< 1 Kronická 24 >

1 Synů pak Aronových tato jsou zpořádaní: Synové Aronovi: Nádab, Abiu, Eleazar a Itamar.
Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Ale že umřel Nádab a Abiu před otcem svým, a neměli synů, protož konali úřad kněžský Eleazar a Itamar.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
3 Kteréž zpořádal David, totiž Sádocha z synů Eleazarových, a Achimelecha z synů Itamarových, vedlé počtu a řádu jejich v přisluhováních jejich.
Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
4 Nalezeno pak synů Eleazarových více předních mužů, než synů Itamarových, a rozdělili je. Z synů Eleazarových bylo předních po domích otcovských šestnáct, a z synů Itamarových po čeledech otcovských osm.
Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
5 I rozděleni jsou losem jedni od druhých, ačkoli byli knížata nad věcmi svatými, a knížata Boží z synů Eleazarových a z synů Itamarových.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
6 I popsal je Semaiáš syn Natanaelův, písař z pokolení Léví před králem a knížaty, a Sádochem knězem a Achimelechem synem Abiatarovým i knížaty čeledí otcovských mezi kněžími a Levíty, tak že dům otcovský jeden zaznamenán Eleazarovi, tolikéž druhý zaznamenán Itamarovi.
Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
7 Padl pak los první na Jehoiariba, na Jedaiáše druhý,
Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
8 Na Charima třetí, na Seorima čtvrtý,
ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
9 Na Malkiáše pátý, na Miamin šestý,
ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
10 Na Hakkoza sedmý, na Abiáše osmý,
ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
11 Na Jesua devátý, na Sechaniáše desátý,
ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
12 Na Eliasiba jedenáctý, na Jakima dvanáctý,
ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
13 Na Chuppa třináctý, na Jesebaba čtrnáctý,
ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
14 Na Bilgu patnáctý, na Immera šestnáctý,
ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
15 Na Chezira sedmnáctý, na Happizeza osmnáctý,
ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
16 Na Petachiáše devatenáctý, na Ezechiele dvadcátý,
ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
17 Na Jachina jedenmecítmý, na Gamule dvamecítmý,
ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
18 Na Delaiáše třimecítmý, na Maaseiáše čtyřmecítmý.
ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
19 Ti jsou, jenž zřízeni byli v přisluhováních svých, aby vcházeli do domu Hospodinova podlé řádu svého, pod spravou Arona otce jejich, jakož mu byl přikázal Hospodin Bůh Izraelský.
Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
20 Z synů Léví ostatních, z synů Amramových Subael, z synů Subael Jechdeiáš.
Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
21 Z Rechabiáše, z synů Rechabiášových kníže Iziáš.
Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
22 Z Izara Selomot, z synů Selomotových Jachat.
Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
23 Synové pak Jeriášovi: Amariáš druhý, Jachaziel třetí, Jekamam čtvrtý.
Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
24 Syn Uzielův Mícha, z synů Míchy Samir.
Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
25 Bratr Míchův Iziáš, a syn Iziášův Zachariáš.
Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
26 Synové Merari: Moholi a Musi, synové Jaaziášovi: Beno.
Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
27 Synové Merari z Jaaziáše: Beno, Soham, Zakur a Ibri.
Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
28 Z Moholi Eleazar, kterýž neměl synů.
Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
29 Z Cisa synové Cisovi: Jerachmeel.
Wana wa Kishi: Yerameli
30 Synové pak Musi: Moholi, Eder a Jerimot. Ti jsou synové Levítů po domích otců svých.
wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
31 I ti také metali losy naproti bratřím svým, synům Aronovým, před Davidem králem, Sádochem a Achimelechem, i knížaty otcovských čeledí z kněží a Levítů, z čeledí otcovských, každý přednější naproti bratru svému mladšímu.
Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.

< 1 Kronická 24 >