přisáhl falešně, kteroukoli věcí z těch, kterouž přihází se člověku učiniti a zhřešiti jí,
au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
4 Když by tedy zhřešil a vinen byl: navrátí zase tu věc, kterouž mocí sobě vzal, aneb tu, kteréž lstivě s útiskem dosáhl, aneb tu, kteráž mu svěřena byla, aneb ztracenou věc, kterouž nalezl,
wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
5 Aneb o kterékoli věci falešně přisáhl: tedy navrátí to z cela, a nad to pátý díl toho přidá tomu, číž bylo; to navrátí v den oběti za hřích svůj.
au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
6 Obět pak za hřích svůj přivede Hospodinu z drobného dobytku, skopce bez poškvrny, vedlé ceny tvé, v obět za vinu knězi.
Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
7 I očistí jej kněz před Hospodinem, a odpuštěno mu bude, jedna každá z těch věcí, kterouž by učinil a jí vinen byl.
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
8 I mluvil Hospodin k Mojžíšovi, řka:
Bwana akamwambia Mose:
9 Přikaž Aronovi i synům jeho a rci: Tento bude řád při oběti zápalné: (slove pak obět zápalná od pálení na oltáři celou noc až do jitra, nebo oheň na oltáři vždycky hořeti bude, )
“Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
10 Obleče se kněz v roucho své lněné, a košilku lněnou vezme na tělo své, a vyhrabe popel, když oheň spálí obět zápalnou na oltáři, a vysype jej u oltáře.
Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
11 Potom svleče šaty své a obleče se v roucho jiné, a vynese popel ven z stanů na místo čisté.
Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
12 Oheň pak, kterýž jest na oltáři, bude hořeti na něm, nebude uhašován. A bude zapalovati jím kněz dříví každého jitra, a zpořádá na něm obět zápalnou, a páliti bude na něm tuk pokojných obětí.
Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
13 Oheň ustavičně hořeti bude na oltáři, a nebudeť uhašen.
Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
14 Tento pak bude řád při oběti suché, kterouž obětovati budou synové Aronovi Hospodinu u oltáře:
“‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
15 Vezme hrst bělné mouky z oběti té a z oleje jejího, se vším tím kadidlem, kteréž bude na oběti suché, a páliti to bude na oltáři u vůni líbeznou, pamětné její Hospodinu.
Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
16 Což pak zůstane z ní, to jísti budou Aron i synové jeho; přesné jísti se bude na místě svatém, v síni stánku úmluvy jísti to budou.
Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
17 Nebude vařeno s kvasem, nebo jsem jim to dal za díl z obětí mých ohnivých; svaté svatých to jest, jako i obět za hřích a jako obět za vinu.
Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
18 Každý mužského pohlaví z synů Aronových jísti bude to právem věčným po rodech vašich, z ohnivých obětí Hospodinových. Což by se koli dotklo toho, svaté bude.
Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
19 I mluvil Hospodin k Mojžíšovi, řka:
Tena Bwana akamwambia Mose,
20 Tato jest obět Aronova a synů jeho, kterouž obětovati budou Hospodinu v den pomazání jeho: Desátý díl míry efi mouky bělné za obět suchou ustavičnou, polovici toho ráno a polovici u večer.
“Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
21 Na pánvici s olejem strojena bude; smaženou přineseš ji, a pečené kusy oběti suché obětovati budeš u vůni spokojující Hospodina.
Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
22 A kněz, kterýž z synů jeho po něm pomazán bude, ať ji obětuje právem věčným. Hospodinu všecko to páleno bude.
Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
23 A všeliká suchá obět kněžská celá spálena bude; nebudeť jedena.
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
24 Mluvil pak Hospodin k Mojžíšovi, řka:
Bwana akamwambia Mose,
25 Mluv Aronovi a synům jeho a rci: Tento bude řád oběti za hřích: Na místě, kdež se zabijí obět zápalná, zabita bude obět za hřích před Hospodinem; svatá svatých jest.
“Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
26 Kněz obětující tu obět za hřích budeť jísti ji; na místě svatém jedena bude v síni stánku úmluvy.
Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
27 Což by se koli dotklo masa jejího, svaté bude; a jestliže by krví její šaty skropeny byly, to, což skropeno jest, obmyješ na místě svatém.
Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
28 A nádoba hliněná, v níž by vařeno bylo, rozražena bude; pakli by v nádobě měděné vařeno bylo, vytřena a vymyta bude vodou.
Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
29 Všeliký pohlaví mužského mezi kněžími jísti to bude; svaté svatých jest.
Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
30 Ale žádná obět za hřích, (z jejížto krve něco vneseno bylo by do stánku úmluvy k očištění v svatyni, ) nebude jedena; ohněm spálena bude.
Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.