< 2 Královská 24 >
1 Za dnů jeho přitáhl Nabuchodonozor král Babylonský, i učiněn jest Joakim služebníkem jeho za tři léta. Potom odvrátiv se, zprotivil se jemu.
Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
2 Protož poslal Hospodin na něj lotříky Kaldejské a lotříky Syrské, i lotříky Moábské a lotříky synů Ammon, poslal je, pravím, na Judu, aby ho zkazili vedlé řeči Hospodinovy, kterouž byl mluvil skrze služebníky své proroky.
Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
3 A jistě podlé řeči Hospodinovy to se dálo proti Judovi, aby jej zavrhl od tváři své pro hříchy Manassesovy, vedlé toho všeho, což byl činil,
Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
4 Ano i pro krev nevinnou, kterouž vylil, naplniv Jeruzalém krví nevinnou, čehož nechtěl Hospodin prominouti.
ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
5 O jiných pak věcech Joakimových, a cožkoli činil, psáno jest v knize o králích Judských.
Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
6 A tak usnul Joakim s otci svými, a kraloval Joachin syn jeho místo něho.
Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 Král pak Egyptský nikdy více nevytáhl z země své; nebo král Babylonský pobral od řeky Egyptské až k řece Eufraten všecko, cožkoli měl král Egyptský.
Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
8 V osmnácti letech byl Joachin, když počal kralovati, a tři měsíce kraloval v Jeruzalémě. Jméno matky jeho Nechusta, dcera Elnatanova z Jeruzaléma.
Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
9 I činil to, což jest zlého před očima Hospodinovýma, všecko tak, jakž byl činil otec jeho.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
10 Toho času vytáhli služebníci Nabuchodonozora krále Babylonského proti Jeruzalému, a obleženo jest město.
Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
11 Ano i Nabuchodonozor král Babylonský přitáhl proti městu, když služebníci jeho leželi vůkol něho.
Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
12 Tedy vyšel Joachin král Judský k králi Babylonskému, i s matkou svou i s služebníky, knížaty i komorníky svými, kteréhož vzal král Babylonský léta osmého kralování svého.
Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
13 A vynesl odtud všecky poklady domu Hospodinova, a poklady domu královského, a ztloukl všecky nádoby zlaté, jichž byl nadělal Šalomoun král Izraelský do domu Hospodinova, jakož byl mluvil Hospodin.
Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
14 Při tom přenesl všecken Jeruzalém a všecka knížata i všecky muže udatné, deset tisíců zajatých, i všecky tesaře a kováře. Žádného nezanechal, kromě chaterných lidí země.
Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
15 Zavedl také i Joachina do Babylona, a matku jeho i ženy královské i komorníky jeho; silné také země zavedl do vězení z Jeruzaléma do Babylona.
Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
16 Všech také mužů udatných sedm tisíců, tesařů také a kovářů tisíc, všecky též zmužilé bojovníky zavedl jaté král Babylonský do Babylona.
Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
17 Ustanovil pak král Babylonský Mataniáše, strýce jeho, králem místo něho, a změnil mu jméno, aby sloul Sedechiáš.
Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
18 V jedenmecítma letech byl Sedechiáš, když počal kralovati a jedenácte let kraloval v Jeruzalémě. Jméno matky jeho bylo Chamutal, dcera Jeremiášova z Lebna.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
19 I činil to, což jest zlého před očima Hospodinovýma, všecko tak, jakž byl dělal Joakim.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
20 Nebo se to dálo pro rozhněvání Hospodinovo proti Jeruzalému a Judovi, až je i zavrhl od tváři své. V tom opět zprotivil se Sedechiáš králi Babylonskému.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.