< Otkrivenje 19 >
1 Nakon toga začujem kao jak glas silnoga mnoštva na nebu: “Aleluja! Spasenje i slava i moć Bogu našemu!
Baada ya mambo haya nilisikia sauti kama ya mlio mkubwa wa kundi kubwa la watu mbinguni ikisema, “Haleluya. Wokovu, utukufu, na nguvu ni vya Mungu wetu.
2 Doista, istiniti su i pravedni sudovi njegovi jer osudi veliku Bludnicu, što pokvari zemlju bludom svojim, i osveti na njoj krv slugu svojih!”
Hukumu zake ni kweli na za haki, kwa kuwa amemhukumu kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uzinzi wake. Amefanya kisasi kwa damu ya watumishi wake, ambayo aliimwaga yeye mwenyewe.”
3 I ponove: “Aleluja! Dim njezin suklja u vijeke vjekova!” (aiōn )
Kwa mara ya pili walisema, “Haleluya! Moshi hutoka kwake milele na milele.” (aiōn )
4 Nato starješine, njih dvadesetčetvorica, i ona četiri bića padoše ničice i p okloniše se Bogu, koji sjedi na prijestolju, govoreći: “Amen! Aleluja!”
Wale wazee ishirini na wanne na viumbe hai wanne wakasujudu na kumwabudu Mungu akaaye kwenye kiti cha enzi. Walikuwa wakisema, “Amina. Haleluya!”
5 I s prijestolja iziđe glas: “Hvalite Boga našega, sve sluge njegove, svi koji se njega bojite, i mali i veliki!”
Ndipo sauti ilitoka kwenye kiti cha enzi, ikisema, “Msifuni Mungu wetu, enyi watumishi wake wote, ninyi mnaomcha yeye, wote wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
6 I začuh kao glas silna mnoštva i kao šum voda mnogih i kao prasak gromova silnih: “Aleluja! Zakraljeva Gospod, Bog naš Svevladar!
Ndipo nilisikia sauti kama sauti ya kundi kubwa la watu, kama sauti ya ngurumo ya maji mengi, na kama ngurumo ya radi, ikisema, “Haleluya! Bwana ni Mungu wetu, mtawala juu ya wote, hutawala.
7 Radujmo se i kličimo i slavu mu dajmo jer dođe svadba Jaganjčeva, opremila se Zaručnica njegova!
Na tushangilie na kufurahi na kumpa utukufu kwa sababu harusi na sherehe ya Mwana Kondoo imekuja, na bibi harusi yuko tayari.”
8 Dano joj je odjenuti se u lan tanan, blistav i čist!” A lan - pravedna su djela svetih.
Aliruhusiwa kuvalishwa kitani safi na yenye kung'aa (kitani safi ni matendo ya haki ya waumini).
9 I reče mi: “Piši! Blago onima koji su pozvani na svadbenu gozbu Jaganjčevu!” I reče mi: “Ove su riječi istinite, Božje.”
Malaika akasema nami, “Yaandike haya: Wamebarikiwa walioalikwa kwenye sherehe ya harusi ya Mwana kondoo.” Vilevile akaniambia, “Haya ni maneno ya kweli ya Mungu.”
10 Padoh mu pred noge da mu se poklonim. A on će mi: “Nipošto! Sluga sam kao i ti i braća tvoja koja imaju svjedočanstvo Isusovo. Bogu se pokloni!” Jer svjedočanstvo Isusovo duh je proročki.
Nilisujudu mbele ya miguu yake nikamwabudu, lakini akaniambia, “Usifanye hivi! Mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako mwenye kuushika ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu, kwa kuwa ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii.”
11 I vidjeh: nebo otvoreno - i gle, konj bijelac, a na nj sjeo On, zvani Vjerni i Istiniti, a sudi i vojuje po pravdi;
Kisha niliona mbingu zimefunguka, na tazama kulikuwa na farasi mweupe! Na yule aliyekuwa amempanda anaitwa Mwaminifu na wa Kweli. Huhukumu kwa haki na kufanya vita.
12 oči mu plamen ognjeni, na glavi mu mnoge krune; nosi napisano ime kojeg nitko ne zna doli on sam;
Macho yake ni kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake ana taji nyingi. Ana jina lililoandikwa juu yake asilolifahamu mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe.
13 ogrnut je ogrtačem krvlju natopljenim; ime mu: Riječ Božja.
Amevaa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aliitwa Neno la Mungu.
14 Prate ga na bijelcima Vojske nebeske, odjevene u lan tanan, bijel i čist.
Majeshi ya mbinguni yalikuwa yakimfuata juu ya farasi weupe, walivalishwa kitani nzuri, nyeupe na safi.
15 Iz usta mu izlazi oštar mač kojim će posjeći narode. Vladat će njima palicom gvozdenom. On gazi u kaci gnjevne srdžbe Boga Svevladara.
Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao huyaangamiza mataifa, naye atawatawala kwa fimbo ya chuma. Naye hukanyaga vyombo vya mvinyo kwa hasira kali ya Mungu, hutawala juu ya wote.
16 Na ogrtač, o boku, napisano mu ime: “Kralj kraljeva i Gospodar gospodara.”
Naye ameandikwa juu ya vazi lake na katika paja lake jina, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA.
17 I vidjeh jednog anđela: stajaše na suncu vičući iza glasa svim pticama što nebom lete: “Ovamo! Skupite se na veliku gozbu Božju
Niliona malaika amesimama katika jua. Aliwaita kwa sauti kuu ndege wote warukao juu, “Njoni, kusanyikeni pamoja kwenye chakula kikuu cha Mungu.
18 da se najedete mesa kraljeva, i mesa vojvoda, i mesa mogućnika, i mesa konja i konjanika njihovih, i mesa svih mogućih ljudi, slobodnjaka i robova, malih i velikih!”
Njoni mle nyama ya wafalme, nyama ya majemedari, nyama ya watu wakubwa, nyama ya farasi na wapanda farasi, na nyama ya watu wote, walio huru na watumwa, wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
19 I vidjeh: Zvijer i kraljevi zemlje i vojske njihove skupiše se u boj da se zarate s Onim što sjedi na konju i s vojskom njegovom.
Nilimwona mnyama na wafalme wa nchi pamoja na majeshi yao. Walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kufanya vita na mmoja aliyepanda farasi na jeshi lake.
20 I Zvijer bi uhvaćena, a s njom i Lažni prorok koji je u njenoj nazočnosti činio znamenja i njima zavodio one što su primili žig Zvijeri i klanjali se njezinu kipu. Živi su oboje bačeni u ognjeno jezero što gori sumporom. (Limnē Pyr )
Mnyama alikamatwa na nabii wake wa uongo aliyezifanya ishara katika uwepo wake. Kwa ishara hizi aliwadanganya wale walioipokea chapa ya mnyama na walioisujudia sanamu yake. Wote wawili walitupwa wangali hai katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr )
21 A drugi su posječeni mačem što iziđe iz usta Onoga koji sjedi na konju i sve se ptice nasitiše mesa njihova.
Wale waliobaki waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa mmoja aliyepanda juu ya farasi. Ndege wote walikula mizoga ya miili yao.