< Ámos 7 >

1 Toto mi ukázal Panovník Hospodin, že aj, formoval kobylky, když nejprvé počala růsti otava, když aj, otava byla po královském posečení.
Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
2 I stalo se, když snědly byliny zemské, že jsem řekl: Panovníče Hospodine, odpustiž, prosím. Kdož zůstane Jákobovi? Neboť ho maličko jest.
Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
3 I želel Hospodin toho. Nestaneť se, řekl Hospodin.
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
4 Tedy ukázal mi Panovník Hospodin, a aj, Panovník Hospodin volal, že při svou povede ohněm. A spáliv propast velikou, spálil i díl.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
5 Já pak řekl jsem: Panovníče Hospodine, přestaniž, prosím. Kdož zůstane Jákobovi? Neboť ho maličko jest.
Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
6 I želel Hospodin toho. A ani toho se nestane, řekl Panovník Hospodin.
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
7 Potom ukázal mi, a aj, Pán stál na zdi podlé pravidla vzdělané, v jehož ruce bylo pravidlo.
Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
8 I řekl mi Hospodin: Co vidíš, Amose? Řekl jsem: Pravidlo. I řekl Pán: Aj, já položím pravidlo u prostřed lidu svého Izraelského, nebuduť již více promíjeti jemu.
Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
9 Nebo zpuštěny budou výsosti Izákovy, a svatyně Izraelovy zpustnou, tehdáž, když povstanu proti domu Jeroboámovu s mečem.
“Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
10 Tedy poslal Amaziáš kněz Bethelský k Jeroboámovi králi Izraelskému, řka: Spuntoval se proti tobě Amos u prostřed domu Izraelského, ta země nemohla by snésti všech slov jeho.
Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
11 Nebo takto praví Amos: Od meče umře Jeroboám, a Izrael jistotně přestěhován bude z země své.
Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
12 Potom řekl Amaziáš Amosovi: Ó vidoucí, ujdi, radímť, utec do země Judské, a jez tam chléb, a tam prorokuj.
Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
13 Ale v Bethel již více neprorokuj, nebo ono svatyně králova i dům královský jest.
Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
14 Tedy odpovídaje Amos, řekl Amaziášovi: Nebylť jsem já prorokem, ano ani synem prorockým, ale byl jsem skotákem, a česával jsem plané fíky.
Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
15 Ale Hospodin mne vzal, když jsem chodil za stádem, a řekl mi Hospodin: Jdi, prorokuj lidu mému Izraelskému.
Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
16 Nyní tedy slyšiž slovo Hospodinovo. Ty pravíš: Neprorokuj v Izraeli, a nekaž v domě Izákově.
Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
17 Protož takto praví Hospodin: Žena tvá cizoložiti bude v městě, synové pak tvoji i dcery tvé od meče padnou; a země tvá provazcem dělena bude, a ty v zemi nečisté umřeš, Izrael pak jistotně přestěhován bude z země své.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”

< Ámos 7 >