< Rimljanima 16 >
1 Preporučujem vam Febu, sestru našu, poslužiteljicu Crkve u Kenhreji:
Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2 primite je u Gospodinu kako dolikuje svetima i priskočite joj u pomoć u svemu što od vas ustreba jer je i ona bila zaštitnicom mnogima i meni samomu.
Naomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.
3 Pozdravite Prisku i Akvilu, suradnike moje u Kristu Isusu.
Wasalimuni Prisila na Akila, watumishi wenzangu katika Kristo Yesu.
4 Oni su za moj život podmetnuli svoj vrat; zahvaljujem im ne samo ja nego i sve Crkve pogana.
Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa.
5 Pozdravite i Crkvu u njihovoj kući. Pozdravite ljubljenog mi Epeneta koji je prvina Azije za Krista.
Lisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Kristo huko Asia.
6 Pozdravite Mariju koja se mnogo trudila za vas.
Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7 Pozdravite Andronika i Juniju, rođake i suuznike moje; oni su ugledni među apostolima i prije mene bili su u Kristu.
Wasalimuni Androniko na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, nao walikuwa katika Kristo kabla yangu.
8 Pozdravite Amplijata, ljubljenoga moga u Gospodinu.
Msalimuni Ampliato, yeye nimpendaye katika Bwana.
9 Pozdravite Urbana, suradnika moga u Kristu, i ljubljenog mi Staha.
Msalimuni Urbano, mtendakazi mwenzetu katika Kristo, pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi.
10 Pozdravite Apela, prokušanoga u Kristu. Pozdravite Aristobulove.
Msalimuni Apele aliyejaribiwa na akaithibitisha imani yake katika Kristo. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11 Pozdravite Herodiona, rođaka moga. Pozdravite Narcisove koji su u Gospodinu.
Msalimuni ndugu yangu Herodioni. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Narkisi walio katika Bwana.
12 Pozdravite Trifenu i Trifozu koje se trude u Gospodinu. Pozdravite ljubljenu Persidu koja se mnogo trudila u Gospodinu.
Wasalimuni Trifaina na Trifosa, wale wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Persisi, mwanamke mwingine aliyefanya kazi kwa bidii katika Bwana.
13 Pozdravite Rufa, izabranika u Gospodinu, i majku njegovu i moju.
Msalimuni Rufo, mteule katika Bwana, pamoja na mama yake, ambaye amekuwa mama kwangu pia.
14 Pozdravite Asinkrita, Flegonta, Herma, Patrobu, Hermu i braću koja su s njima.
Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15 Pozdravite Filologa i Juliju, Nereja i njegovu sestru, i Olimpu, i sve svete koji su s njima.
Wasalimuni Filologo, Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watakatifu wote walio pamoja nao.
16 Pozdravite jedni druge cjelovom svetim. Pozdravljaju vas sve Crkve Kristove.
Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.
17 Zaklinjem vas, braćo, čuvajte se onih koji siju razdore i sablazni mimo nauk u kojem ste poučeni, i klonite ih se.
Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na kujiepusha na wale watu waletao matengano na kuweka vikwazo mbele yenu dhidi ya mafundisho mliyojifunza.
18 Jer takvi ne služe Gospodinu našemu Kristu, nego svom trbuhu te lijepim i laskavim riječima zavode srca nedužnih.
Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno laini na ya kubembeleza, hupotosha mioyo ya watu wajinga.
19 Doista, vaša je poslušnost doprla do sviju. Zbog vas se dakle radujem i htio bih da budete mudri za dobro, a bezazleni za zlo.
Kila mtu amesikia juu ya utii wenu, nami nimejawa na furaha tele kwa ajili yenu. Lakini nataka mwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu.
20 Bog mira satrt će ubrzo Sotonu pod vašim nogama. Milost Gospodina Isusa s vama!
Mungu wa amani atamponda Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu iwe nanyi. Amen.
21 Pozdravlja vas Timotej, suradnik moj, i Lucije, Jason i Sosipater, rođaci moji.
Timotheo, mtendakazi mwenzangu anawasalimu. Vivyo hivyo Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu.
22 Pozdravljam vas u Gospodinu ja, Tercije, koji napisah ovu poslanicu.
Mimi, Tertio, niliye mwandishi wa waraka huu, nawasalimu katika Bwana.
23 Pozdravlja vas Gaj, gostoprimac moj i cijele Crkve. Pozdravlja vas Erast, gradski blagajnik, i brat Kvart.
Gayo, ambaye ni mwenyeji wangu na wa kanisa lote, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto ndugu yetu pia wanawasalimu. [
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amen.]
25 Onomu koji vas može učvrstiti - po mojem evanđelju i propovijedanju Isusa Krista, po objavljenju Otajstva prešućenog drevnim vremenima, (aiōnios )
Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. (aiōnios )
26 a sada očitovanog i po proročkim pismima odredbom vječnoga Boga svim narodima obznanjenog za poslušnost, vjeru - (aiōnios )
Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii (aiōnios )
27 jedinomu Mudromu, Bogu, po Isusu Kristu: Njemu slava u vijeke! Amen. (aiōn )
Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen. (aiōn )