< 1 Korintským 14 >
1 Stůjtež o lásku, horlivě žádejte duchovních věcí, nejvíce však, abyste prorokovali.
Jitahidini kuwa na upendo. Vilevile fanyeni bidii ya kupata vipaji vingine vya kiroho, hasa kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu.
2 Nebo ten, kdož mluví cizím jazykem, ne lidem mluví, ale Bohu; nebo žádný neposlouchá, ale duchem vypravuje tajemství.
Mwenye kunena lugha ngeni hasemi na watu bali anasema na Mungu. Yeye hunena kwa nguvu ya Roho mambo yaliyofichika.
3 Kdož pak prorokuje, lidem mluví vzdělání, i napomínání, i potěšení.
Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, husema na watu kwa ajili ya kuwajenga, kuwafariji na kuwatia moyo.
4 Kdož mluví cizím jazykem, sám sebe vzdělává, ale ten, kdož prorokuje, církev vzdělává.
Mwenye kunena lugha ngeni anajijenga mwenyewe. Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, analijenga kanisa.
5 Chtělť bych pak, abyste všickni jazyky mluvili, ale však raději, abyste prorokovali. Nebo větší jest ten, kterýž prorokuje, nežli ten, kdož jazyky mluví, leč by také vykládal, aby se vzdělávala církev.
Basi, ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha ngeni lakini ningependelea hasa muwe na kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, maana mtu mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, ni wa maana zaidi kuliko yule mwenye kusema lugha ngeni, isipokuwa tu kama yupo hapo mtu awezaye kuyafafanua hayo mambo asemayo, ili kanisa lipate kujengwa.
6 A protož, bratří, přišel-li bych k vám, jazyky mluvě, což vám prospěji, nebudu-liť vám mluviti, buď v zjevení neb v umění, buď v proroctví neb v učení?
Hivyo, ndugu zangu, kama nikija kwenu na kusema nanyi kwa lugha ngeni itawafaa nini? Haitawafaa chochote, isipokuwa tu kama nitawaelezeni ufunuo wa Mungu au ujuzi fulani au ujumbe wa Mungu au mafundisho fulani.
7 Však i bezdušné věci, vydávající zvuk, jako píšťalka neb harfa, kdyby rozdílného zvuku nevydávaly, kterak by vědíno bylo, co se píská, aneb na harfu hrá?
Ndivyo ilivyo kwa vyombo visivyo na uhai vyenye kutoa sauti kama vile filimbi au kinanda. Je, mtu anawezaje kuutambua wimbo unaochezwa kama vyombo hivyo havitoi sauti waziwazi vinapopigwa?
8 Ano trouba vydala-li by nejistý hlas, kdož se bude strojiti k boji?
La mgambo likilia bila kufuata taratibu zake, nani atajiweka tayari kwa vita?
9 Tak i vy, nevydali-li byste jazykem srozumitelných slov, kterak bude rozumíno, co se mluví? Budete jen u vítr mluviti.
Hali kadhalika na ninyi, kama ulimi wenu hausemi kitu chenye kueleweka, nani ataweza kufahamu mnayosema? Maneno yenu yatapotea hewani.
10 Tak mnoho, (jakž vidíme, ) rozdílů hlasů jest na světě, a nic není bez hlasu.
Zipo lugha mbalimbali ulimwenguni, na hakuna hata mojawapo isiyo na maana.
11 Protož nebudu-liť znáti moci hlasu, budu tomu, kterýž mluví, cizozemec, a ten, kdož mluví, bude mi cizozemec.
Lakini ikiwa mimi sifahamu maana ya lugha asemayo mtu fulani, mimi ni mgeni kwake mtu huyo naye pia ni mgeni kwangu.
12 Tak i vy, poněvadž jste horliví milovníci duchovních věcí, toho hledejte, abyste se k vzdělání církve rozhojnili.
Hali kadhalika na ninyi, maadam mna hamu ya kupata vipaji vya Roho, jitahidini hasa kujipatia vile vinavyosaidia kulijenga kanisa.
13 A protož, kdož mluví jazykem, modl se, aby mohl vykládati.
Kwa hiyo, mwenye kunena lugha ngeni na aombe apate uwezo wa kuzifafanua.
14 Nebo modlím-liť se jazykem, duch můj se modlí, ale mysl má bez užitku jest.
Maana, nikisali kwa lugha ngeni roho yangu ndiyo inayosali, lakini akili yangu hubaki bure.
15 Což tedy jest? Modliti se budu duchem a modliti se budu i myslí; plésati budu duchem, a plésati budu i myslí.
Nifanye nini, basi? Nitasali kwa roho yangu, nitasali pia kwa akili yangu; nitaimba kwa roho yangu, nitaimba pia kwa akili yangu.
16 Nebo kdybys dobrořečil duchem, kterakž ten, kterýž prostý člověk jest, k tvému díků činění řekne Amen, poněvadž neví, co pravíš?
Ukimsifu Mungu kwa roho yako tu, atawezaje mtu wa kawaida aliye katika mkutano kuitikia sala yako ya shukrani kwa kusema: “Amina,” kama haelewi unachosema?
17 Nebo ač ty dobře díky činíš, ale jiný se nevzdělává.
Sala yako ya shukrani yaweza kweli kuwa bora, lakini huyo mwingine haitamfaidia.
18 Děkuji Bohu svému, že více než vy všickni jazyky mluvím;
Namshukuru Mungu kwamba mimi nasema kwa lugha ngeni zaidi kuliko ninyi nyote.
19 Ale v zboru raději bych chtěl pět slov srozumitelně promluviti, abych také jiných poučil, nežli deset tisíců slov jazykem.
Lakini katika mikutano ya waumini napendelea zaidi kusema maneno matano yenye kueleweka ili niwafundishe wengine, kuliko kusema maneno elfu ya lugha ngeni.
20 Bratří, nebuďte děti v smyslu, ale zlostí buďte děti, smyslem pak buďte dospělí.
Ndugu, msiwe kama watoto katika fikira zenu. Kuhusu uovu muwe kama watoto wachanga lakini katika kufikiri ni lazima muwe kama watu waliokomaa.
21 Psáno jest v zákoně: Protož rozličnými jazyky a cizími rty budu mluviti lidu tomuto, a aniž tak mne slyšeti budou, praví Pán.
Imeandikwa katika Sheria: “Bwana asema hivi: Kwa njia ya wenye kunena lugha ngeni, na kwa midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, hata hivyo, hawatanisikiliza.”
22 A tak jazykové jsou za div ne těm, kteříž věří, ale nevěřícím, proroctví pak ne nevěřícím, ale věřícím.
Hivyo basi, kipaji cha kusema lugha ngeni ni ishara, si kwa ajili ya watu wenye imani, bali kwa ajili ya wale wasioamini; lakini kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni kwa ajili ya wale wanaoamini na si kwa ajili ya wasioamini.
23 A protož když by se sešla všecka církev spolu, a všickni by jazyky mluvili, a vešli by tam i neučení neb nevěřící, zdaliž neřeknou, že blázníte?
Basi, kanisa lote linapokutana pamoja, na wote wakaanza kusema kwa lugha ngeni, kama wakija watu wa kawaida au wasioamini, je, hawatasema kwamba ninyi mna wazimu?
24 Ale kdyby všickni prorokovali, a všel by někdo nevěřící neb neučený, přemáhán by byl ode všech, a souzen ode všech.
Lakini, wote wakiwa wanautangaza ujumbe wa Mungu, akija mtu wa kawaida au asiyeamini, yote atakayosikia yatamhakikishia ubaya wake mwenyewe; yote atakayosikia yatamhukumu.
25 A tak tajnosti srdce jeho zjeveny budou, a padna na tvář, klaněti se bude Bohu, vyznávaje, že jistě Bůh jest mezi vámi.
Siri za moyo wake zitafichuliwa, naye atapiga magoti na kumwabudu Mungu akisema: “Kweli Mungu yupo pamoja nanyi.”
26 Což tedy, bratří? Když se scházíte, jeden každý z vás píseň má, učení má, jazyk má, zjevení má, vykládání má, všecko to budiž k vzdělání.
Ndugu, tuseme nini, basi? Mnapokutana pamoja, mmoja aimbe wimbo, mwingine atoe mafundisho, mwingine awe na ufunuo kutoka kwa Mungu, mwingine atumie kipaji cha kusema kwa lugha ngeni na mwingine afafanue yanayosemwa. Yote yawe kwa ajili ya kulijenga kanisa.
27 Buď že kdo jazykem mluví, tedy skrze dva neb nejvíce tři, a to jeden po druhém, a jeden ať vykládá.
Wakiwepo watu wenye vipaji vya kusema kwa lugha ngeni, waseme wawili au watatu, si zaidi, tena mmojammoja; na aweko mtu wa kufafanua yanayosemwa.
28 Pakli by nebylo vykladače, nechť mlčí v shromáždění, sám pak sobě nechažť mluví a Bohu.
Lakini kama hakuna awezaye kufafanua, basi, mwenye kusema lugha ngeni anyamaze mkutanoni, aseme na nafsi yake mwenyewe na Mungu.
29 Proroci pak dva neb tři ať mluví, a jiní nechť rozsuzují.
Kuhusu wale wenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, waseme wawili au watatu, na wengine wayapime maneno yao.
30 Pakliť by jinému tu přísedícímu zjeveno bylo, první mlč.
Ikiwa mmoja anaposema mwingine wa wasikilizaji amepata ufunuo kutoka kwa Mungu, basi, yule anayesema anyamaze.
31 Nebo můžete všickni, jeden po druhém, prorokovati, aby se všickni učili, a všickni se potěšovali.
Maana nyote mwaweza kutangaza ujumbe wa Mungu, mmoja baada ya mwingine, ili nyote mpate kujifunza na kutiwa moyo.
32 Duchovéť pak proroků prorokům poddání jsou.
Kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni lazima kitawaliwe na huyo mwenye hicho kipaji.
33 Neboť Bůh není původ neřádu, ale pokoje, jako i ve všech shromážděních svatých.
Maana Mungu si Mungu wa fujo, ila wa amani.
34 Ženy vaše v shromážděních ať mlčí, nebo nedopouští se jim mluviti, ale aby poddány byly, jakž i zákon praví.
Kama ilivyo desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu, wanawake wakae kimya katika mikutano ya waumini. Hawana ruhusa kusema; ila wawe watii kama isemavyo Sheria.
35 Pakli se chtí čemu naučiti, doma mužů svých nechať se ptají. Nebo mrzká věc jest ženám mluviti v shromáždění.
Ikiwa wanayo maswali ya kuuliza, wawaulize waume zao nyumbani, maana ni aibu kwa mwanamke kusema katika mikutano ya waumini.
36 Zdali od vás slovo Boží pošlo? Zdali k samým vám přišlo?
Je, mnadhani neno la Mungu limetoka kwenu ninyi au kwamba limewajieni ninyi peke yenu?
37 Zdá-li se sobě kdo býti prorokem neb duchovním, nechažť pozná, co vám píši, žeť jsou přikázaní Páně.
Kama mtu yeyote anadhani kwamba yeye ni mjumbe wa Mungu au kwamba anacho kipaji cha Roho, na ajue kwamba haya ninayowaandikia ninyi ni amri ya Bwana.
38 Pakli kdo neví, nevěz.
Lakini mtu asiyetambua hayo, basi, mtu asimjali mtu huyo.
39 A takž, bratří, snažte se o to, abyste prorokovali, a jazyky mluviti nezbraňujte.
Hivyo basi, ndugu zangu, mnapaswa kuwa na hamu ya kutangaza ujumbe wa Mungu; lakini msimkataze mtu kusema kwa lugha ngeni.
40 Všecko slušně a podlé řádu ať se děje.
Lakini yote yafanyike kwa heshima na kwa utaratibu.