< Zaharija 14 >
1 Gle, dolazi dan Jahvin kada će se podijeliti plijen usred tebe.
Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.
2 I sabrat ću sve narode u Jeruzalem u borbu. I zaposjest će grad, opljačkati kuće i silovati žene. Polovina će grada otići u izgnanstvo, ali Ostatak neće biti istrijebljen iz grada.
Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.
3 Tada će Jahve izaći i boriti se protiv tih naroda kako on zna ratovati u dan ratni.
Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita.
4 Noge će mu, u dan onaj, stajati na Gori maslinskoj koja je nasuprot Jeruzalemu na istoku. I raskolit će se Gora maslinska po srijedi, između istoka i zapada, u golemu dolinu: jedna će se polovina pomaknuti na sjever, druga na jug.
Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
5 Dolina Gore moje bit će ispunjena od Goe pa do Jasola i bit će zakrčena kao što je bila zakrčena poslije potresa u dane Uzije, kralja judejskog. Tada će doći Jahve, Bog tvoj, i svi sveci s njim.
Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.
6 U dan onaj neće više biti ni studeni ni leda.
Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji.
7 Bit će to dan čudesan - znade ga Jahve - ni dan ni noć; i u vrijeme večeribit će svjetlo.
Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.
8 U onaj dan žive će vode poteći iz Jeruzalema, pola k moru istočnom, pola kmoru zapadnom. Bit će tako ljeti i zimi.
Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika.
9 I Jahve će biti kralj nad svom zemljom.
Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.
10 Sva će se zemlja pretvoriti u ravnicu, od Gebe do Rimona negepskog. A Jeruzalem će se uzvisiti na svom mjestu; i bit će nastanjen - od Vrata Benjaminovih do Prvih vrata, to jest do Vrata ugaonih, i od Kule Hananeelove do Kraljeva tijeska.
Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme.
11 Opet će se stanovati u njemu, i više neće biti prokletstva; Jeruzalem će živjeti u miru.
Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.
12 A evo kojom će ranom Jahve udariti sve narode koji budu zavojštili na Jeruzalem: meso će im se raspadati dok budu na nogama; oči će im trunuti u dupljama, jezik gnjiti u ustima.
Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.
13 U dan onaj nastat će među njima silan metež od Jahve: jedan će drugoga za ruku hvatati, i ruka će se jednoga dizati na drugoga.
Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana.
14 I Juda će se boriti u Jeruzalemu. Tu će se sakupiti bogatstva svih okolnih naroda: zlato, srebro, odjeća u velikoj množini.
Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo.
15 A slična će rana pasti na konje, mazge, deve i magarce, i na svu stoku koja se nađe u tome taboru.
Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.
16 Tko preživi od svih naroda koji dođu na Jeruzalem, uzlazit će godimice da se pokloni pred Kraljem, Jahvom nad Vojskama, i da slave Blagdan sjenica.
Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
17 Ako koje pleme zemlje ne uzađe u Jeruzalem da se pokloni pred Kraljem, Jahvom nad Vojskama, neće biti kiše za njega.
Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao.
18 Ako li pleme egipatsko ne uzađe i ne dođe, stići će ga isti udarac kojim će Jahve udariti narode koji ne bi uzašli svetkovati Blagdan sjenica.
Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
19 Takva će biti kazna Egiptu i svim narodima koji ne budu uzašli da svetkuju Blagdan sjenica.
Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
20 U onaj dan stajat će na konjskim praporcima 'Jahvi posvećen'; a u Domu Jahvinu bit će lonci kao žrtvene čaše pred žrtvenikom;
Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu.
21 i svaki će lonac u Jeruzalemu i u Judeji biti posvećen Jahvi nad Vojskama - svi koji budu htjeli žrtvovati uzimat će ih i kuhati u njima. I u dan onaj neće više biti trgovaca u Domu Jahve nad Vojskama.
Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.