< 1 Samuelova 8 >
1 Když se pak zstaral Samuel, ustanovil syny své za soudce v Izraeli.
Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
2 A bylo jméno syna jeho prvorozeného Joel, a jméno druhého Abia; ti byli soudcové v Bersabé.
Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
3 Nechodili pak synové jeho po cestách jeho, ale uchýlili se po lakomství, a berouce dary, převraceli soud.
Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
4 Shromáždili se tedy všickni starší Izraelští, a přišli k Samuelovi do Ramata.
Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
5 A řekli jemu: Aj, tys se již zstaral, a synové tvoji nechodí po cestách tvých; protož nyní ustanov nám krále, aby soudil nás, jakož jest u všech národů.
Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
6 I nelíbila se ta řeč Samuelovi, že řekli: Dej nám krále, aby nás soudil. Protož modlil se Samuel Hospodinu.
Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.
7 Tedy řekl Hospodin Samuelovi: Uposlechni hlasu lidu ve všem, což mluví tobě; nebo ne tebouť jsou pohrdli, ale mnou pohrdli, abych nekraloval nad nimi.
Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.
8 Podlé všech skutků těch, kteréž činili od onoho dne, v němž jsem je vyvedl z Egypta až do tohoto dne, kdyžto opustili mne, a sloužili bohům cizím, takť oni činí i tobě.
Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.
9 Protož nyní uposlechni hlasu jejich, a však nejprv osvědč pilně před nimi, a oznam jim obyčej krále, kterýž nad nimi kralovati bude.
Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”
10 I mluvil Samuel všecky řeči Hospodinovy k lidu, kteříž krále žádali od něho.
Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.
11 A řekl: Tento bude obyčej krále, kterýž kralovati bude nad vámi: Bráti bude syny vaše, a dá je k vozům svým, a zdělá sobě z nich jezdce, a běhati budou před vozem jeho.
Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.
12 Také ustanoví je sobě za hejtmany nad tisíci a za padesátníky, a aby jemu orali rolí jeho, a žali obilé jeho, též aby jemu dělali nástroje válečné a přípravy k vozům jeho.
Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.
13 Dcery také vaše bráti bude, aby dělaly masti, a byly kuchařky a pekařky.
Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.
14 Nadto pole vaše a vinice vaše, i olivoví vaše nejvýbornější pobéře a rozdá služebníkům svým.
Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
15 Také z toho, což vsejete, a z vinic vašich desátky bráti bude, a dá komorníkům a služebníkům svým.
Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.
16 Též služebníky vaše a děvky vaše, a mládence vaše nejzpůsobnější, i osly vaše vezme, aby jimi dělal dílo své.
Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.
17 Z stád vašich desátky bráti bude, a vy budete jemu za služebníky.
Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.
18 I budete volati v ten den příčinou krále vašeho, kteréhož byste sobě vyvolili, a nevyslyší vás Hospodin dne toho.
Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”
19 Nechtěl však lid uposlechnouti řeči Samuelovy, a řekli: Nikoli, ale král bude nad námi,
Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala.
20 Abychom i my také byli, jako všickni jiní národové, a souditi nás bude král náš, a vycházeje před námi, bojovati bude za nás.
Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”
21 Vyslyšev tedy Samuel všecka slova lidu, oznámil je Hospodinu.
Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana.
22 I řekl Hospodin Samuelovi: Uposlechni hlasu jejich, a ustanov jim krále. Protož řekl Samuel mužům Izraelským: Jdětež jeden každý do města svého.
Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.” Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”