< 2 Korintským 3 >
1 Začínáme opět sami sebe chváliti? Zdaliž potřebujeme, jako někteří, schvalujících listů k vám, neb od vás k jiným?
Je, tumeanza kujisifia wenyewe tena? Hatuhitaji barua ya mapendekezo kwenu au kutoka kwenu, kama baadhi ya watu, je twahitaji?
2 List náš vy jste, napsaný v srdcích našich, kterýž znají a čtou všickni lidé.
Ninyi wenyewe ni barua yetu ya mapendekezo, iliyoandikwa kwenye mioyo yetu, inayojulikana na kusomwa na watu wote.
3 Nebo to zjevné jest, že jste list Kristův způsobený skrze přisluhování naše, napsaný ne černidlem, ale Duchem Boha živého, ne na dskách kamenných, ale na dskách srdce masitých.
Na mnaonesha kwamba ninyi ni barua kutoka kwa Kristo, iliyotolewa na sisi. Iliandikwa siyo kwa wino bali kwa Roho wa Mungu aliye hai. Haikuandikwa juu ya vibao vya mawe, bali juu ya vibao vya mioyo ya wanadamu.
4 Doufání pak takové máme skrze Krista k Bohu,
Na huu ndiyo ujasiri tulio nao katika Mungu kupitia Kristo.
5 Ne že bychom dostateční byli mysliti něco sami z sebe, jakožto sami z sebe, ale dostatečnost naše z Boha jest.
Hatujiamini wenyewe kwa kudai chochote kama kutoka kwetu. Badala yake, kujiamini kwetu kunatoka kwa Mungu.
6 Kterýž i hodné nás učinil služebníky Nového Zákona, ne litery, ale Ducha. Nebo litera zabijí, ale Duch obživuje.
Ni Mungu ambaye alitufanya tuweze kuwa watumishi wa agano jipya. Hili ni agano sio la barua bali ni la Roho. Kwa kuwa barua huua, lakini roho inatoa uhai.
7 Jestližeť pak přisluhování smrti, literami vyryté na dskách kamenných, bylo slavné, tak že nemohli patřiti synové Izraelští v tvář Mojžíšovu, pro slávu oblíčeje jeho, kteráž pominouti měla,
Sasa kazi ya kifo iliyokuwa imechongwa katika herufi juu ya mawe ilikuja kwa namna ya utukufu kwamba watu wa Israeli hawakuangalia moja kwa moja kwenye uso wa Musa. Hii ni kwa sababu ya utukufu wa uso wake, utukufu ambao ulikuwa unafifia.
8 I kterakž by ovšem přisluhování Ducha nemělo býti slavné?
Je, kazi ya Roho haitakuwa na utukufu zaidi?
9 Nebo jestližeť přisluhování pomsty slavné bylo, mnohemť se více přisluhování spravedlnosti rozhojňuje v slávě.
Kwa kuwa kama huduma ya hukumu ilikuwa na utukufu, ni mara ngapi zaidi huduma ya haki huzidi sana katika utukufu!
10 Nebo to, což oslaveno bylo, aniž oslaveno bylo v té částce, u přirovnání této předůstojné slávy.
Ni kweli kwamba, kile kilichofanywa utukufu kwanza hakina utukufu tena katika heshima hii, kwa sababu ya utukufu unaouzidi.
11 Nebo jestližeť to pomíjející bylo slavné, mnohemť více to, což zůstává, jestiť slavné.
Kwa kuwa kama kile ambacho kilikuwa kinapita kilikuwa na utukufu, ni kwa kiasi gani zaidi kile ambacho ni cha kudumu kitakuwa na utukufu!
12 Protož majíce takovou naději, mnohé svobody v mluvení užíváme,
Kwa kuwa tunajiamini hiyo, tunaujasiri sana.
13 A ne jako Mojžíš kladl zástěru na tvář svou, aby nepatřili synové Izraelští k cíli té věci pomíjející.
Hatuko kama Musa, aliyeweka utaji juu ya uso wake, ili kwamba watu wa Israel wasiweze kuangalia moja kwa moja kwenye mwisho wa utukufu ambao ulikuwa unatoweka.
14 Pročež ztupeni jsou smyslové jejich. Nebo až do dnes ta zástěra v čítání Starého Zákona zůstává neodkrytá; nebo skrze Krista se odnímá.
Lakini fahamu zao zilikuwa zimefungwa. Hata mpaka siku hii utaji uleule bado unabaki juu ya usomaji wa agano la kale. Haijawekwa wazi, kwa sababu ni katika Kristo pekee inaondolewa mbali.
15 Protož až do dnes, když čten bývá Mojžíš, zástěra jest položena na jejich srdci.
Lakini hata leo, wakati wowote Musa asomwapo, utaji hukaa juu ya mioyo yao.
16 Než jakž by se obrátilo ku Pánu, odňata bude ta zástěra.
Lakini mtu anapogeuka kwa Bwana, utaji unaondolewa.
17 Nebo Pán jest Duch ten, a kdež jest ten Duch Páně, tu i svoboda.
Sasa Bwana ni Roho. Palipo na Roho wa Bwana, kuna uhuru.
18 My pak všickni odkrytou tváří slávu Páně jako v zrcadle spatřujíce, v týž obraz proměněni býváme od slávy v slávu, jakožto od Ducha Páně.
Sasa sisi sote, pamoja na nyuso zisizo wekewa utaji, huona utukufu wa Bwana. Tunabadilishwa ndani ya muonekano uleule wa utukufu kutoka shahada moja ya utukufu kwenda nyingine, kama ilivyo kutoka kwa Bwana, ambaye ni Roho.