< Józua 7 >

1 Zhřešili pak synové Izraelští přestoupením při věcech proklatých; nebo Achan, syn Charmi, syna Zabdi, syna Záre, z pokolení Juda, vzal něco z věcí proklatých. Pročež rozpálila se prchlivost Hospodinova na syny Izraelské.
Lakini watu wa Israeli hawakutenda katika uaminifu kuhusiana na vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu. Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka katika kabila la Yuda, alivitwaa baadhi ya vitu hivyo vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya uharibifu, na hasira ya Yahweh iliwaka juu yawatu wa Israeli.
2 Nebo když poslal Jozue muže některé od Jericha do Hai, kteréž bylo blízko Betaven, k východní straně Bethel, a mluvil k nim, řka: Vstupte a shlédněte zemi, vstoupili tedy muži ti, a shlédli Hai.
Yoshua alituma watu kutoka Yeriko kwenda Ai, mji uliokuwa karibu na Bethi Aveni, mashariki mwa Betheli. Aliwaambia, “Nendeni na mkaipeleleza nchi.” Wale watu walikwea na kuipeleleza Ai.
3 Kteřížto navrátivše se k Jozue, řekli jemu: Nechť nevstupuje všecken lid tento, okolo dvou tisíc mužů neb okolo tří tisíců mužů nechť vstoupí, a dobudouť Hai; neobtěžuj všeho lidu, vysílaje jej tam, nebo málo jest oněchno.
Waliporudi kwa Yoshua, walimwambia, “Usitume watu wote kwenda Ai. Tuma tu watu elfu mbili au elfu tatu waende kuiteka Ai. Usiwafanye watu wateseke katika vita, kwani ni watu wachache.”
4 Tedy vytáhlo jich z lidu tam okolo tří tisíc mužů, a utekli před muži města Hai.
Hivyo ni watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi ndio walioenda, lakini watu hawa waliwakimbia watu wa Ai.
5 I zabili z nich obyvatelé Hai okolo třidcíti a šesti mužů, a honili je od brány až k Sabarim, a porazili je, když s vrchu utíkali. I rozpustilo se srdce lidu, a bylo jako voda.
Watu wa Ai waliwaua watu wapatao thelathini na sita, waliwafuata katika lango la mji hadi katika machimbo ya mawe, na waliwauwa walipokuwa wakishuka katika kilima. Na mioyo ya watu ilijawa hofu na ujasiri wao ukawatoka.
6 Tedy Jozue roztrhl roucho své, a padl tváří svou na zem před truhlou Hospodinovou, a ležel až do večera, ano i starší Izraelští, a sypali prach na hlavy své.
Basi Yoshua alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh, na walibaki pale mpaka jioni.
7 I řekl Jozue: Ach, Panovníče Hospodine, proč jsi kdy převedl lid tento přes Jordán, abys nás vydal v ruku Amorejského, tak aby nás zahubil? Ó kdybychom byli raději zůstali za Jordánem.
Kisha Yoshua akasema, “Oo, Yahweh Bwana, kwanini umewavusha watu hawa ng'ambo ya Yordani? Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza? ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti na tungekaa katika upande mwingine wa Yordani!
8 Ó Pane, což mám říci, když již lid Izraelský utíká před nepřátely svými?
Bwana, niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao?
9 Nebo uslyšíce Kananejští a všickni obyvatelé země, obklíčí nás vůkol, a vyhladí jméno naše z země. I což to učiníš jménu svému velikému?
Kwa kuwa Wakaanani na wenyeji wote wa nchi watakaposikia, watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu. Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?
10 I řekl Hospodin k Jozue: Vstaň. Proč jsi padl na tvář svou?
Yahweh akamwambia Yoshua, “Inuka! kwanini umelala kifudifudi?
11 Zhřešil Izrael, tak že smlouvu mou přestoupili, kterouž jsem jim přikázal; nebo jsou i vzali z věcí proklatých, k tomu i ukradli, také i sklamali, nad to i odložili mezi nádobí svá.
Israeli imetenda dhambi. Wamevunja agano langu nililowaagiza. Wameiba baadhi ya vitu vilivyokuwa vimetengwa. Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao kwa kuweka vitu vile walivyochukua miongoni mwa mali zao wenyewe.
12 Protož nebudou moci synové Izraelští ostáti před nepřátely svými, utíkati budou před nepřátely svými, nebo poškvrnili se věcí proklatou. Nebuduť více s vámi, leč vyhladíte prokletí to z prostředku svého.
Na matokeo yake ni kwamba watu wa Israeli hawataweza kusimama mbele za maadui zao. Walitega migongo yao kwa maadui zao kwasababu wao wenyewe wametengwa kwa ajili ya uharibifu. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka pale mtakapoteketeza vitu vile vilivyotakiwa kuharibiwa, lakini sasa bado viko miongoni mwenu.
13 Vstaň, posvěť lidu a rci: Posvěťte se k zítřku; nebo takto praví Hospodin Bůh Izraelský: Věc proklatá jest u prostřed tebe, Izraeli, nebudeš moci ostáti před nepřátely svými, dokudž neodejmeš prokletí toho z prostředku svého.
Inuka! Waweke watu wakfu kwangu, na uwaambie, 'Jiwekeeni wakfu ninyi wenyewe kesho. Kwa kuwa, Yahweh, Mungu wa Israeli asema hivi, “Kuna vitu vilitengwa ili kuteketezwa ambavyo bado viko miongoni mwenu, Israeli. Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu mpaka pale mtakapoviondoa miongoni mwenu vitu vyote ambavyo vilitengwa kwa ajili ya kuteketezwa.”
14 Protož přistupovati budete ráno po pokoleních svých, a pokolení, kteréž ukáže Hospodin, přistupovati bude po rodech, takž rod, kterýž ukáže Hospodin, přistupovati bude po domích, a dům, kterýž ukáže Hospodin, přistupovati bude po osobách.
Asubuhi, mtajisogeza wenyewe kwa makabila. Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake. Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba. Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja.
15 Kdož pak postižen bude vinný věcí proklatou, ohněm spálen bude, on i všecko, což jeho jest, proto že přestoupil smlouvu Hospodinovu, a že učinil nešlechetnost v Izraeli.
Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa na aliye navyo vitu hivyo vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, atachomwa moto, yeye na kila kitu alichonacho, kwasababu amelivunja agano la Yahweh na kwasababu amefanya jambo la aibu katika Israeli.'”
16 Vstav tedy Jozue ráno, kázal přistupovati Izraelovi po pokoleních jejich. I postiženo jest pokolení Judovo.
Basi, Yoshua aliamka asubuhi na mapema na aliwaleta Israeli karibu, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda lilichaguliwa.
17 Tedy když kázal přistupovati čeledem Juda, postižena jest čeled Záre. Potom kázal přistupovati čeledi Záre po osobách, a postižen jest Zabdi.
Yoshua akazisogeza koo za Yuda karibu, na ukoo wa Zera ulichaguliwa. Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu, na Zabdi alichaguliwa.
18 I kázal přistupovati domu jeho po osobách, i postižen jest Achan, syn Charmi, syna Zabdi, syna Záre z pokolení Judova.
Akaisogeza karibu nyumba ya Zabdi mtu kwa mtu, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka kabila la Yuda, alichaguliwa.
19 I řekl Jozue Achanovi: Synu můj, dej, prosím, chválu Hospodinu Bohu Izraelskému, a vyznej se jemu, a oznam mi aspoň již, co jsi učinil, netaj již toho přede mnou.
Kisha Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, niambie ukweli mbele za Yahweh, Mungu wa Israel, na ufanye ukiri wako kwake. Tafadhali niambie kile ulichofanya. Usinifiche.”
20 Tedy odpovídaje Achan k Jozue, řekl: Pravdať jest, já jsem zhřešil proti Hospodinu Bohu Izraelskému, tak že to a toto jsem učinil.
Akani akamjibu Yoshua, “Kwa kweli nimetenda dhambi mbele Yahweh, Mungu wa Israeli.
21 Viděl jsem mezi loupeží plášť jeden Babylonský pěkný, a dvě stě lotů stříbra, a prut zlatý jeden, padesáte lotů ztíží, čehož požádav, vzal jsem to, a aj, jsou ty věci skryté v zemi prostřed stanu mého, a stříbro pod tím.
Nilichofanya ni hiki: Nilipoona miongoni mwa nyara mkoti mzuri kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kipande cha dhahabu chenye uzito wa shekeli hamsini, nilivitamani na nikavichukua. Vimefichwa chini ardhini katikati ya hema langu, na fedha iko chini yake.”
22 Tedy poslal Jozue posly, kteříž běželi do stanu, a aj, bylo to skryto v stanu jeho, a stříbro pod tím.
Yoshua akatuma wajumbe waliokimbia mpaka kwenye hema mahali palipokuwa na vile vitu. Walipoangalia, waliviona vimefichwa katika hema lake, na fedha chini yake.
23 A vzavše to z stanu, přinesli k Jozue a ke všechněm synům Izraelským, a položili ty věci před Hospodinem.
Walivichukua vitu hivyo kutoka katikati ya hema na kuvileta kwa Yoshua na watu wote wa Israeli. Walivimwaga mbele za Yahweh.
24 Vzav tedy Jozue a všecken Izrael s ním Achana, syna Záre, a stříbro i plášť, i prut zlatý, i syny jeho, i dcery jeho, voly a osly, dobytek i stan jeho i všecko, což měl, vyvedli je do údolí Achor.
Kisha Yoshua na Waisraeli wote pamoja naye, walimchukua Akani mwana wa Zera, na fedha, na koti, na kipande cha dhahabu, wana na binti zake, ng'ombe zake, punda zake, kondoo zake, hema lake, na kila kitu alichokuwa nacho, na wakavileta hata bonde la Akori.
25 Kdež řekl Jozue: Proč jsi zkormoutil nás? Zkormutiž tebe Hospodin v tento den. I uházel jej všecken lid kamením, a spálili je ohněm, ukamenovavše je kamením.
Kisha Yoshua akasema, “Kwanini umetusumbua? Leo Yahweh atakutesa na wewe.” Waisraeli wote wakampiga kwa mawe. Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe.
26 Potom nametali naň hromadu kamení velikou, kteráž trvá až do tohoto dne; a tak odvrácen jest Hospodin od hněvu prchlivosti své. Protož nazváno jest jméno místa toho údolí Achor, až do dnešního dne.
Kisha wakaweka juu yake kichuguu kikubwa cha mawe ambayo yapo hata leo. Yahweh akaachilia mbali hasira yake. Hivyo basi, jina la mahali hapo likawa Akori hata leo.

< Józua 7 >