< Izaiáš 30 >

1 Běda synům zpurným, dí Hospodin, skládajícím radu, kteráž není ze mne, a přikrývajícím ji přikrytím, ale ne z ducha mého, aby hřích k hříchu přidávali;
Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
2 Kteříž chodí a sstupují do Egypta, nedotazujíce se úst mých, aby se zmocňovali v síle Faraonově, a doufali v stínu Egyptském.
wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
3 Nebo síla Faraonova bude vám k hanbě, a to odpočívání v stínu Egyptském k lehkosti,
Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
4 Proto že knížata jeho byli v Soan, a poslové jeho do Chanes chodili.
Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
5 Všeckyť k zahanbení přivede skrze lid, kterýž jim nic neprospěje, aniž bude ku pomoci, ani k užitku, ale k hanbě toliko a k útržce.
kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
6 Břímě hovad poledních v zemi nátisku a ssoužení, odkudž lev a lvíče, ještěrka a drak ohnivý létající, odnesou na hřbetě hovádek bohatství svá, a na hrbu velbloudů poklady své k lidu, kterýž jim nic neprospěje.
Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
7 Nebo Egyptští nadarmo a na prázdno pomáhati budou. Pročež ohlašuji to, že by síla jejich byla s pokojem seděti.
kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
8 Nyní jdi, napiš to na tabuli před očima jejich, a na knize vyrej to, aby to zůstávalo do nejposlednějšího dne, a až na věky věků,
Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
9 Že lid tento zpurný jest, synové lháři, synové, kteříž nechtí poslouchati zákona Hospodinova;
Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
10 Kteříž říkají vidoucím: Nemívejte vidění, a prorokům: Neprorokujte nám toho, což pravého jest; mluvte nám pochlebenství, prorokujte oklamání.
Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
11 Sejděte s cesty, svozujte od stezky, nechať se vzdálí od tváří naší Svatý Izraelský.
Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
12 Protož takto praví Svatý Izraelský: Proto že pohrdáte slovem tím, a doufáte ve lsti a v převrácenosti, a spoléháte na ni:
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
13 Z té příčiny bude vám tato nepravost jako zed tržená padající, a vydutí na zdi vysoké, jejíž brzké a náhlé bývá oboření.
dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
14 A rozrazí ji, jako rozrážejí nádobu hrnčířskou rozbitou; neodpustíť, tak že nebude nalezena po rozražení jejím ani střepina k nabrání ohně z ohniště, anebo k nabrání vody z louže.
Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
15 Nebo tak řekl Panovník Hospodin, Svatý Izraelský: Obrátíte-li se, a spokojíte-li se, zachováni budete. V utišení se a v doufání bude síla vaše. Ale nechcete.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
16 Nýbrž říkáte: Nikoli, ale na koních utečeme. Protož utíkati budete. Na rychlých ujedeme. Ale rychlejší budou stihající vás.
Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
17 Jeden tisíc před okřiknutím jednoho, a před okřiknutím pěti utíkati budete, až (jestliže však vás co pozůstane), budete zanecháni jako okleštěné dřevo na vrchu hory, a jako korouhev na pahrbku.
Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
18 Protoť pak shovívá Hospodin, milost vám čině, a protoť se vyvýší, aby se smiloval nad vámi; nebo Hospodin jest Bůh spravedlivý. Blahoslavení všickni, kteříž očekávají na něj.
Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
19 Lid zajisté na Sionu a v Jeruzalémě bydliti bude. Nikoli plakati nebudeš; k hlasu volání tvého bude všelijak milost činiti s tebou. Hned jakž uslyší, ohlásíť se.
Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
20 A ačkoli Pán dá vám chleba úzkosti a vody ssoužení, však nebudou více odjati tobě učitelé tvoji, ale očima svýma vídati budeš učitele své,
Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
21 A ušima svýma slýchati slovo tobě po zadu řkoucích: Toť jest ta cesta, choďte po ní, buď že byste se na pravo neb na levo uchýlili.
Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
22 Tedy zavržete obestření rytin svých stříbrných, a oděv slitin svých zlatých; odloučíš je jako nemoc svou trpící, řka jim: Táhněte tam.
Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
23 Dáť i déšť na rozsívání tvé, kterýmž bys osíval zemi, a chléb z úrody země, kterýž bude jadrný a zdárný; v ten den pásti se bude i dobytek tvůj na pastvišti širokém.
Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
24 Volové také i oslové, dělající zemi, píci čistou jísti budou, kteráž opálkou a věječkou vyčištěna bývá.
Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
25 Budou také na všeliké hoře vysoké, a na všelikém pahrbku vyvýšeném pramenové a potokové vod, v den porážky veliké, když padnou věže.
Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
26 Bude i světlo měsíce jako světlo slunce, světlo pak slunce bude sedmernásobní, jako světlo sedmi dnů, v den, v kterýž uváže Hospodin zlámání lidu svého, a ránu zbití jeho uzdraví.
Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
27 Aj, jméno Hospodinovo přichází z daleka, jehožto hněv hořící a těžká pomsta; rtové jeho naplněni jsou prchlivostí, a jazyk jeho jako oheň sžírající.
Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
28 Duch pak jeho jako potok rozvodnilý, kterýž až do hrdla dosáhne, aby tříbil národy, až by v nic obráceni byli, a uzdou svíral čelisti národů.
Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
29 I budete zpívati, jako když se v noci zasvěcuje slavnost, a veseliti se srdečně, jako ten, kterýž jde s píšťalkou, bera se na horu Hospodinovu, k skále Izraelově,
Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
30 Když dá slyšeti Hospodin hlas důstojnosti své, a ukáže vztaženou ruku svou s hněvem prchlivosti a plamenem ohně sžírajícího, an vše rozráží i přívalem i kamenným krupobitím.
Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
31 Hlasem zajisté Hospodinovým potřín bude Assur, kterýž jiné kyjem bijíval.
Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
32 Ale stane se, že každé udeření holí, kterouž doloží na něj Hospodin, silně dolehne; s bubny a harfami a bitvou veselou bojovati bude proti němu.
Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
33 Nebo připraveno jest již dávno peklo, také i samému králi připraveno jest. Hluboké a široké je učinil, hranic jeho, ohně a dříví mnoho; dmýchání Hospodinovo jako potok siry je zapaluje. (questioned)
Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.

< Izaiáš 30 >