< Ezechiel 10 >

1 I viděl jsem, a aj, na obloze, kteráž byla nad hlavou cherubínů, jako kámen zafirový na pohledění, jako podobenství trůnu se ukázalo nad nimi.
Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
2 Tedy promluviv k muži tomu oděnému rouchem lněným, řekl: Vejdi do prostřed kol pod cherubíny, a naplň hrsti své uhlím řeřavým z prostředku cherubínů, a roztrus po městě. Kterýžto všel před očima mýma.
Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
3 (Cherubínové pak stáli po pravé straně domu, když vcházel muž ten, a oblak hustý naplnil síň vnitřní.
Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
4 Nebo když se byla zdvihla sláva Hospodinova s cherubínů k prahu domu, tedy naplněn byl dům tím hustým oblakem, a síň naplněna byla bleskem slávy Hospodinovy.
Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
5 Zvuk také křídel cherubínů slyšán byl až k té síni zevnitřní jako hlas Boha silného, všemohoucího, když mluví.)
Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
6 I stalo se, když přikázal muži tomu oděnému rouchem lněným, řka: Vezmi ohně z prostředku kol, z prostředku cherubínů, že všel a postavil se podlé kol.
Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
7 Tedy vztáhl cherubín jeden ruku svou z prostředku cherubínů k ohni tomu, kterýž byl u prostřed cherubínů, a vzav, dal do hrsti toho oděného rouchem lněným. Kterýžto vzal a vyšel.
Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
8 Nebo ukazovalo se na cherubíních podobenství ruky lidské pod křídly jejich.
(Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
9 I viděl jsem, a aj, čtyři kola podlé cherubínů, jedno kolo podlé jednoho každého cherubína, podobenství pak kol jako barva kamene tarsis.
Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
10 A na pohledění měla podobnost jednostejnou ta kola, jako by bylo kolo u prostřed kola.
Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
11 Když chodili, na čtyři strany jejich chodili. Neuchylovali se, když šli, ale k tomu místu, kamž se obracel vůdce, za ním šli. Neuchylovali se, když šli.
Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
12 Všecko také tělo jejich i hřbetové jejich, i ruce jejich, i křídla jejich, též i kola plná byla očí vůkol jich samých čtyř i kol jejich.
Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
13 Kola pak ta nazval okršlkem, jakž slyšely uši mé.
Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
14 Čtyři tváři mělo každé. Tvář první tvář cherubínová, tvář pak druhá tvář člověčí, a třetí tvář lvová, čtvrtá pak tvář orličí.
Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
15 I zdvihli se cherubínové. To jsou ta zvířata, kteráž jsem viděl u řeky Chebar.
Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
16 Když pak šli cherubínové, šla i kola podlé nich, a když vznášeli cherubínové křídla svá, aby se pozdvihli od země, neuchylovala se také kola od nich.
Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
17 Když stáli oni, stála, a když se vyzdvihovali, vyzdvihovala se s nimi; nebo duch zvířat byl v nich.
Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
18 I odešla sláva Hospodinova od prahu domu, a stála nad cherubíny,
Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
19 Hned jakž pozdvihli cherubínové křídel svých a vznesli se od země, před očima mýma odcházejíce, a kola naproti nim, a stála u vrat brány domu Hospodinova východní, a sláva Boha Izraelského svrchu nad nimi.
Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
20 To jsou ta zvířata, kteráž jsem viděl pod Bohem Izraelským u řeky Chebar, a poznal jsem, že cherubínové byli.
Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
21 Po čtyřech tvářích měl jeden každý, a po čtyřech křídlích jeden každý; podobenství také rukou lidských pod křídly jejich.
Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
22 Podobenství pak tváří jejich bylo jako tváří, kteréž jsem byl viděl u řeky Chebar, oblíčej jejich i oni sami. Jeden každý přímo k své straně chodil.
Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.

< Ezechiel 10 >