< Rimljanima 14 >

1 Slaboga u vjeri prigrlite, ali ne da se prepirete o mišljenjima.
Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.
2 Netko vjeruje da smije sve jesti, slabi opet jede samo povrće.
Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.
3 Tko jede, neka ne prezire onoga tko ne jede; tko pak ne jede, neka ne sudi onoga tko jede. Ta Bog ga je prigrlio.
Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.
4 Tko si ti da sudiš tuđega slugu? Svojemu Gospodaru i stoji i pada! A stajat će jer moćan je Gospodin da ga podrži.
Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
5 Netko razlikuje dan od dana, nekomu je opet svaki dan jednak. Samo nek je svatko posve uvjeren u svoje mišljenje.
Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.
6 Tko na dan misli, poradi Gospodina misli; i tko jede, poradi Gospodina jede: zahvaljuje Bogu. I tko ne jede, poradi Gospodina ne jede i - zahvaljuje Bogu.
Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.
7 Jer nitko od nas sebi ne živi, nitko sebi ne umire.
Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe
8 Doista, ako živimo, Gospodinu živimo, i ako umiremo, Gospodinu umiremo. Živimo li dakle ili umiremo - Gospodinovi smo.
maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.
9 Ta Krist zato umrije i oživje da gospodar bude i mrtvima i živima.
Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.
10 A ti, što sudiš brata svoga? Ili ti, što prezireš brata svoga? Ta svi ćemo stati pred sudište Božje.
Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
11 Jer pisano je: Života mi moga, govori Gospodin, prignut će se preda mnom svako koljeno i svaki će jezik priznati Boga.
Maana Maandiko yanasema: “Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti, na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”
12 Svaki će dakle od nas za sebe Bogu dati račun.
Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja yake mbele ya Mungu.
13 Dakle, ne sudimo više jedan drugoga, nego radije sudite o tome da ne valja postavljati bratu stupice ili spoticala.
Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.
14 Znam i uvjeren sam u Gospodinu: ništa samo od sebe nije nečisto. Samo je onomu nečisto tko to smatra nečistim.
Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.
15 Doista, ako je poradi hrane tvoj brat ražalošćen, već nisi na putu ljubavi. Ne upropašćuj tom svojom hranom onoga za koga je Krist umro!
Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!
16 Nemojte da se pogrđuje vaše dobro!
Basi, msikubalie kitu mnachokiona kuwa kwenu ni kitu chema kidharauliwe.
17 Ta kraljevstvo Božje nije jelo ili piće, nego pravednost, mir i radost u Duhu Svetome.
Maana Utawala wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.
18 Da, tko tako Kristu služi, mio je Bogu i cijene ga ljudi.
Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.
19 Nastojmo stoga promicati mir i uzajamno izgrađivanje!
Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.
20 Ne razaraj djela Božjega poradi hrane! Sve je, istina, čisto, ali je zlo za onoga tko na sablazan jede.
Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.
21 Dobro je ne jesti mesa i ne piti vina i ne uzimati ništa o što se tvoj brat spotiče.
Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.
22 Ti imaš uvjerenje. Za sebe ga imaj pred Bogom. Blago onomu tko samoga sebe ne osuđuje u onom na što se odlučuje!
Basi, shikilia unachoamini kati yako na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.
23 Jede li tko dvoumeći, osudio se jer ne radi iz uvjerenja. A sve što nije iz uvjerenja, grijeh je.
Lakini mtu anayeona shaka juu ya chakula anachokula, anahukumiwa kama akila, kwa sababu msimamo wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho na msingi wake katika imani ni dhambi.

< Rimljanima 14 >